Baadhi Ya Watanzania Ni Vipofu Kabisaa

Kidzogolae

Senior Member
Apr 20, 2008
133
2
Jambo forum pamoja na watz wengine wenye uwelewa, tunayo kazi kubwa ya kuwaelimisha watz wenzetu walio vipofu. si kosa lao, kikubwa najua ni umasikini na kunyimwa elimu, ndo maana hawajui yanayoendelea duniani na tz kwa ujumla. mfano, Lowasa alikula kodi zao, lakini walipomwona kule Monduli waliungana nae, wakamshangilia na kuona kama watz tuliomfichua ni wabaya. pili, kule kwa mzee chenge, au kenge kwa jina lingine wanalomwita watu mtaani. siliafiki jina hili. alipoende kule kwenye jimbo lake, wamemshangilia na kumpa sifa zote, na wanaona kama vile sisi tuliomfichua ni watu wabaya. Naombeni, hivi tufanye nini ili watz wote wajue kinachoendelea duniani? mbona wengi wetu huko vijijini ni vipofu kabisa, ndo maana hadi leo tunaogopa mabadiliko, hata kubadili chama, watu wanafikiri ccm ndo kila kitu, ukibadilisha ccm ni kuleta vita. ndo maana ccm wana wini sana vijijini kwasababu vijijini watu wana uelewa mdogo sana. Mungu saidia watz wenzangu hawa, wajue kuwa hela zinazoibiwa na hawa mafisadi ni za kwao, ni kodi zao. hivyo wao wenyewe ndo wanaibiwa. asante. nimeandika haraka, nitasahihisa vizuri baadae. nafanya kazi hapa, naomba niendelee.
 
Jambo forum pamoja na watz wengine wenye uwelewa, tunayo kazi kubwa ya kuwaelimisha watz wenzetu walio vipofu. si kosa lao, kikubwa najua ni umasikini na kunyimwa elimu, ndo maana hawajui yanayoendelea duniani na tz kwa ujumla. mfano, Lowasa alikula kodi zao, lakini walipomwona kule Monduli waliungana nae, wakamshangilia na kuona kama watz tuliomfichua ni wabaya. pili, kule kwa mzee chenge, au kenge kwa jina lingine wanalomwita watu mtaani. siliafiki jina hili. alipoende kule kwenye jimbo lake, wamemshangilia na kumpa sifa zote, na wanaona kama vile sisi tuliomfichua ni watu wabaya. Naombeni, hivi tufanye nini ili watz wote wajue kinachoendelea duniani? mbona wengi wetu huko vijijini ni vipofu kabisa, ndo maana hadi leo tunaogopa mabadiliko, hata kubadili chama, watu wanafikiri ccm ndo kila kitu, ukibadilisha ccm ni kuleta vita. ndo maana ccm wana wini sana vijijini kwasababu vijijini watu wana uelewa mdogo sana. Mungu saidia watz wenzangu hawa, wajue kuwa hela zinazoibiwa na hawa mafisadi ni za kwao, ni kodi zao. hivyo wao wenyewe ndo wanaibiwa. asante. nimeandika haraka, nitasahihisa vizuri baadae. nafanya kazi hapa, naomba niendelee.
Si kweli kwamba vijijini wana upungufu wa kuelewa yanoyoendelea katika TZ. Vijijini kuna shule za msingi hadi sekondari, katika mtawanyiko wa Kata hadi Tarafa. Kupitia shule hizo na watoto wasomao huko, wazee na vijana wanajua kila kinachiendelea katika nchi hii.

Kuna redio kadhaa za kimataifa ambazo hutangaza kila siku yanayotokea Duniani na kuwafikia watu wa huko vijijini, mfano BBC. VOA, China na Ujerumani wana idhaa zao za kiswahili ambazo licha ya kuripoti juu ya tuhuma mbalimbali za viongozi wa nchi hii, hufanya mahojiano nao,hivyo kupelekea kwa walio huko vijijini kujua nini kinaendelea katika nchi hii. Labda wanakosa magazeti ya kila siku na yale magazeti yapendwayo na wengi ya udaku.

Kuwepo hapa JF kusiwe kigezo cha kwamba unajua kila kinachoendelea hapa Duniani, Unaweza kuwepo hapa JF na ukapitwa na makala nzuri nzuri zenye kuelimisha kupitia Radio za kimataifa na unaweza kuumbuka vilevile inapotokea kuwa unabishana na hao wa vijijini ambao wamesikiliza makala hizo.

