Baba anaesadikiwa kumpa mimba mwanae wakumzaa afikishwa mahakamani jijini mbeya...!!!

Money Stunna

JF-Expert Member
Aug 9, 2011
13,054
6,281
Mkazi wa Mtaa wa Mbete, Kata ya Isanga Jijini Mbeya Bwana Yussuf Hamad(39),anatuhumiwa kumpa mimba binti yake wa kumzaa(16) jina lake limehifadhiwa. akiingia mahakamani leo mbele yake ni mke wake na mtoto wake aliyezaanae ambao sura zao tumefunika
Bwana Yussuf Hamad anaetuhumiwa kuzaa na bintie akitaka kumpokonya kamera mwandishi wa gazeti la majira Rashid Mkwinda ili asimpige picha
Jamaa kuona amezidiwa akaamua kujifunika na shati lake huku akitoa maneno makali kuwa nyie waandishi mmekosa cha kuandika mmeona hii ndiyo habari hakuna habari nyingine? alihoji mtuhumiwa huyo
Huyoooo anatoka nje ya mahakama

Sasa anavaa kofia yake ili watu wasimtambue huku akisema nifuateni niwaonyeshe kazi
Njooni sasa huku kashika jiwe
Kuona anazidi kufuatwa akaamua kuondoka mahali hapo huku akiwa na jiwe lake mkononi
Akina mama wanamsindikiza kwa kumzomea mtuhumiwa huyo
---

Mkazi wa Mtaa wa Mbete, Kata ya Isanga Jijini Mbeya Bwana Yussuf Hamad(39),anatuhumiwa kumpa mimba binti yake wa kumzaa(15) jina lake limehifadhiwa.

Hayo yamethibitishwa na Mama mzazi wa binti huyo Bi, Regina Simon(35) baada ya kupata taarifa Mei 11 mwaka huu kuwa binti yake ana ujauzito wa miezi minne,na kuamua kutoa taarifa kwa Balozi wa mtaa huo Bwana Steven Ovaova ambaye naye alitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Kitongoji Bwana Angelo Sanga.​
Viongozi hao wa mtaa walimuita mtuhumiwa na ili kupata ukweli wa tukio hilo,lakini mtuhumiwa alikanusha ingawa binti yake alithibitisha kutendewa ukatili huo na kwamba alikuwa akitishiwa kwa mapanga kila alipokuwa akifanya naye tendo la ndoa.​
Baada ya uongozi kupata maelezo kutoka kwa binti huyo na mzazi kukataa waliamua kuipeleka kesi hiyo Polisi,ambapo walitoa PF3 iliyomwezesha binti huyo kupelekwa kwa​
daktari ambaye alithibitisha kuwa binti huyo ana ujauzito.


Binti huyo amejifungua mtoto wa kike ambae sasa anamiezi mitatu mtoto huyo kaletwa leo mahakamani kama ushahidi kesi hiyo imeairishwa mapaka tarehe 12/12 mwaka huu.

Source: Mbeya Yetu
 
Picha zinajieleza!
Ilikuwaje hadi akaachwa huru na kujirudia kwake?
Kesi hii ina dhamana?
 
issue hapa ni nini kuwa kambaka mtoto ama kampa mimba mtoto wake...kwani kuna sheria inakataza mtu kuwa na mahusiano na mtu fulani na mtu furani ni sumu?
 
issue hapa ni nini kuwa kambaka mtoto ama kampa mimba mtoto wake...kwani kuna sheria inakataza mtu kuwa na mahusiano na mtu fulani na mtu furani ni sumu?

sheria ipo inayokataza kufanya mapenzi na ndugu kama mtoto, mama au baba. Kwa upande wa huyu bwana kama ni kweli atakuwa na kesi ya kujibu, inaitwa (incest by female).
 
issue hapa ni nini kuwa kambaka mtoto ama kampa mimba mtoto wake...kwani kuna sheria inakataza mtu kuwa na mahusiano na mtu fulani na mtu furani ni sumu?

mtoto ana miaka 15 hivo ni kama amembaka,nimeshangaa kuona yuko nje uku kesi ikiendelea,kwa mnaojua mtueleze kama kesi kama hii ina dhamana
 
Ninaambiwa kwamba dini ya jaamaa haina dhambi,kwa maana ya kwamba mambo yote kama kutukana, kuua, ushirikina, uwongo uchawi, chuki, udanganyifu n.k ni ruksa. Lakini sikufikiria kwamba hata conscious kumbe huwa zinakufa. Jamaa hata haya wala hofu hana.
 
issue hapa ni nini kuwa kambaka mtoto ama kampa mimba mtoto wake...kwani kuna sheria inakataza mtu kuwa na mahusiano na mtu fulani na mtu furani ni sumu?

Ndio sheria ya Jinai inakaza! Huyo baba amefanya kosa kisheria linaitwa incest na anaweza kufungwa si chini ya miaka ishirini.
 
Ninaambiwa kwamba dini ya jaamaa haina dhambi,kwa maana ya kwamba mambo yote kama kutukana, kuua, ushirikina, uwongo uchawi, chuki, udanganyifu n.k ni ruksa. Lakini sikufikiria kwamba hata conscious kumbe huwa zinakufa. Jamaa hata haya wala hofu hana.

Dini gani hiyo Tabby?
 
Jamani dunia hii inakwenda kubaya mnoooooooooo!! Tumegeuka mang'ombe na mambuzi, ni kinyaaaaa hata kufikiria! Tuhurumiwe kwa kweli!
 
Najishauri ningekuwa mke wake ningefanyaje kuficha aibu hii??? aibu ya :mimba: , aibu ya :behindsofa: sura.
ok ningempikia pilau tamu nikaweka sumu akafia mbali nikabaki na wanangu.
 
Ndio sheria ya Jinai inakaza! Huyo baba amefanya kosa kisheria linaitwa incest na anaweza kufungwa si chini ya miaka ishirini.

kama nikweli basi kuna ulakini vipi apate Dhamana kwa kesi ya Kubaka na kutishia kwa mapanga??je USALAMA WAKE UKOJEE je usalama wa mlalamikaji ambae ni Mtoto unakuwaje hao Majirani wata mchukulia vipi ki Usalama hebu tuwekeni sawa ki Akili na Upeo hiyokesi ukweli kama sio huo huyo Mwandishi ana Kesi yakujbu polen
 
narudia tena wanaume ni viumbe hatari sana ,siwezi watofautisha na nguruwe mwenye uwezo wakula watoto wake aliowazaa sasa tofauti ikowapi??
 
narudia tena wanaume ni viumbe hatari sana ,siwezi watofautisha na nguruwe mwenye uwezo wakula watoto wake aliowazaa sasa tofauti ikowapi??

Nivea si wanaume wote wako hivyo,hiyo tabia ni ya mtu husika.Kuna thread siku za nyuma kidogo inazungumzia mwanamke anayeishi kinyumba na mwanae wa kiume wa kumzaa.


Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Ndio sheria ya Jinai inakaza! Huyo baba amefanya kosa kisheria linaitwa incest na anaweza kufungwa si chini ya miaka ishirini.

tena ana yote incest na pia kubaka... ni chini ya 18 hiyooooooooooooooo. japo marehemu kanuamba ali.....
 
tena ana yote incest na pia kubaka... ni chini ya 18 hiyooooooooooooooo. japo marehemu kanuamba ali.....

We acha tu! Niwe hakimu wa hiyo kesi lazima nitenganishe adhabu! Anamaliza mvua za incest anaanza mvua 30 za kubaka!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom