Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,510
- 23,722
Wadau kuna siku nipo nafanya service garage fulani mara na baba mkwe naye akatia team amekuja fanya garage hapo hapo. Wametengeneza mara kuna spare inahitajika na amepungukiwa 190,000.
Akanambia nimwazime 250,000. Nikamwazima. Miezi miwili imekata. Naona amejisahaulisha kabisa. Kila mara namkumbusha kidizaini kwa salamu tu. Naona anajibu kama vile shwari tu. Hagusii kabisa deni.
Sasa mimi nahitaji mkwanja wangu nimeshapeleka watoto shule nahitaji balance hapa home. Nakumbuka hakuomba alisema nimkopeshe. Sasa anajisahaulisha kitu ambacho mi kinanikwaza.
Mimi mtoto wake nililipa mahari cash na sikutaka hata punguzo. So hapa yasije mambo ya baba mkwe ni kama mzee wako. Ndiyo ni kama mzee wangu nami namtreat kama mzee wangu ndo maana nataka kumdai. Mimi hata mdingi huwa tunadaiana vizuri tu Maana alinifundisha dawa la deni ni kulipa tu.
Sasa jana kidogo nimzukie home kwao maana nlikuwa majalala sana but bahati nzuri nikapata ugeni. Ila nawazia leo hii nimfuate ofisini kwake au home. Anipe tu changu.hiyo itanisukuma mpaka tarehe 25.
Nlikuwa naongea na jamaa yangu ananambia eti baba mkwe ni kama mzazi wako hadaiwi. Nikamwambia mi mzazi wangu tunadaiana vizuri tu. Akabadili tena kuwa baba mkwe usimdai. Hapo nikashangaa. Hadi nchi inadaiwa itakuwa baba mkwe?
Sasa nikaona niulize why baba mkwe hatakiwi kudaiwa ikiwa alikopa? Shida ni nini?
Akanambia nimwazime 250,000. Nikamwazima. Miezi miwili imekata. Naona amejisahaulisha kabisa. Kila mara namkumbusha kidizaini kwa salamu tu. Naona anajibu kama vile shwari tu. Hagusii kabisa deni.
Sasa mimi nahitaji mkwanja wangu nimeshapeleka watoto shule nahitaji balance hapa home. Nakumbuka hakuomba alisema nimkopeshe. Sasa anajisahaulisha kitu ambacho mi kinanikwaza.
Mimi mtoto wake nililipa mahari cash na sikutaka hata punguzo. So hapa yasije mambo ya baba mkwe ni kama mzee wako. Ndiyo ni kama mzee wangu nami namtreat kama mzee wangu ndo maana nataka kumdai. Mimi hata mdingi huwa tunadaiana vizuri tu Maana alinifundisha dawa la deni ni kulipa tu.
Sasa jana kidogo nimzukie home kwao maana nlikuwa majalala sana but bahati nzuri nikapata ugeni. Ila nawazia leo hii nimfuate ofisini kwake au home. Anipe tu changu.hiyo itanisukuma mpaka tarehe 25.
Nlikuwa naongea na jamaa yangu ananambia eti baba mkwe ni kama mzazi wako hadaiwi. Nikamwambia mi mzazi wangu tunadaiana vizuri tu. Akabadili tena kuwa baba mkwe usimdai. Hapo nikashangaa. Hadi nchi inadaiwa itakuwa baba mkwe?
Sasa nikaona niulize why baba mkwe hatakiwi kudaiwa ikiwa alikopa? Shida ni nini?