Nafasi hii ya internet itumiwe vizuri zaidi ya kubeza hao walio wengi waishio vijijini kwamba hawajui chochote kwa kuwa una nafasi ya kubonyeza keyboard tu...!
 
Mkuu, naomba uelewe vizuri hii topic. bahati mbaya sijui wewe upo upande gani na upo kwaajili ya nini humu Jf. kwani, kuna wengine humu nimehisi ni makachelo wa selikali, na wengine wapo ili kuchangia na kuyafichua maovu tz kwa maslahi ya watz wote.

Nikija kwenye topic, mimi sijaja humu ndani ya JF mda mrefu, niliipenda kwasababu niliona mambo mengi ambayo hayaongelewi bayana mtaani,pamoja na kwamba watu wanajua, hapa yanaongelewe bayana. kuwepo humu si ufahari wowote kwangu, kwasababu hapa so ndo sehemu pekee napata information. ninafanya utafiti sana, na nipo kwenye jamii, najua kinachoendelea tz.

Ninaposema kuwa, watz wengi vijijini wana uelewa mdogo, nina uhakika na ninachoongea kwasababu nimeishi huko, nimefanya kazi na NGOs na kuishi na watu huko sana, na mara nyingi natembelea huko kwaajili ya shughuli zangu. hizo redio unazosema kuwa watu wanasikiliza, uwe na uhakika na unachoongea, na kwamba kila mtu ana afford kununua betri na hizo radio. Najua kati ya watu mia moja, mmoja anaweza akajua nusu ya kinachoendelea, ila asilimia 99 ya watu vijijini hawajui uhalisia juu ya nchi yetu. usifiche maovu bwana, hivyo vijisent ndo hela ingetosha kupeleka watu hao shule, na wangekuwa na broad knowledge ya kuelewa mambo. kama wanaelewa, kwanini walimpaparikia Chenge na Lowasa wakati wanajua ni mafisadi? cha kwanza hapa tz, inabidi tupigane na ujinga, halafu umasikini utajiengua wenyewe.

wewe jamaa unaonekana ni kada wa ccm.halafu, una uelewa sio mkubwa sana. hivi una uhakika na unachoongea kuwa watz vijijini wana access information vizuri na wanajua kinachoendelea selikalini vizuri na duniani vizuri?umeshawai kuishi village wewe, akili gani ya kuwa na uelewa kama huo wako?wewe uko wapi kwanza? duh!
 
Mkuu, naomba uelewe vizuri hii topic. bahati mbaya sijui wewe upo upande gani na upo kwaajili ya nini humu Jf. kwani, kuna wengine humu nimehisi ni makachelo wa selikali, na wengine wapo ili kuchangia na kuyafichua maovu tz kwa maslahi ya watz wote.

Nikija kwenye topic, mimi sijaja humu ndani ya JF mda mrefu, niliipenda kwasababu niliona mambo mengi ambayo hayaongelewi bayana mtaani,pamoja na kwamba watu wanajua, hapa yanaongelewe bayana. kuwepo humu si ufahari wowote kwangu, kwasababu hapa so ndo sehemu pekee napata information. ninafanya utafiti sana, na nipo kwenye jamii, najua kinachoendelea tz.

Ninaposema kuwa, watz wengi vijijini wana uelewa mdogo, nina uhakika na ninachoongea kwasababu nimeishi huko, nimefanya kazi na NGOs na kuishi na watu huko sana, na mara nyingi natembelea huko kwaajili ya shughuli zangu. hizo redio unazosema kuwa watu wanasikiliza, uwe na uhakika na unachoongea, na kwamba kila mtu ana afford kununua betri na hizo radio. Najua kati ya watu mia moja, mmoja anaweza akajua nusu ya kinachoendelea, ila asilimia 99 ya watu vijijini hawajui uhalisia juu ya nchi yetu. usifiche maovu bwana, hivyo vijisent ndo hela ingetosha kupeleka watu hao shule, na wangekuwa na broad knowledge ya kuelewa mambo. kama wanaelewa, kwanini walimpaparikia Chenge na Lowasa wakati wanajua ni mafisadi? cha kwanza hapa tz, inabidi tupigane na ujinga, halafu umasikini utajiengua wenyewe.

