Babati, Manyara: Serikali yamfutia Mashtaka ya Uhujumu uchumi Mhadhiri wa Chuo Kikuu

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Mkurugenzi wa Mashitaka ya jinai nchini l (DPP)amemfutia Mashtaka ya uhujumu uchumi yaliyokuwa yakimkabili Mahakamani mhadhiri wa Chuo kikuu cha SAUT tawi la Arusha, Subilaga Masebo na wenzake wanne.

Akiwasilisha maombi ya kuondoa shtaka hilo, mwendesha mashtaka wa serikali Lusiana Shaban ameiambia mahakama ya wilaya Babati Mkoani Manyara ,upande wa jamhuri haina Tena Nia ya kuendelea na shtaka hilo lililofunguliwa dhidi ya washtakiwa hao.

"Mheshimiwa hakimu ,kesi hii ilikuja Kwa ajili ya kusikilizwa lakini upande wa jamhuri unawasilisha Mbele Yako maombi ya kuliondoa shauri hilo mahakamani"alisema Shaban.

Alisema tunaomba kufanya hivyo kupitia kifungu Cha 91(1) Cha Sheria ya makosa ya jinai, sura ya 20 ya mwaka 2019.Tunaliondoa shauri hili Kwa hiyari bila kushurutishwa na yeyote.

Katika shauri hilo wengine waliokuwa wameshtakiwa ni Hilari Mmbando,Hemed Nyokaa, Ramadhani Hasani na Ally Juma wote wakati wa wilaya ya Babati.

Mhadhili huyo alikuwa akitetewa na wakili Kapimpiti Mgalula wa jijini Arusha baada ya kufunguliwa kesi hiyo ya jinai namba 39/2021 katika mahakama ya wilaya Mkoani Manyara, April 29,mwaka huu yeye na wenzake wakikabiliwa na mashtaka ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi kilo 40 .50 yaliyokuwa kwenye gari yake.

Akisoma uamuzi wa kuondolewa Kwa shauri hilo, Hakimu wa wilaya ya Babati Victor Kimaro alisema mahakama yake haina pingamizi na uamuzi wa serikali wa kuondoa shauri hilo mahakamani.

Alisema washtakiwa hao Kwa Sasa wapo huru kuendelea na shughuli zao kama kawaida ,Hata hivyo aliongeza kuwa upande wa mashtaka unaweza kufungua upya shauri hilo wakati wowote itakapotaka.

Akizungumza nje ya mahakama wakili Mgalula alimshukuru DPP Kwa kuwafutia mashtaka watuhumiwa wote kwani aliamini kwamba Mhadhili huyo hakuwahi kuhusika na biashara ya mirungi ukizingatia kwamba yeye ni mhadhili wa Chuo kikuu,taaluma inayoheshimika kwenye Jamii.

Naye Sublaga Masebo ambaye alikuwa mshtakiwa namba moja katika shauri hilo ,alisema katika maisha yake hakuwahi kufanya biashara ya mirungi ila kilichomponza ni kuwapatia lifti kwenye gari yake watu wasiofahamika na baada ya kusimamishwa na askari polisi Watuhumiwa walifanikiw kutoroka na yeye kukamatwa ,hivyo anashukuru mahakama kwa kumwachia huru.

Ends...
 
Which statement is correct, “guilty until proven innocent” or “Innocent until proven guilty “. Dunia hadaa ulimwengu ndio mama. Ikibidi wamuachie na hizo kilo zake 40 za gomba.
 
Nimewai mbebea mtu gongo bila kujua, bahati nzuri kumbe polisi waliishtukia ile issue kuwa nimebambikizwa ,,wakawa wanafuatilia mchezo kwa mbali.
Ile nimekabidhi wakambananisha wakamweka chini ya ulinzi.
Kesho polisi mmoja akaja ananiambia we dogo kuwa makini, jana umebebeshwa gongo wewe hujui.
Tusingekuwa tunakufahamu ungekuwa jela muda huu.
Nilishtuka ,, yule mzee nilimsaidia tu dumu lake nikajua ni la maji kumbe gongo.
 
Nimewai mbebea mtu gongo bila kujua, bahati nzuri kumbe polisi waliishtukia ile issue kuwa nimebambikizwa ,,wakawa wanafuatilia mchezo kwa mbali.
Ile nimekabidhi wakambananisha wakamweka chini ya ulinzi.
Kesho polisi mmoja akaja ananiambia we dogo kuwa makini, jana umebebeshwa gongo wewe hujui.
Tusingekuwa tunakufahamu ungekuwa jela muda huu.
Nilishtuka ,, yule mzee nilimsaidia tu dumu lake nikajua ni la maji kumbe gongo.
Hii inatokea Sana
Kuna jamaa anasafiri sana dom - dar kwa gari yake, Ila ubahili wa mafuta unamfanya ale vichwa(kupakia abiria njiani)
Si akapakia kimeo, hadi kuja kugundulika kusa hausiki kishaa jela miezi ya kutosha
 
Nimewai mbebea mtu gongo bila kujua, bahati nzuri kumbe polisi waliishtukia ile issue kuwa nimebambikizwa ,,wakawa wanafuatilia mchezo kwa mbali.
Ile nimekabidhi wakambananisha wakamweka chini ya ulinzi.
Kesho polisi mmoja akaja ananiambia we dogo kuwa makini, jana umebebeshwa gongo wewe hujui.
Tusingekuwa tunakufahamu ungekuwa jela muda huu.
Nilishtuka ,, yule mzee nilimsaidia tu dumu lake nikajua ni la maji kumbe gongo.
Tatizo mnajipendekeza sana kwa wazee kusifiwa eti mnaheshima. Utakuta hata mshua au maza homu hamwasaidii. Kazi kushinda vijiweni kusubiria wazee kupita kujipendekeza msifiwe mna heshima uchwara.

Nadhani umejifunza.
 
Tatizo mnajipendekeza sana kwa wazee kusifiwa eti mnaheshima. Utakuta hata mshua au maza homu hamwasaidii. Kazi kushinda vijiweni kusubiria wazee kupita kujipendekeza msifiwe mna heshima uchwara.

Nadhani umejifunza.
acha panic bana, huyo mzee anafahamika na familia.
Ila ni kweli nilijifunza.
 
acha panic bana, huyo mzee anafahamika na familia.
Ila ni kweli nilijifunza.
Bwana mdogo nakupa tu ushauri wa bure. Usimuamini yeyote yule jiamini wewe mwenyewe pekee yako. Utakuwa salama.

Sasa jitahidi kutafuta kazi vibaruani huko uwe busy usije kuingia mtegoni kwa kuwasaidia vigagula kubebeba madumu kwa kutafuta sifa uchwara.
 
Which statement is correct, “guilty until proven innocent” or “Innocent until proven guilty “. Dunia hadaa ulimwengu ndio mama. Ikibidi wamuachie na hizo kilo zake 40 za gomba.
Hiyo ya pili. Kawapa watu lift tu, wamebeba nini, yeye hakujua.
 
Bwana mdogo nakupa tu ushauri wa bure. Usimuamini yeyote yule jiamini wewe mwenyewe pekee yako. Utakuwa salama.

Sasa jitahidi kutafuta kazi vibaruani huko uwe busy usije kuingia mtegoni kwa kuwasaidia vigagula kubebeba madumu kwa kutafuta sifa uchwara.
Sawa bwana mzee
 
Back
Top Bottom