Baba Levo adai Diamond amelipwa TSh. 2.7 Bilioni kutumbuiza kwenye birthday ya Bilionea Ghana

Baba Levo adai Diamond amelipwa TSh. 2.7 Bilioni kutumbuiza kwenye birthday ya Bilionea Ghana

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,687
Reaction score
15,614
Msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amewasili Accra, Ghana, kwa ajili ya kutumbuiza kwenye sherehe ya kuzaliwa ya bilionea maarufu wa nchi hiyo, Richard Nii Armah Quaye.

Kwa mujibu wa Baba Levo, Diamond amelipwa kiasi cha shilingi bilioni 2.7 za Kitanzania kwa ajili ya kutumbuiza katika hafla hiyo ya kifahari.

photo-output.jpeg
Tukio hilo limewaleta pamoja mastaa wakubwa wa Afrika, akiwemo msanii wa Nigeria, Davido, na watu mashuhuri wengine wa bara hili.

IMG_3635.jpeg
 
Hivi Baba Levo anajua kwamba bilioni 2.7 ni sawa dollar za Marekani milioni 1.07 hivi??

Hata kama anampenda Diamond platinums kama boss wake, hii chumvi ni too much

Aseme labda analipwa dollar laki 4 ama pungufu lakini sio dollar milioni 1.07
 
Uongo mwingi sana kwa wasanii wa Tz.
Na hao machawa wao wengi ni mapunga.
 
Hivi Baba Levo anajua kwamba bilioni 2.7 ni sawa dollar za Marekani milioni 1.07 hivi??

Hata kama anampenda Diamond platinums kama boss wake, hii chumvi ni too much

Aseme labda analipwa dollar laki 4 ama pungufu lakini sio dollar milioni 1.07
Alilipwa usd 600,000/=
 
Alilipwa usd 600,000/=
Tatizo la Wasanii wa Bongo kupenda kuongeza sifuri, yaani alifikiri dollar milioni 1.06 ni chache kiasi hicho mtu alipwe Kwa show Moja tu

By the way, hongera zake Diamond

Hata hivyo malipo ya dollar 600,000 sio haba ni zaidi ya Bilioni 1.3 hivi za Tanzania
 
2.7B kutumbuiza tu?? Au na tajiri nae akatumbuiza? 😂😂 maana mmmh!!
 
Sasa hili uliloleta linawasaidiaje waTz au kila mkiona choo au kichaka mavi yanawabana??
 
Sasa hili uliloleta linawasaidiaje waTz au kila mkiona choo au kichaka mavi yanawabana??
Mkuu mbona kama umevurugwa vile........ upo jukwaa la selebriti ujue😂😂😂

Ukitaka mambo ya kukusaidia nenda kapige kambi jukwaa la Kilimo, biashara na uchumi, siasa nk

Jukwaa la selebriti chit chat love connection ni majukwaa ya maskara, umbea na kupunguzia stress
 
Msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amewasili Accra, Ghana, kwa ajili ya kutumbuiza kwenye sherehe ya kuzaliwa ya bilionea maarufu wa nchi hiyo, Richard Nii Armah Quaye.

Kwa mujibu wa Baba Levo, Diamond amelipwa kiasi cha shilingi bilioni 2.7 za Kitanzania kwa ajili ya kutumbuiza katika hafla hiyo ya kifahari.

Tukio hilo limewaleta pamoja mastaa wakubwa wa Afrika, akiwemo msanii wa Nigeria, Davido, na watu mashuhuri wengine wa bara hili.

labda mtuambie peza zote hizo zinajumuisha na huduma ya u-pididy
 
Back
Top Bottom