Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
MKAZI wa Makumbusho, Gharibu Ayubu (35) anashikiliwa kituo cha polisi Kinondoni jijini hapa kwa kumkanyaga kichwani kwa gari lake hadi kufa, mtoto wake, Ayubu Gharibu aliyekuwa na mwaka mmoja na miezi mitano wakati alipokuwa akirudi nyuma ili kutoka katika nyumba yake wakati akitaka kuelekea Sinza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elius Kalinga aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2.00 asubuhi katika nyumba ya Gharibu iliyopo barabara ya New Bagamoyo eneo la Makumbusho katika Wilaya ya Kinondoni.
Kalinga alisema tukio hilo lilitokea baada ya mtoto huyo kutaka kwenda na baba yake asubuhi hiyo, lakini baba yake akamkabidhi kwa makewe ambaye alirudi naye ndani, lakini baada ya muda mtoto huyo alitoka tena nje na kulifuata gari hilo bila mama yake kujua.
Alisema mtoto huyo alipolifikia gari hilo aina ya Toyota Folona alikwenda kusimama nyuma yake na Gharibu alipokuwa akirudi nyuma ili aweze kupata mwelekeo wa kutoka katika nyumba yake kuelekea Sinza ghafla akamkanyaga mtoto huyo kichwani na kumsababishia kifo kwa kuwa aliumia sana kichwani.
Kamanda Kalinga alisema Gharibu anashikiliwa na jeshi lake na atafikishwa mahakamani huku uchunguzi wa kesi yake ukiendelea kufanyika.
Katika tukio jingine, Kamanda Kalinga alisema maiti ya mwanaume aliyefahamika kwa jina la Yusuph Mwinchande (36) ilikutwa ikiwa kandokando ya makaburi huku pembeni kukiwa na bomba la sindano linalosadikiwa kuwa na dawa za kulevya.
Kalinga alisema maiti hiyo ilikutwa juzi saa 9.00 jioni na chanzo cha kifo hicho bado hakijafahamika, uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.
Katika tukio jingine, Mkazi wa Handeni Tanga, Shola Mwangomo (37) alifariki dunia akiwa ndani ya basi la Kampuni ya Sai Baba akitokea nchini Msumbiji pamoja na rafiki yake, Obed Mwakihaba (37) ambaye ni mkazi wa Kihonda Morogoro.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Temeke, David Sime alisema Obed alitoa taarifa juu ya kifo hicho baada ya kufika jijini Dar es Salaam ambapo alisema yeye na rafiki yake huyo ambaye sasa ni marehemu walitoka nchini Msumbiji katika kitongoji cha Montepwesi kijiji cha Nanupo, Aprili 9 saa 11.00 alfajiri lakini walipofika Somanga katika daraja la Mkapa rafiki yake akafariki dunia.
Hata hivyo Kamanda Sime alisema kuwa Obedi alidai kuwa rafiki yake huyo kabla hajafariki alikuwa akiumwa malaria. Maiti imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya Temeke kwa uchunguzi.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=19163
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elius Kalinga aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2.00 asubuhi katika nyumba ya Gharibu iliyopo barabara ya New Bagamoyo eneo la Makumbusho katika Wilaya ya Kinondoni.
Kalinga alisema tukio hilo lilitokea baada ya mtoto huyo kutaka kwenda na baba yake asubuhi hiyo, lakini baba yake akamkabidhi kwa makewe ambaye alirudi naye ndani, lakini baada ya muda mtoto huyo alitoka tena nje na kulifuata gari hilo bila mama yake kujua.
Alisema mtoto huyo alipolifikia gari hilo aina ya Toyota Folona alikwenda kusimama nyuma yake na Gharibu alipokuwa akirudi nyuma ili aweze kupata mwelekeo wa kutoka katika nyumba yake kuelekea Sinza ghafla akamkanyaga mtoto huyo kichwani na kumsababishia kifo kwa kuwa aliumia sana kichwani.
Kamanda Kalinga alisema Gharibu anashikiliwa na jeshi lake na atafikishwa mahakamani huku uchunguzi wa kesi yake ukiendelea kufanyika.
Katika tukio jingine, Kamanda Kalinga alisema maiti ya mwanaume aliyefahamika kwa jina la Yusuph Mwinchande (36) ilikutwa ikiwa kandokando ya makaburi huku pembeni kukiwa na bomba la sindano linalosadikiwa kuwa na dawa za kulevya.
Kalinga alisema maiti hiyo ilikutwa juzi saa 9.00 jioni na chanzo cha kifo hicho bado hakijafahamika, uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.
Katika tukio jingine, Mkazi wa Handeni Tanga, Shola Mwangomo (37) alifariki dunia akiwa ndani ya basi la Kampuni ya Sai Baba akitokea nchini Msumbiji pamoja na rafiki yake, Obed Mwakihaba (37) ambaye ni mkazi wa Kihonda Morogoro.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Temeke, David Sime alisema Obed alitoa taarifa juu ya kifo hicho baada ya kufika jijini Dar es Salaam ambapo alisema yeye na rafiki yake huyo ambaye sasa ni marehemu walitoka nchini Msumbiji katika kitongoji cha Montepwesi kijiji cha Nanupo, Aprili 9 saa 11.00 alfajiri lakini walipofika Somanga katika daraja la Mkapa rafiki yake akafariki dunia.
Hata hivyo Kamanda Sime alisema kuwa Obedi alidai kuwa rafiki yake huyo kabla hajafariki alikuwa akiumwa malaria. Maiti imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya Temeke kwa uchunguzi.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=19163