Hivi karibuni kumekuwa na watu wenye fikra hasi kuelekea maendeleo ya kitaifa.
1. Ajali ya treni Bahi. Kuna Watanzania wenzetu wanaikuza habari na kukataa kuwa ni vifo vitatu tu, wanasema namba imefichwa. Wanatamani maafa yangekuwa makubwa sana sababu tu serikali imepeleka nguvu nyingi kwenye miundo mbinu ya reli.
2. Mwanzoni hospitali nzuri ya kisasa ya Mloganzila nayo ilitangazwa kama hospitali hatari ukipelekwa huponi. Kipindi ambacho ilibidi watanzania tujivunie kwa kuwa na hospitali nzuri.
3. Uvunjaji rekodi wa mapato ya TRA, kama taifa ilibidi tushangilie mafanikio na kuongeza juhudi kwani mapato yakiwa makubwa taifa litaweza kwenda mbele kwa kasi lakini kuna Watanzania wenzetu hili nalo hawalifurahii.
Umewaza itakuwaje reli ya SGR ikisombwa na mafuriko? Au kwa bahati mbaya ndege yetu moja ikapata ajali? Je, tutasikitika kama taifa ama wapo watakaoshangilia?
Baadhi yetu wanatamani taifa lianguke, likumbwe na magonjwa na maafa ili tu serikali ilaumiwe. Kama taifa tufanye nini tutoke hapa maana hali inavyozidi kuna hati hati ya adui wa taifa kupata support na kuweza kuyumbisha taifa kirahisi.
1. Ajali ya treni Bahi. Kuna Watanzania wenzetu wanaikuza habari na kukataa kuwa ni vifo vitatu tu, wanasema namba imefichwa. Wanatamani maafa yangekuwa makubwa sana sababu tu serikali imepeleka nguvu nyingi kwenye miundo mbinu ya reli.
2. Mwanzoni hospitali nzuri ya kisasa ya Mloganzila nayo ilitangazwa kama hospitali hatari ukipelekwa huponi. Kipindi ambacho ilibidi watanzania tujivunie kwa kuwa na hospitali nzuri.
3. Uvunjaji rekodi wa mapato ya TRA, kama taifa ilibidi tushangilie mafanikio na kuongeza juhudi kwani mapato yakiwa makubwa taifa litaweza kwenda mbele kwa kasi lakini kuna Watanzania wenzetu hili nalo hawalifurahii.
Umewaza itakuwaje reli ya SGR ikisombwa na mafuriko? Au kwa bahati mbaya ndege yetu moja ikapata ajali? Je, tutasikitika kama taifa ama wapo watakaoshangilia?
Baadhi yetu wanatamani taifa lianguke, likumbwe na magonjwa na maafa ili tu serikali ilaumiwe. Kama taifa tufanye nini tutoke hapa maana hali inavyozidi kuna hati hati ya adui wa taifa kupata support na kuweza kuyumbisha taifa kirahisi.