Baba na mama wanapoachana na kila mmoja kuoa na kuolewa, nani mwenye nguvu ju ya mali

Mr. Masasi

Member
May 12, 2011
53
4
Nahitaji msada wenu jamani, mimi ni mmoja kati ya watoto sita tuliozaliwa na baba yetu pamoja na mama yetu wakiwa ndani ya ndoa. Lakini walitengana mara baada ya baba yangu kuwa na nyumba ndogo ambako alifanikiwa kuzaa watoto watatu, mara tu baada ya mama yngu kuligundua hilo aliamua kuondoka kwenye mji wake na kwenda kuolewa na yeye na kufanikiwa kuzaa watoto wawili, baadae mume wake na mama ambaye ni baba yngu wa kambo alifariki. Alipofarik mama aliamua kurudi kwenye mji wake ambao aliukimbia, yaani nyumban kwetu. Kwa bahati mbaya sisi watoto wake wote sita hatukubahatika kupelekwa shule na baba yetu pamoja na kwamba baba alikuwa mtumishi na kuna mali ambayo ingetosha kutusomesha, lakin watoto ambao baba alizaa nje ya ndoa wote amewasomesha. Sasa kwa sasa mara bada ya mama kurudi kwenye mji wake akawa amepiga marufuku ile mali yote kutumika kuhudumia familia ndogo ya baba ambapo bado anaish na huyo mke wake mdogo. Baba bada ya kuzuiwa kuchukua mali kutoka kwetu maisha yamemgonga hana uwezo tena wa kuhudumia tena familia hyo, amekimbilia mahakan na amefungua kesi akidai anataka kugawa mali kwa wanae. Sasa kisheria hapo inakuaje mana wazazi wote hakuna aliyefariki, mama hataki ile mali igawanywe, tukiwa tunampa suport sisi wanae wanne, wakike watatu na wakiume ni mimi tu, kiukweli baba mi simkubal, harafu baba anapewa suport na watoto wawil wakiume kwan nao wanataka mali igawanywe na wanamfeel dingi. Je kisheria twaweza itaka mahakama tupige kura mana ss tuko wengi najua tutawashinda tu. Na sheria inasemaje ili kumlinda mwanamke yani mama yetu. Nipeni ushauri mana mi ndo msemaji mkuu pale mahakamani harafu ndo kama wakili harafu elimu ya sheria sina . Natanguliza shukran kwa wanasheria wote
 
duh pole sana hizi ndoa za mitala hizi.....
ngoja tuone wanasheria watasemaje....
 
Nahitaji msada wenu jamani, mimi ni mmoja kati ya watoto sita tuliozaliwa na baba yetu pamoja na mama yetu wakiwa ndani ya ndoa. Lakini walitengana mara baada ya baba yangu kuwa na nyumba ndogo ambako alifanikiwa kuzaa watoto watatu, mara tu baada ya mama yngu kuligundua hilo aliamua kuondoka kwenye mji wake na kwenda kuolewa na yeye na kufanikiwa kuzaa watoto wawili, baadae mume wake na mama ambaye ni baba yngu wa kambo alifariki. Alipofarik mama aliamua kurudi kwenye mji wake ambao aliukimbia, yaani nyumban kwetu. Kwa bahati mbaya sisi watoto wake wote sita hatukubahatika kupelekwa shule na baba yetu pamoja na kwamba baba alikuwa mtumishi na kuna mali ambayo ingetosha kutusomesha, lakin watoto ambao baba alizaa nje ya ndoa wote amewasomesha. Sasa kwa sasa mara bada ya mama kurudi kwenye mji wake akawa amepiga marufuku ile mali yote kutumika kuhudumia familia ndogo ya baba ambapo bado anaish na huyo mke wake mdogo. Baba bada ya kuzuiwa kuchukua mali kutoka kwetu maisha yamemgonga hana uwezo tena wa kuhudumia tena familia hyo, amekimbilia mahakan na amefungua kesi akidai anataka kugawa mali kwa wanae. Sasa kisheria hapo inakuaje mana wazazi wote hakuna aliyefariki, mama hataki ile mali igawanywe, tukiwa tunampa suport sisi wanae wanne, wakike watatu na wakiume ni mimi tu, kiukweli baba mi simkubal, harafu baba anapewa suport na watoto wawil wakiume kwan nao wanataka mali igawanywe na wanamfeel dingi. Je kisheria twaweza itaka mahakama tupige kura mana ss tuko wengi najua tutawashinda tu. Na sheria inasemaje ili kumlinda mwanamke yani mama yetu. Nipeni ushauri mana mi ndo msemaji mkuu pale mahakamani harafu ndo kama wakili harafu elimu ya sheria sina . Natanguliza shukran kwa wanasheria wote

Kisheria hakuna mwenye nguvu. Wakati wa kutengana mali hugawanywa nusu kwa nusu na kila moja kuchukua hamsini zake. Kutokana na wao kuachana bila talaka kunaweza kufanya hiyo ndoa bado halali kwa hiyo inategemea mazingira yakoje. Je, walioana wapi mahakamani, kanisani au msikitini. Talaka ilitolewa? unatakiwa umpate mtu ambaye anafahamu sheria za ndoa akusaidie vizuri kutokana na mazingira yenu.
 
