Baba wa Taifa hakumtendea haki Kikwete, Ndio maana tuko hapa tulipo?

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674
Kama taarifa hii ni kweli wakati JK akiwa Mwanafunzi wa elimu ya siasa chuoni Monduli,alipowasilisha taarifa yake kwa Baba wa Taifa Mwalimu JK Nyerere,na kisha Baba wa Taifa kuukabidhi waraka huo kwa wakuu wa kijeshi wa JK ukiwa kama ulivyo pasipo kuficha jina au utambulisho wa mtoa taarifa.Hakika tendo hilo halikuwa sawa hata kidogo na ndio chanzo na tatizo la sura ya utawala huu tulionao sasa,ambao uliacha kovu moyoni mwa mhusika ambae kwa hakika kwa kuwa alichokiwakilisha kilikuwa ni kweli kulingana na siasa za ujamaa [Comrade System] na kujikuta anaingia matatizoni na kumuacha akishindwa kujua msimamo wa Itikadi ambayo ametumwa kuisambaza na kuitetea.

Namheshimu sana Baba wa Taifa mpaka hapo alipotufikisha,lakini nae pia anayo yake ambayo yamechangia pia kutufikisha hapa tulipo leo hii.Kitendo cha Mwalimu kutoa taarifa hile ya JK kwa Wakuu wa Jeshi ikiwa na jina la Mhusika au mleta taarifa kilikuwa ni UCHONGANISHI, japo kwa upande wake pia hatujui kama alikujua kama Mkuu wa Majeshi uenda angeipeleka kama ilivyo eneo tajwa na mtoa taarifa [Ukizingatia upeo wa Elimu wa Wakuu wa Jeshi wa zama hizo].

Kikwete kama kijana mdogo ambae aliitaji kuongozwa kupitia wakubwa wake ukizingatia unyeti wa kazi yake,lakini the Court break become the court breaker. Hatimae songombingo hilo la wakuu wake na songombingo la wanafunzi wenzie wa kitaaluma wa kada ya kijeshi ambayo yeye alisimama katika kada ya siasa, vilimshape na kumuweka katika hali tata sana kisaikolojia.Na hata dhamira yake kusimama kama Rais wa Nchi hii siku moja kwa kusudio la kujenga kile ambacho alikiona na kuamini toka ujana wake akifikilia kuwa angeweza, lakini kumbe sivyo kulingana na mfumo [system].Lakini kwa kuwa mambo yale yale ya the Court Break become the Court Breaker pamoja na kuibuka kwa Azimio la Zanzibar, yale ya kule chuo yalikuwa yamekwisha sambaa sehemu kubwa ya Nchi yetu na idala nyingi za Serikali.

Tufike sehemu tukili kuwa tunahitaji watu jasiri ambao kwanza hawakuwepo kwenye zama za kumjua huyu alikuwa nani,watakao wasulubu hata rafiki zao endapo wametenda ndivyo sivyo,lakini kwa style ya Jakaya Kikwete kila akikumbuka aliko toka na njia alizopita na mafairi yanayopita mikononi mwake yakiwa na taarifa kadha wa kadha juu ya wale wale aina ya viongozi waliokuwa chini ya Mwalimu ambao kwake ni senior toka akiwa kijana anakosa nini cha kufanya.

Kwangu mimi yeye nilipenda kuona kuwa anakuwa Free Mind Man,alipofika yeye hadhi yake kama Rais hana wa kuwajibika kwake bali kusimamia kile ambacho anakiamini pasipo kuhesabu yaliyopita huko nyuma.Kwa kuwa yaliyotokea kwake MUNGU ALIKUWA NA SABABU NAE NDIO MAANA AKAWA RAIS ILI MUNGU AFIKISHE UJUMBE KWA WALE WOTE WALIOMTENDEA YALIYOPITA, AKIWA NA DHAMIRA YA KWELI KWA MUJIBU WA ITIKADI YA WAKATI HUO.

Lakini nae kageuka kuyafungia macho hayo na hakika nae woga huo ataulipia kwa style ya namna yake.
Atuthibitishie kuwa Mwalimu hakumtendea haki.Nasi tutapata cha kujifunza na watu kutambua haya tuliyonayo ni matokeo ya historia ya yale yaliyotokea kwake pia asisahau kutuandikia kitabu haswa sisi vijana wa kizazi kipya ambao tutajifunza kupitia kitabu hicho.

