Mugabe Jr
Senior Member
- Aug 19, 2020
- 160
- 287
Miaka mitatu iliyopita dogo alimaliza kidato cha sita. Akafaulu, akiwa ajiandaa kujiunga na chuo. Dingi akamwambia dogo asomee sheria (bachelor of law). Dogo akamkubalia dingi, na kweli aka apply na kuchaguliwa kusoma sheria ambayo inachukua miaka minne.
Dogo alikosa mkopo chuoni, hivyo dingi akawa anamlipia ada na mahitaji yote ili dogo asome hiyo bachelor of law.
Sasa kumbe dogo baada ya kufika tuu chuoni mwaka wa kwanza akabadili kozi kutoka (bachelor of law) ambayo alishauriwa na dingi kwenda (bachelor of philosophy with education)
Miaka yote hii mitatu dingi amekuwa akimsapoti sana dogo akijua anasomea sheria, kumbe dogo anasoma philosophy with education.
Sasa juzi dogo akiwa likizo fupi maskani, si akaja mzee mmoja rafiki yake na dingi, ambaye ni Wakili wa serikali. Dingi akamtambulisha dogo kwa huyo mzee ambaye ni Wakili, akamwambia kuwa dogo anasomea pia sheria na yuko mwaka wa tatu. Yule mzee ambaye ni Wakili alifurahi mno.
Sasa kimbembe kikaja, Mzee ambaye ni Wakili si akaanza kumuuliza uliza maswali ya sheria dogo akawa anatoa macho tuu. Mzee Wakili akajua hapa hamna kitu, alivyokuwa anaondoka akamuuliza dingi, hivi kweli dogo anasomea sheria? Ili swali likamshitua dingi.
Baada ya mzee ambaye ni Wakili kuondoka. Mzee akambana dogo. Baada ya kubanwa dogo ikabidi afunguke kuwa hasomi sheria, alibadili kozi toka mwaka wa kwanza. Dingi akapaniki akamuuliza kwahiyo unasomea nini? Dogo akajibu ' bachelor of philosophy with education ' dingi aliwaka sana na mpaka sasa hawaongei na dogo hata sapoti hatoi tena.
Dingi anaona dogo kapoteza muda na pesa na kwamba hicho anachosoma hakina future. Dingi haelewi chochote kuhusu hiyo kozi. Mwenye uelewa wa hii degree ya bachelor of philosophy with education hebu anisaidie inahusika na nini? na future yake ikoje? Niweze kumuelewesha dingi.
Dogo alikosa mkopo chuoni, hivyo dingi akawa anamlipia ada na mahitaji yote ili dogo asome hiyo bachelor of law.
Sasa kumbe dogo baada ya kufika tuu chuoni mwaka wa kwanza akabadili kozi kutoka (bachelor of law) ambayo alishauriwa na dingi kwenda (bachelor of philosophy with education)
Miaka yote hii mitatu dingi amekuwa akimsapoti sana dogo akijua anasomea sheria, kumbe dogo anasoma philosophy with education.
Sasa juzi dogo akiwa likizo fupi maskani, si akaja mzee mmoja rafiki yake na dingi, ambaye ni Wakili wa serikali. Dingi akamtambulisha dogo kwa huyo mzee ambaye ni Wakili, akamwambia kuwa dogo anasomea pia sheria na yuko mwaka wa tatu. Yule mzee ambaye ni Wakili alifurahi mno.
Sasa kimbembe kikaja, Mzee ambaye ni Wakili si akaanza kumuuliza uliza maswali ya sheria dogo akawa anatoa macho tuu. Mzee Wakili akajua hapa hamna kitu, alivyokuwa anaondoka akamuuliza dingi, hivi kweli dogo anasomea sheria? Ili swali likamshitua dingi.
Baada ya mzee ambaye ni Wakili kuondoka. Mzee akambana dogo. Baada ya kubanwa dogo ikabidi afunguke kuwa hasomi sheria, alibadili kozi toka mwaka wa kwanza. Dingi akapaniki akamuuliza kwahiyo unasomea nini? Dogo akajibu ' bachelor of philosophy with education ' dingi aliwaka sana na mpaka sasa hawaongei na dogo hata sapoti hatoi tena.
Dingi anaona dogo kapoteza muda na pesa na kwamba hicho anachosoma hakina future. Dingi haelewi chochote kuhusu hiyo kozi. Mwenye uelewa wa hii degree ya bachelor of philosophy with education hebu anisaidie inahusika na nini? na future yake ikoje? Niweze kumuelewesha dingi.