Baba wa taifa

collezione

JF-Expert Member
Oct 22, 2010
352
178
wana jF, leo nakuja na maoni mazito.

ni wazi kila mtu anatambua na kuthamini mchango aliotoa DR.SLAA katika kuibua na kupambana na maovu mazito, ya ufisadi. ingawaji kuna baadhi ya watu mpka leo wanamuona kama anabwa-bwaja na kupoteza muda.

ila naamini DR. anafanya hii sacrifies ngumu, si kwa ajili ya kuijongezea kipato au kwa kizazi cha leo wala kesho. but ni kwa ajili ya vizazi vijavyo. ndo maana katika kampeni zake, alishwahi kutamka kuwa "YUKO TAYARI KUPIGWA RISASI, LAKINI HATACHOKA KUPIGANA NA UFISADI".

kabla ya DR.Slaa hakuna mtu aliyewahi kuthubutu kuongelea swala la ufisadi hadaharani. ingawaji wote tulijua kuwa viongozi wetu wanadhurumu nchi yetu. na kutufanya tuwe masikini.
leo hii maelfu ya watu wamefunguliwa macho. tulikua tumelala, lakini sasa kila mtu ameamka kwa ujasiri mkubwa. na kupambana kwa style yake anayoijua.
lakini haya yote, yame-asisiwa na baba yetu SLAA.

ni kwa-ajili hiyo basi sina budi kusema, DR.SLAA ndiye shujaa wa kizazi hiki cha TAnzania.
huyu ndiye baba mpya wa taifa, aliyejitolea kupigana kufa na kupona, kwa ajili ya manufaaa ya watanzania.
kama ilivyo martini luther king jr, wa marekani. DR. SLAA atakumbukwa milele na wajukuu na vitukuu vyetu..sio TANZANIA tu bali duniani kote.
DR SLAA hatasaulika kwa watanzania, maana yeye ndo ailyetoa nuru mpya na kuleta tumaini jipya.
kwa kupigana na dhuruma inayoletwa na viongozi, ambao tumewapa dhamana ya kutuongoza.

asanteni
 
Back
Top Bottom