NINA MUHESHIMU BABA WA TAIFA MWALIMU JK NYERERE, LAKINI KWA HILI MWALIMU HAKUMTENDEA HAKI HATA KIDOGO?

Nawasilisha
 
Mnafiki utamtendea haki gani; lazima umtose na unafiki wake ndio dawa anayostahili!!
 
Sielewi kilichaoandikwa hapa. I think there is a lot of background information missing. Improve your writing skill. Actually I don't see anything that was done to JK in here.
 
Mnafiki utamtendea haki gani; lazima umtose na unafiki wake ndio dawa anayostahili!!

Naomba kujua unafiki wake ni upi mkuu?nijuze manake ndio tunaelimishana hivyo?
 
Sielewi kilichaoandikwa hapa. I think there is a lot of background information missing. Improve your writing skill. Actually I don't see anything that was done to JK in here.
Kipi kisichoeleweka hapa?
 
sielewi alichafanya nyerere kwa jk ambacho sio haki ni nini????????
The Boss,
Nadhani jamaa ana refer ile incident ambapo Kikwete is alleged to have written to Mwalimu complaining about Sayore feeding the soldiers with produce from his farm. Mwalimu inasemekana alimkabidhi Msuguri hiyo barua akisema suala hilo lishughulikiwe huko huko jeshini ( as it should have been) And the end result was that Kikwete was forced to escape from Monduli without finishing his courses. Sasa hapo mwenye kosa nani?
 
Mkuu nafkiri unareffer enzi za Sayore akiwa Mkuu wa chuo cha jeshi Monduli na JK akiwa kada wa siasa Monduli. Mkuu Sayore alijipa tender ya kusupply yeye mwenyewe chakula na vitu vingine pale chuoni, tena kwa kujipangia bei ya hizo bidhaa, halafu hapohapo anakuja kuhalalisha malipo kama mkuu wa chuo. Yani yeye ndio muuzaji na mpanga bei, halafu yeye ndiye muidhinishaji wa malipo kwa upande mwingine.

Kitu ambacho kwa enzi hizi za leo kingepigiwa kelele mpaka mbingu kupasuka!

Jk akiwa Kada wa siasa, alimuandikia Mwalimu waraka wa siri kumjulisha juu ya hii anomally pale chuoni. Alichofanya Mwalimu, badala ya kuchukua hatua dhidi ya Sayore ambaye alikua amekiuka maadili ya ujamaa kipindi kile, akampelekea barua kama ilivyo Sayore, na hivyo kumuumbua Jk.
Habari zinadai mkuu ilibidi atumie mafunzo ya mbinu za medani kutoroka pale chuoni.

Binafsi kama hii story ni kweli kama ilivyosimuliwa, naona Mwalimu hakutenda haki kwa Jk.

Ila naomba nisikubaliane kwamba lile jungu alilofanyiwa na Mwalimu ndiyo inayomfanya mpaka sasa ashindwe kuwa Rais mwenye msimamo usioyumba... Yeye ndiye rais, the buck stops with him, there are no excuses for inaction under his watch!
 
DSN.....DSN..DSN..........

hii habari tuliwahi kuichambua humu mezi wa pili kama sikosei....Nyerere alikuwa sawa kabisa ....hakutaka majungu jk ni mtu wa majungu sana .uamzi wa mmwl kuirudha ile barua kule ilikuwa ni kuwaonyeha wale wakuu wa monduli kama ni kweli maana malalamiko yalitoka pale monduli na si kwingine........kama alijua dhamira yake ilikuwa safi kikwete asingetoroka na kutembea kwa mguu akipitia vichakani na amshukuru shimbo aliyekutana nae njia na kumwandikia ni meseji ili apeleke kwa mjomba wake pale tengelu ili jk aweze kupata hifadhi ya kijamii pale...


kingine kumbuka haya yanayotoke loe ni matokeao ya tabia ya kikwet ya ndani kabisa toka zamani huyu mtu yuko hivi...ni mtu asiyejali wenzake...hasaidii wenzake...ana wivu..ana uchu...muongo....hapendi wenzake wafanikiwe ..... hana msimamo..hana kiasi..hana maamuzi .....mwanaume wa ukweli huwa anapenda wenzake wafanikiwe ..hyu hapana ..hana sifa hizo....