wewe jamaa unaonekana ni kada wa ccm.halafu, una uelewa sio mkubwa sana. hivi una uhakika na unachoongea kuwa watz vijijini wana access information vizuri na wanajua kinachoendelea selikalini vizuri na duniani vizuri?umeshawai kuishi village wewe, akili gani ya kuwa na uelewa kama huo wako?wewe uko wapi kwanza? duh!
Kamanda kidzogolae:
Jina gumu kidogo!
Nikirudi kwenye mada bado unaonyesha kuwa upo hapa kwa ajili ya kuhukumu na sio kujadili hoja mbalimbali. Aya yako ya kwanza inaonyesha upo hapa kwa mtazamo gani na unakusudia kusema na kuandika nini wakati wote ule ambao utakuwepo katika forum hii. Hilo ni kosa la kwanza ambalo ni lazima nitilie shaka lengo zima la hii mada yako.

Kwa taarifa tu wakati wote unapokuwa hapa usitegemee kusikia kile ambacho masikio yanategemea kusika ili kuthibitisha kuwa upo sahihi katika bandiko lako.

Bandiko lako lina mapungufu makubwa na hasa pale ulipoamua kuhitimisha kuwa huko vijijini ni vipofu kuhusu mstakabala wa nchi yetu leo hii. Kisa kwa kuwa Baadhi ya mafisadi wameweza kupokelewa kwa shangwe na vifijo na wapiga kura wao. Katika hili ilikupasa kujiuliza ni kwa nini hayo yametokea aidha kwenda ndani zaidi kwa kujiuliza kwa nini mafisadi hao bado wanakumbatiwa na wapiga kura wao.

Kama u mfuatiliaji wa mabandiko kadhaa hapa JF, na hasa katika baraza hili la siasa nina hakika kuwa usingekuja na bandiko la aina hii. Kwani tokea mwanzo wa vita hivi vya kifikra kupitia hapa mengi yamejadiliwa na imekuwa ni wajibu wa kila mwanachama kufahamu ni nini kinaendelea na ni nini kifanyike ili nchi irudi katika mstari.

Kumekuwepo na tofauti za kiitikadi,malengo,sera binafsi n.k haya yote yamechanganywa katika mabandiko kadhaa yenye kufanana na hili na wanaJF na wengine wasimuliao yayatotokea humu ndani kujua nini kinaendelea na tatizo la haya yote ni nini.

Leo hii kuja na kubeza kuwa Watz ni vipofu ni dharau ya hali ya juu. Huko vijijini pamoja na kuwepo na miundombinu mibovu kulinganisha na mijini bado wanapata taarifa muhimu kwa yale ambayo yanajili katika nchi hii. Ni vijijini ambako bado watu wanajadiliana uso kwa uso katika masoko,misiba,arusi na zaidi jioni kwenye vilabu vya pombe. Zaidi wageni wanatokea mijini hupeleka taarifa na habari mbalimbali kwa njia ya mdomo kama ulivyokuwa ukienda huko kwa ajili ya NGO.

Kwa ushauri tu, jaribu kupitia mada zenye muelekeo kama huu ambazo zipo lukuki hapa JF, badala ya kuhukumu kuwa kuna makachero wa serikali, wapinzani wa vita vya fikra, wanaolipwa kuwepo hapa na wazo lingine lolote ambalo unalo kichwani kwa mjumbe mwenye mtazamo tofauti na wewe.
 
Mtoa Mada Unakosea Sana Unaposema Kuna Watu Vipofu Nchi Hii Unatakiwa Ubadilike Wewe Mwenyewe Kwanza Kimtazamo Ndio Unyooshe Kidole
 
Kama ulikusudia "upofu" kumaanisha kushindwa kung'amua naona wewe ndiye una "upofu" mkubwa wa aina hiyo kuliko hao unaowasema.

Kwanza ni offensive (and yes sooo 20th century) kuhusisha conditions za watu na mapungufu ya ung'amuzi au mengine yeyote yasiyotokea naturally.It is not cool to say "Muogope kama Mkoma" anymore.It is germophobic. Will Smith katika wimbo wake "Live at Union Square" (1986) alisema

I want everybody out there that's ugly

all the ugly people be quiet
all the filthy, stinky, nasty people be quiet
all the homeboys that got aids be quiet
all the girls out there that don't like guys, be quiet
hold on, wait a minute
all the girls that don't like guys be quiet

Leo hii anajisikia very embarassed kwa sababu ni maneno yanayoonyesha ujinga wake kuhusu matatizo haya.Anaweza kusamehewa kwa sababu ilikuwa 1986, alikuwa mdogo sana na hata haya mambo nayo yalikuwa relatively mapya


Ni basi tu hatupo katika society iliyo au inayotaka kuwa completely politically correct.Otherwise wengine tungekuwa justified kuona kuhusishwa kwa wale walio "visually challenged" na kutojua mambo ni kashfa.Kuna mtu wa aina hii ni Gavana wa jimbo la New York, sasa unaposema Watanzania ni vipofu maana yako nini?

