Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,125
| Baba mmoja wa nchini Australia amejikuta akiingia matatani kwa hatua yake ya kumruhusu binti yake mwenye umri wa miaka 14 kufanya mapenzi na mpenzi wake mwenye umri wa miaka 26 ndani ya nyumbani yake kisa akiogopa binti yake asije akatoroka na mwanaume huyo. |
Katika kesi hiyo ambayo imedaiwa kuwa ya kwanza kutokea nchini Australia, Baba huyo mwenye umri wa miaka 14 alihofia binti yake asije akatoroka na mpenzi wake mwenye umri wa miaka 26 hivyo akawaruhusu wawe wanafanya mapenzi mara kwa mara ndani ya nyumba yake. Baba huyo alikiri mashtaka aliyofunguliwa ya kumsaidia mtoto wake wa kike kuingia kwenye mapenzi na mtu mzima. Baba huyo alisema kuwa binti yake alitishia kutoroka na mwanaume huyo hali iliyopelekea akubali huyo mpenzi wake awe anakuja nyumbani kwake kufanya mapenzi na binti yake. Mwanasheria wa baba huyo alisema kuwa baba wa binti huyo alibaki na maamuzi mawili ya kuchagua mojawapo, aruhusu mapenzi yafanyike ndani ya nyumbani yake au akubali mtoto wake atoroke na mwanaume huyo na kwenda kuishi sehemu nyingine. Baba huyo mkazi wa Hobart katika jimbo la Tasmania nchini Australia anasubiri hukumu yake wakati mpenzi wa binti yake tayari ameishatupwa jela kwa kufanya mapenzi na mtoto chini ya miaka 17. |
Baba Amruhusu Binti Yake wa Miaka 14 Kufanya Mapenzi na Mwanaume