ndio maana sayore aliuliz mara tatu mle nda ni nani haridhiki ? jk alikuwemo humo ndani lakini hakusmama kuleleza duku duku lake.....hadi pale alipoumbuliwa .....ana baahai yake baada ya kutoka tengeru kw mjomba wake shimbo alirudi bagamoyo hadi pale alipopigiwachapuo wakubwa na kupelekwa huku kusini kufanya kazi ya tanu

nyerere alimjua vizuri huyu mtu na ndio maana mwaka 1995 yule mzee alisema..''mimi sio kuku sitagi mayai lakini ukinipa yai bovu nitaligundua'' kauli hii ilimlenga jk moja kwa moja....na pia akaongeza jk bado hhuwezi kuongoza nchi'' yule mzee alimkataa kata kata maana alijua tabia ya huyu jk..........
 
taarifa yenyewe hii hapa


1. Kipindi hicho mkuu wa chuo alikuwa Gideon Sayore, Kikwete alikuwa ni mmoja wakufunzi wa siasa chuoni hapo.

Sasa ilikuwa hivi,
Mzee Sayore alikuwa anafuga ng'ombewengi pamoja kufanya shughuli za kilimo kwawingi wakati huohuo akiwa mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli.

Hivyo basi baada ya kuona ng'ombe wanatoa maziwamengi mno na mazao yametapakaa mashambani,. akaamua kuwa awe analiuzia jeshi mazao kama vile maharage na mahindi pamoja na maziwa na nyama kutoka kwenye mifugo yake.......na pesa anachukua yeye mwenye mazo.

Aliendelea kufanya hivyokwa kipindi kirefu tu.. ikiwa ni kama sehemu yake ya maisha....

Sasa bwana ,,kumbe Kikwette (JK) ilikuwa inamuuma sana sana, yaani mno! sasa haieleweki kama ilikuwa kweli ni kwa uzalendo ua wivu tu....akaandika barua kwa raisi kipindi hicho JK Nyerere.

Katika barua hiyo akaandika lawama nyiingi mno na majungu mengi sana dhidi ya Sayore, akimwita bepari, bwenyenye, mnyonyaji n.k huku akisema hafai kuwa mkuu wachuo hicho kwakuwa navunja miiko ya uongozi na mambo mengine meengi (si mnamjua JK anavyojua kupiga fitna!)...

Basi bwana, akamalizia mwisho kwakujiandika jina lake na sahihi yake huku akijiita mzalendo kamili barua ikapostiwa ikiwa imeadresiwa kwa rais wa nchi wakati huo!......

Mwalimu, aliipata barua ile aliifungua akaisomaaaa kisha akapiga hesabu zake....sijui aliwaza nini mzee yule, akaihifadhi ile barua ikaa sana ofini kwake bila kuchukua uamuzi wowote.

Siku moja alipokuja mkuu wa majeshi wakati huo "General Mtukula" (David Musuguli) ofisini kwa Mwalimu eaisi kipindi hicho, mwalimu akampa ile barua kutoka kwa Kikwete "akisema hayo ni maMbo yenu kayamalizeni hukohuko".

Basi bwana ile barua Mkuu wa majeshi alikaa nayo muda hivi kwenye makabrasha yakee...., sasa siku mija alikuja Mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli(Sayore) Dar es salaam kufanya shughuli za kikazi akaenda hadi ofisini kwa Mkuu wa majeshi.

Baada ya shughuli kwisha na Sayore akiwa anajiandaa kwenda Monduli Mkuu wa majeshi alimwita, akampa ile barua ya Kikwete aliyomwandikia rais!!....

Sayore akaisoomaaa we akashangaa mno!! na akafura kwa hasira yule mmasai...., akuliza mwalimu kasemaje? Akaambiwa mwalimu kasema yamalizeni wenyewe!!.... Akasema naam, na akaondoka na ile barua hadi Monduli...

Alipofika tu yule mmasai aliitisha kikao cha wakufunzi wote na wakuu wengine pale chuoni, wakati wanajikusanya kwenda kwenye chumba cha mkutano yeye aliamua kwenda kutoa copy ile barua ya Kikwete, kopi nyingi idadi sawa na wajumbe wa mkutano ule....