Kuna kina Nico Zengekala, Kina Mzee Morris Nyunyusa na kuna mpiga ngoma mwingine maarufu kipofu jina nimemsahau, sasa hawa achievement zao ndogo? Kuna watu wana vision zao na hawawezi kuimba au kupiga ngoma kama hawa.

Kwa hiyo tukitaka kusema Watanzania hawajui kitu tusitumie mifano offensive na ambayo inawabagua watu fulani wa society.Sema Watanzania wamezubaa, wajinga, hawana akili etc usiseme Watanzania vipofu. Vipi vipofu wanaoelewa mambo na ambao hawapigii kura wala kushabikia uzandiki huu unaoukashifu, wao watakuwa vipofu wa aina gani? watakuwa vipofu wa aina zote mbili metaphorically and literary au watakuwa "vipofu wanaoona"?

Hilo la kwanza na wengine wanaweza kuliona trivial, lakini liko deep in our collective subconscious as a nation.Ukiwa na attitude kuwa vipofu ni watu wasiojua hukawii kuwa condescende na hata kuwa abuse.Kuna vipofu wanaojua kusoma (braille) na wengi wenye macho wasiojua kusoma!


Lakini zaidi ya hapo, tukiondoa swala la matumizi mabaya ya lugha na mifano, kuna swala zima la kutoelewa nature ya Watanzania.Watanzania wana complexity inayo defy conventions nyingi tu.Trust me, hawa watu wanaelewa due process kuliko tunavyofikiri na inawezekana wengi wana suspend judgement, of course kuna ma partisan ambao kila mtu wa CCM hakosei, of course kuna ma opportunist wanaojua Chenge ana vijisenti kwa hiyo tusicheze mabali, of course kuna ma radical kama yule mchizi wangu aliyemkata Kikwete mtama kwenye campaigns, kwa hiyo kuna kila mtu wa kila hali tanzania.Usione hao wachache waliojitokea barabarani kuangalia commotion ya magari pamoja na kuamini ripoti za magazeti uchwara yaliyonunuliwa ukafikiri Chenge ana mass appeal na support kiasi hicho.Ikumbukwe Bariadi ni moja ya sehemu zenye upinzani mkubwa kwa CCM na hata kama DP inachechemea bado networks zake huko kwa kina Cheyo zipo.

Sitaki kudismiss argument yako kuwa kuna watu hawajui kinachoendelea, na mara nyingi tumejadili jinsi ya kupanga mikakati ya kuongeza elimu ya uraia nchini.Lakini pia kuna hii elitist attitude ya kuwa "sisi ndio tunajua kinachoendelea, watu wa vijijini hawajui kitu" inakosa adabu na haijui kuwa ushamba wa ushamba nao ni ushamba! Kwamba kama vile baadhi ya watu wa vijijini walivyokosa elimu ya magharibi na wasivyosoma magazeti, na sisi inawezekana tumekosa elimu ya asili na hatujui ku reason kivyao.Kuna mababu/ mabibi wengi wana akili na busara sana bila shule.Tunafanya juhudi gani kuungana nao, kuwasikiliza na kuwaelewa kwa nini wanapigia kura CCM?

Tukiweza kujibu hili swali, bila ya kufanya assumptions za haraka haraka za elimu -ya magharibi- ndogo (inaweza kuwa factor but lets find out) tutakuwa na sehemu nzuri ya kuanzia.
 
Ni kweli huko vijijini wako watu waliniuliza mbona Mwalimu Nyerere siku hizi hawamuoni katika siasa ,nikawajibu amekuwa mzee sana na mambu ya misafara haiwezi ,maana ni miaka 8 sasa imepita jamaa anakuuliza mbona Nyerere haonekani ,huoni kama kuna waathirika huko vijijini.
 