poleni sana kwa miparaganyiko hiyo. wewe mtoto wa kiume, inaeleweka kumkasirikia babako kwa sababu ya kumuumiza mama yako. lakini kumchukia ni neno zito,muangalie kama baba aliyekuleta duniani. hiyo ni amri ya Mungu kaka,tena yenye ahadi ya kuongezewa siku za kuishi. ngoja wajuba waje,mie layman, lakini nadhani wakitalikiana inaweza kusaidia wagawane mali kila mtu aende zake. ni-pm mkoa uliopo nikutaftie ofisi zinazotoa msaada wa kisheria bure kwa wanawake ili umpeleke mama. kila la kheri,Mungu awapiganie
 
Pole sana ndugu. Kwa kifupi katila mali walizochuma wanandoa hao kila mmoja anastahili gawio (share) baada ya kupeana talaka. Lakini aina ya ndoa waliofunga ( kanisani,msikitini,kimila au serikalini) inamchango mkubwa juu ya namna ya kugawana mali hizo.Pia wataangalia kuna watoto wangapi wa ndoa wasioweza kujitegemea na kwamba hao watoto wasioweza kujitegemea watakaa na nani baada wanandoa kupeana talaka, kwa baba au mama. Hivyo kugawana mali vigezo ni vingi.Watoto wa nyumba dogo watalidhi fungu la baba na mali aliyochuma akiwa na mama yao. Vilele mimi binafsi nakushauri usijenge chuki kupita kiasi kwa baba badala yake wewe uwe msaada kwao wazazi waachane salama kama kusameheana na kurudiana imeshidikana, pia uwe makini na mahakama zetu usidanganyike kwa rushwa .Zaidi ya yote fanya kazi kwa bidii na muombe Mola akujalie maisha mema.
 
Pole sana, ila hao walitengana kienyeji wakati wao ni wanandoa regardless ndoa imefungwa wapi, tunaomba uwe wazi uko mkoa gani ili tukuelekeze wapi uende ili upate msaada wa kisheria
 
Loh, pole sana, wewe kaa kati wasaidie kisheria, napata kigugumizi, all the best.
 
Kaka mi cjui mana ya ku-pm, lakini napatikana mkoa wa shinyanga, kesi iko mahakama ya wilaya shy na itasomwa tarehe 12 mwezi ujao. Napatikana kwa namba 0757 922293 au 0658922293. Ahsanten ndugu nahitaji sana mawazo yenu
 
Nahitaji msada wenu jamani, mimi ni mmoja kati ya watoto sita tuliozaliwa na baba yetu pamoja na mama yetu wakiwa ndani ya ndoa. Lakini walitengana mara baada ya baba yangu kuwa na nyumba ndogo ambako alifanikiwa kuzaa watoto watatu, mara tu baada ya mama yngu kuligundua hilo aliamua kuondoka kwenye mji wake na kwenda kuolewa na yeye na kufanikiwa kuzaa watoto wawili, baadae mume wake na mama ambaye ni baba yngu wa kambo alifariki. Alipofarik mama aliamua kurudi kwenye mji wake ambao aliukimbia, yaani nyumban kwetu. Kwa bahati mbaya sisi watoto wake wote sita hatukubahatika kupelekwa shule na baba yetu pamoja na kwamba baba alikuwa mtumishi na kuna mali ambayo ingetosha kutusomesha, lakin watoto ambao baba alizaa nje ya ndoa wote amewasomesha. Sasa kwa sasa mara bada ya mama kurudi kwenye mji wake akawa amepiga marufuku ile mali yote kutumika kuhudumia familia ndogo ya baba ambapo bado anaish na huyo mke wake mdogo. Baba bada ya kuzuiwa kuchukua mali kutoka kwetu maisha yamemgonga hana uwezo tena wa kuhudumia tena familia hyo, amekimbilia mahakan na amefungua kesi akidai anataka kugawa mali kwa wanae. Sasa kisheria hapo inakuaje mana wazazi wote hakuna aliyefariki, mama hataki ile mali igawanywe, tukiwa tunampa suport sisi wanae wanne, wakike watatu na wakiume ni mimi tu, kiukweli baba mi simkubal, harafu baba anapewa suport na watoto wawil wakiume kwan nao wanataka mali igawanywe na wanamfeel dingi. Je kisheria twaweza itaka mahakama tupige kura mana ss tuko wengi najua tutawashinda tu. Na sheria inasemaje ili kumlinda mwanamke yani mama yetu. Nipeni ushauri mana mi ndo msemaji mkuu pale mahakamani harafu ndo kama wakili harafu elimu ya sheria sina . Natanguliza shukran kwa wanasheria wote

Ingawa kisheria hairuhusiwi kuizungumzia kesi ambayo ipo mahakamani. Lakini kujua kama walifunga ndoa ya aina gani (kkiislamu, kikristo au kimila) na je walikuwa na cheti cha ndoa, Na vile vile watoto wana vyeti vya kuzaliwa (je viliandikwa jina kamili la baba na mama) , na kama walitalikiana lini na kuna docs zozote kuthibitisha hilo.

hayyo ndio mambo ya msingi katika kujenga hoja zenu mahakamani na pasi na shaka mtafikia muafaka.

Pole sana
 
Back
Top Bottom