Alipoingia mkutanoni akawaona wakuu na wakufunzi wote wameketi wakimsubiri wajue alicho waitia,.. akaanza kwa kuwauliza..jamani kama kuna mtu ana matatizo, au anaona kuna jambo haliendi sawa anyooshe mkono na saemekinacho mkereketa......watu wote wakawa kimya huku wengine wakisema hamna mkuu akiwemo Kikwette!!!

Basi bwana, tumalizie mkasa huu wa ******...

Sayore akaanza kuwagawia zile nakala (copies) za ile barua ya Kikwete kwenda kwa rais akawagawia wooote including Kikwete!!! Huku yule mmasasi Sayore akiwa amefura kwa hasira, macho mekunduuu! Akagonga ngumi juu ya meza kwa hasira na kusema someni hiyo barua!! kisha akatoka na kusema anakuja muda si mrefu...

Hapo Kikwete akajua kifo chake kimefika, akikumbuka macho ya yuile mmasai! akatetemeka macho yakamtoka lip! kwa woga!.. na wenzie wakamwanzishia zogo mle ndani......

Alichokifanya ni kuondoka haraka pale kikaoni wenzie wakajua bado yupo chuoni, kumbe safari ya Dar ikawa imeanza...!! Jamaa alitembea uchochoroni kwa muda mrefu sana huku akiogo kabisa kuingia barabara ya kuu...

Mashuhuda wanasema yule bwana akaja kupanda lift ya gari za vyama vya ushirika maeneo ya USA RIVER, hakukumbuka kubeba mzigo wowote!! Just imagine kutoka Monduli hadi hapo jamaa aliteseka sana... lakini yeye hakujali, cha muhimu ilikuwa kusalimisha maisha yake......

Basi huo ndiyo ukawa mwisho wa JK Monduli,........... hukurudi akaja Dar na kupangiwa kazi nyingine na chama... lakini alikuwa anamlaani sana Nyerere eti kwanini alimfanyia vile!!

Hicho ndicho chanzo cha JK kumchukia mwalimu na kugoma katakata kumwita baba wa taifa hadi leo! Yeye humwita mzee Nyrere tu au mwalimu baasi...na mara chache akiwa nje ya nchi humwita 'Father of our Nation', lakini ni pale anapotaka kupigiwa makofi kwa nukuu za Mwalimu....

**Ndugu zangu hiki ni kisa cha ukweli kwa 100%, inawezekana uandishi wangu ukawa na upungufu, lakini niemekipata kutoka watu mbalimbali waliowahi kuwa karibu sana na mkasa huu...
 
sielewi alichafanya nyerere kwa jk ambacho sio haki ni nini????????

Kuexpose Identity ya Jakaya Kikwete Kwa Makamanda wake wakati anajua kuwa yule ni junior,na kuwa alichofanya kama kijana ambae anafundishwa kuwa mjamaa anamuona Kiongozi katika style ile ya kimaisha nae anatumia wajibu wake wa kijamaa kupeleka taarifa kwa mkuu wa chama na ambae ndiye Rais wa Nchi.Kisha kiongozi huyo ambae ni Rais anaitoa taarifa hiyo kwa makamanda wake pasipo kuficha utambulisho [Identity] ya mtoa taarifa hakika kwa usalama wa mtoa taarifa ni kitendo kibaya na hatari.

Kupitia hayo na mengineyo ambayo hayajasemwa hapa kwa kuwa wenyewe bado wapo si vyema kuyasema muda ukifika watu pia watajua.Hakika kama binadamu mwingine yoyote ni hakika yalimpa historia ambayo leo watu wanalalamika juu ya utawala wake,lakini kupitia experince ya matukio hayo yamemshape hivi alivyo leo.Yamemtengeneza kuwa mwoga juu ya maamuzi.
 
Sielewi kilichaoandikwa hapa. I think there is a lot of background information missing. Improve your writing skill. Actually I don't see anything that was done to JK in here.

Yaani ata mimi sijaelewa kitu! huyu mwandishi ni kanjanja tu. Sasa kuna faida gani ya kufichaficha habari? alafu inaonekana kama mtu aliyekata na kupaste.
 