Ni kweli huko vijijini wako watu waliniuliza mbona Mwalimu Nyerere siku hizi hawamuoni katika siasa ,nikawajibu amekuwa mzee sana na mambu ya misafara haiwezi ,maana ni miaka 8 sasa imepita jamaa anakuuliza mbona Nyerere haonekani ,huoni kama kuna waathirika huko vijijini.
Kamanda Mwiba:
You're better than that... wacha hadithi za vijiweni/maskani/barazani
 
Jambo forum pamoja na watz wengine wenye uwelewa, tunayo kazi kubwa ya kuwaelimisha watz wenzetu walio vipofu. si kosa lao, kikubwa najua ni umasikini na kunyimwa elimu, ndo maana hawajui yanayoendelea duniani na tz kwa ujumla. mfano, Lowasa alikula kodi zao, lakini walipomwona kule Monduli waliungana nae, wakamshangilia na kuona kama watz tuliomfichua ni wabaya. pili, kule kwa mzee chenge, au kenge kwa jina lingine wanalomwita watu mtaani. siliafiki jina hili. alipoende kule kwenye jimbo lake, wamemshangilia na kumpa sifa zote, na wanaona kama vile sisi tuliomfichua ni watu wabaya. Naombeni, hivi tufanye nini ili watz wote wajue kinachoendelea duniani? mbona wengi wetu huko vijijini ni vipofu kabisa, ndo maana hadi leo tunaogopa mabadiliko, hata kubadili chama, watu wanafikiri ccm ndo kila kitu, ukibadilisha ccm ni kuleta vita. ndo maana ccm wana wini sana vijijini kwasababu vijijini watu wana uelewa mdogo sana. Mungu saidia watz wenzangu hawa, wajue kuwa hela zinazoibiwa na hawa mafisadi ni za kwao, ni kodi zao. hivyo wao wenyewe ndo wanaibiwa. asante. nimeandika haraka, nitasahihisa vizuri baadae. nafanya kazi hapa, naomba niendelee.

Ujumbe Mzito
 
Ni kweli huko vijijini wako watu waliniuliza mbona Mwalimu Nyerere siku hizi hawamuoni katika siasa ,nikawajibu amekuwa mzee sana na mambu ya misafara haiwezi ,maana ni miaka 8 sasa imepita jamaa anakuuliza mbona Nyerere haonekani ,huoni kama kuna waathirika huko vijijini.

Hii kali. Inafungua wikiendi.
 
Kamanda kidzogolae:
Jina gumu kidogo!
Nikirudi kwenye mada bado unaonyesha kuwa upo hapa kwa ajili ya kuhukumu na sio kujadili hoja mbalimbali. Aya yako ya kwanza inaonyesha upo hapa kwa mtazamo gani na unakusudia kusema na kuandika nini wakati wote ule ambao utakuwepo katika forum hii. Hilo ni kosa la kwanza ambalo ni lazima nitilie shaka lengo zima la hii mada yako.

Kwa taarifa tu wakati wote unapokuwa hapa usitegemee kusikia kile ambacho masikio yanategemea kusika ili kuthibitisha kuwa upo sahihi katika bandiko lako.

Bandiko lako lina mapungufu makubwa na hasa pale ulipoamua kuhitimisha kuwa huko vijijini ni vipofu kuhusu mstakabala wa nchi yetu leo hii. Kisa kwa kuwa Baadhi ya mafisadi wameweza kupokelewa kwa shangwe na vifijo na wapiga kura wao. Katika hili ilikupasa kujiuliza ni kwa nini hayo yametokea aidha kwenda ndani zaidi kwa kujiuliza kwa nini mafisadi hao bado wanakumbatiwa na wapiga kura wao.

Kama u mfuatiliaji wa mabandiko kadhaa hapa JF, na hasa katika baraza hili la siasa nina hakika kuwa usingekuja na bandiko la aina hii. Kwani tokea mwanzo wa vita hivi vya kifikra kupitia hapa mengi yamejadiliwa na imekuwa ni wajibu wa kila mwanachama kufahamu ni nini kinaendelea na ni nini kifanyike ili nchi irudi katika mstari.

Kumekuwepo na tofauti za kiitikadi,malengo,sera binafsi n.k haya yote yamechanganywa katika mabandiko kadhaa yenye kufanana na hili na wanaJF na wengine wasimuliao yayatotokea humu ndani kujua nini kinaendelea na tatizo la haya yote ni nini.

