Baba V anamtaka madame B

Chimbuvu

JF-Expert Member
Jul 17, 2012
4,401
2,333
Kwenda kwa:kamati kuu ya mahusiano chitchat
copy: Baba V,
copy: Judgement Mamndenyi BADILI TABIA,
yah:kutokua na imani na mwenyekiti wa mahusiano chitchat Baba V.



Rejea kichwa cha habari hapo juu chahusika,nikiwa pamoja na mwenzi wangu Madame B,tunasikitika kutokana na tabia ama kauli za kidikteta anazozileta mwenyekiti kwa kuona yupo juu ya sheria.mojawapo ya baadhi ya sababu zinazotupa wasiwasi ni kama zifuatazo,
1.toka tumetangaza tuna mahusiano,amekuwa mstari wa mbele kutaka kuvuruga ama kuuvunja uhusiano wetu na Madame B,kwa kuzusha tuhuma mbalimbali,
2.amekuwa ana nia ya kuvunja mahusiano na sio kusuluhisha kwa kuwa anakuja katika usuluhishi akiwa na jibu na uamuzi tayari
3.toka ameanza kutufuatilia tumeshindwa kuelewa ni yeye ndiye anayeleta malalamiko akidai ameletewa na mtu anayejiita Ruttashobolwa,ilhali hatujawahi kuona huyo mtu akitamka hadharani
4:mwenzi wangu Madame B alishatamka kuwa hamtaki na wala hampendi mtu anayejiita Ruttashobolwa lakini mwenyekiti amejifanya kama hakuona hiyo statement
5.sababu inayotupa mashaka ni kuwa barua niliyoituma katika kamati ya screening ameidharau na amewadharau wanakamati hiyo kwa kuwa hakusubiri wakae kikao na kuamua kujichukulia hatua mikononi kwa kujiona yupo juu ya sheria
ninaomba kuupitia kamati hii mwenyekiti aweke vithibitisho vifuatavyo,malalamiko ya ndugu Ruttashobolwa,na taarifa rasmi aliyoletewa na kamati ya screening kama anavyojaribu kuuhadaa umma wa wanachitchat watuone sisi ni wabaya.
Pia kwa muonekano dhahiri inaonyesha kuwa mwenyekiti Baba V anamtaka mwandani wangu Madame B ndio maana ananishinikiza niutangazie umma kwamba nimemuacha ili nikishatangaza yeye apate sababu ya kimaandishi ya kutumia ili yeye ampate janja yake tumeishtukia.
Na swali analotakiwa kujibu Baba V ni ndoa ipi ambayo mwanaume hajui mke wake analala wapi,anavaa nini,anakula nini kwa muda mrefu?kwa sababu anajua fika ktk umri alionao bado anakaa kwa wazazi na alimuona Madame B anakaa katika nyumba yeye mwenyewe ameona atumie huo mwanya ili akaishi na mwandani wangu.
Ndugu wanakamati,mpenzi wangu Madame B sikumfuata katika nyumba ya mtu anayejiita Ruttashobolwa la,bali nilimkuta katika nyumba moja yeye mwenyewe na ndipo nilipomwaga sera zangu naye akazikubali,.
Kutokana na hayo machache naomba kamati iitishe kikao cha dharula kuangalia mwenendo mzima wa mwenyekiti kwa kuwa kila dalili inaonyesha kuna mchezo mchafu unafanyika na ambao wanaujua ni Baba V na Ruttashobolwa.HAKI IPO WAPI KAMA NA MWENYEKITI ANAANZA KUZENGEA WACHUMBA WETU,JE KWA WASIO NA UWEZO WATASALIMIKA?
Asanteni
Chimbuvu & Madame B
 
Last edited by a moderator:
Wewe Wasema hivyo,na punde tutaanza kukupigia kura za kutokuamini

Have you checked the grounds well,??? angalia tu kila kauli zako unazotoa na uweke kumbukumbu sahihi kwa ajili ya baadae
 
Sikuwa na haja ya kupiga kelele nilicho fanya nikupeleka malalamiko yangu kwa kamati husika na imefanyia kazi!

Tuhuma unazo zielekeza kwa mwenyekiti ni ushahidi hazina ushahidi bali ni kutafuta huruma ya kamati!

Jaribu kufata utaratibu, huwezi ukafunga ndoa bila kuvunja ndoa ya awali.
 
Kweli madameB kweli kaoga ya baharini, mbona mnajigonga sana, alafu Arushaone na Baba V wote hawa ni watu na mpakani mwa tz na kenya au mnataka kumfanyia nini mtoto wa mwanamke mwenzetu.
 
Last edited by a moderator:
Ningekuona mwenye busara kama ungetamka hadharani na unayedai ni mke wako akiri hadharani,

Sikuwa na haja ya kupiga kelele nilicho fanya nikupeleka malalamiko yangu kwa kamati husika na imefanyia kazi!

Tuhuma unazo zielekeza kwa mwenyekiti ni ushahidi hazina ushahidi bali ni kutafuta huruma ya kamati!

Jaribu kufata utaratibu, huwezi ukafunga ndoa bila kuvunja ndoa ya awali.
 
Ningekuona mwenye busara kama ungetamka hadharani na unayedai ni mke wako akiri hadharani,

Ndio maana tukaunda kamati dogo, siku nyingine unapoingia mahali pageni uwe unauliza taratibu, sasa hii itakula kwako kwa kutaka taratibu zikiukwe ili ufanikishe azma yako. bado tupo
 
Mmmmhhhh ama kweli kua uyaone,wanaume mnamgombea madame B utadhani mpira wa kona? Kunani? Madame B embu nitonye siri yamafanikio yako maana si bure.
 
Last edited by a moderator:
Mmmmhhhh ama kweli kua uyaone,wanaume mnamgombea madame B utadhani mpira wa kona? Kunani? Madame B embu nitonye siri yamafanikio yako maana si bure.

Bishanga huyu mtoto alieleta uzi huu ana hasira na tume yangu baada ya kuvunja uhusiano wake na Madame B kwani yule bado ni mke wa rutta , sasa kwa hasira na frustrations dogo kaja na uzi huu kwa dhana ya MKIMWAGA MBOGA..........., hajui kuwa hiyo theory hai apply katika baadhi ya mazingira. Haya sasa ugali unaliwa hata kwa chumvi
 
Last edited by a moderator:
This drama has to come to its terms...jamani eenh hebu wekeni mambo yenu sawa kabla sijakasirika
 
Back
Top Bottom