DSN.....DSN..DSN..........

hii habari tuliwahi kuichambua humu mezi wa pili kama sikosei....Nyerere alikuwa sawa kabisa ....hakutaka majungu jk ni mtu wa majungu sana .uamzi wa mmwl kuirudha ile barua kule ilikuwa ni kuwaonyeha wale wakuu wa monduli kama ni kweli maana malalamiko yalitoka pale monduli na si kwingine........kama alijua dhamira yake ilikuwa safi kikwete asingetoroka na kutembea kwa mguu akipitia vichakani na amshukuru shimbo aliyekutana nae njia na kumwandikia ni meseji ili apeleke kwa mjomba wake pale tengelu ili jk aweze kupata hifadhi ya kijamii pale...


kingine kumbuka haya yanayotoke loe ni matokeao ya tabia ya kikwet ya ndani kabisa toka zamani huyu mtu yuko hivi...ni mtu asiyejali wenzake...hasaidii wenzake...ana wivu..ana uchu...muongo....hapendi wenzake wafanikiwe ..... hana msimamo..hana kiasi..hana maamuzi .....mwanaume wa ukweli huwa anapenda wenzake wafanikiwe ..hyu hapana ..hana sifa hizo....

ndio maana sayore aliuliz mara tatu mle nda ni nani haridhiki ? jk alikuwemo humo ndani lakini hakusmama kuleleza duku duku lake.....hadi pale alipoumbuliwa .....ana baahai yake baada ya kutoka tengeru kw mjomba wake shimbo alirudi bagamoyo hadi pale alipopigiwachapuo wakubwa na kupelekwa huku kusini kufanya kazi ya tanu

nyerere alimjua vizuri huyu mtu na ndio maana mwaka 1995 yule mzee alisema..''mimi sio kuku sitagi mayai lakini ukinipa yai bovu nitaligundua'' kauli hii ilimlenga jk moja kwa moja....na pia akaongeza jk bado hhuwezi kuongoza nchi'' yule mzee alimkataa kata kata maana alijua tabia ya huyu jk..........

Mkuu Edson ebu vaa viatu vya huyu jamaa na wewe ndio junior [UJANA] over ambitious kama kada ulietumwa kueneza siasa sio mbinu za kivita kisha unayakuta ya Mkuu yuke unatoa taarifa zako kisha wanakukaanga.To be frank leo hii mnamkubali Zitto,nina hakika Jakaya wakati huo alikuwa ni zaidi ya zitto kwa kuwa kumbuka ulikuwa ni mfumo wa chama kimoja.Matendo ya Zito kufumua uchafu tunaoukubali sasa unatofauti gani na wakati huo kwa itikadi hiyo ya ujamaa na masharti yake ambayo kwa wakati huo huyu kama kijana yalikuwa kichwani kama saa na mkono.
 
Yaani ata mimi sijaelewa kitu! huyu mwandishi ni kanjanja tu. Sasa kuna faida gani ya kufichaficha habari? alafu inaonekana kama mtu aliyekata na kupaste.

Ni vyema ukawa msikivu ili kujua,sio lazima kuchangia usichokijua.
 
Mkuu Edson ebu vaa viatu vya huyu jamaa na wewe ndio junior [UJANA] over ambitous kama kada ulietumwa kueneza siasa sio mbinu za kivita kisha unayakuta ya Mkuu yuke unatoa taarifa zako kisha wanakukaanga.To be Frank leo hii mnamkubali Zitto,nina hakika Jakaya wakati huo alikuwa ni zaidi ya zitto kwa kuwa kumbuka ulikuwa ni mfumo wa chama kimoja.Matendo ya Zito kufumua uchafu tunaoukubali sasa unatofauti gani na wakati huo kwa itikadi hiyo ya ujamaa na masharti yake ambayo kwa wakati huo huyu kama kijana yalikuwa kichwani kama saa na mkono.
Kosa alilofanya Kikwete ni kukiuka hierarchy ya kijeshi. Hakupaswa kumwandikia Mwalimu. Angemwandikia mkuu wa jeshi halafu tatizo hilo lishughulikiwe katika ngazi hiyo. Unless uniambie kuwa jeshi halina taratibu zake kuwawezesha maafisa wa ngazi za chini kutoa malalamiko yao.
 
Back
Top Bottom