Leo hii kuja na kubeza kuwa Watz ni vipofu ni dharau ya hali ya juu. Huko vijijini pamoja na kuwepo na miundombinu mibovu kulinganisha na mijini bado wanapata taarifa muhimu kwa yale ambayo yanajili katika nchi hii. Ni vijijini ambako bado watu wanajadiliana uso kwa uso katika masoko,misiba,arusi na zaidi jioni kwenye vilabu vya pombe. Zaidi wageni wanatokea mijini hupeleka taarifa na habari mbalimbali kwa njia ya mdomo kama ulivyokuwa ukienda huko kwa ajili ya NG

kibunango heshima yako mkuu...
kwanza kabisa kuna mstari umenisikitisha katika majibu uliyompa ndugu yetu kidzogolae. nimepata kupita katika vilabu vya pombe au hata kusikia tu taarifa zao wanaoongeaga wakiwa humo, mi sidhani kama kuna mlevi wa ubanda akishaanza kupata mambo yake ataweza kumueleza mwenzie mkasa wa chenge na vijisenti au rostam na richmond, kwa hilo mkuu nakupinga, na ni wazi kuwa alichokizungumzia huyo ndugu yangu ni ukweli ulio wazi ambao sijui hata ni kitu gani kinapelekea kujifinya nyuma ya kivuli kwa kuuogopa ukweli huu.
ni kweli watu wa vijijini wamelala na ni vipofu na ukitaka kuamini maneno ya mtoa mada subiri kifike kipindi cha uchaguzi kisha nenda bush then sikiliza kauli wanazoambiwa na wagombea wa CCM kuwa (mkichagua upinzani mtaleta vita). je kwa nini CCM huwa hawasemi kauli hizo mwembe yanga au jangwani hapa Dar? sasa CCM wanajua wa kuwaokota hivyo ni kina nani.
 
kibunango heshima yako mkuu...
kwanza kabisa kuna mstari umenisikitisha katika majibu uliyompa ndugu yetu kidzogolae. nimepata kupita katika vilabu vya pombe au hata kusikia tu taarifa zao wanaoongeaga wakiwa humo, mi sidhani kama kuna mlevi wa ubanda akishaanza kupata mambo yake ataweza kumueleza mwenzie mkasa wa chenge na vijisenti au rostam na richmond, kwa hilo mkuu nakupinga, na ni wazi kuwa alichokizungumzia huyo ndugu yangu ni ukweli ulio wazi ambao sijui hata ni kitu gani kinapelekea kujifinya nyuma ya kivuli kwa kuuogopa ukweli huu.
ni kweli watu wa vijijini wamelala na ni vipofu na ukitaka kuamini maneno ya mtoa mada subiri kifike kipindi cha uchaguzi kisha nenda bush then sikiliza kauli wanazoambiwa na wagombea wa CCM kuwa (mkichagua upinzani mtaleta vita). je kwa nini CCM huwa hawasemi kauli hizo mwembe yanga au jangwani hapa Dar? sasa CCM wanajua wa kuwaokota hivyo ni kina nani.
Kamanda gang chomba;
Heshima yako mkuu, michango yako hapa JF ni mizuri na yenye kutoa somo katika fani mbalimbali na hasa siasa.

Kampeni ya kutumia vitisho vya vita ilikuwa wakati ule Tz inaingia kwa mara ya pili katika mfumo wa vyama vingi... (Kumbuka kuwa baada ya uhuru tulikuwa na vyama vingi vilevile...) na huo ulikuwa mwaka 1995 ambapo Tz bara walikuwa ndio kwa wana mwaka mmoja wa kuangalia Tv, na hivyo kuwa ni tishio kweli kweli.. Ilhali huko Rwanda na Burundi mambo yalikuwa ni tete! Hivyo kwa ufupi ilikuwa ni njia mojawapo ya kampeni... kumbuka kuwa katika kampeni lolote linaweza kuzungumzwa kwa faida ya mpiga kampeni hiyo.

Nimesema na nitaendelea kusema kuwa huko Vijijini pamoja na mambo yote, inapofika jioni,wazee na vijana hukutana katika vilabu vya ulabu, lengo sio kuwa walevi bali ni kubadilishana mawazo.. Hivyo masuala ya siasa uzungumzwa vilevile...!
 
Huu ujumbe MZITO haya ni kweli yanatokea kabisa tena bila ubishi wowote..Jamaa hapa anamaanisha upofu wa kifikra wengi naona wameanza kumponda...
 
Lakini na wewe mtoa mada umesahau, Wamasai wanapenda Nyama, Wanyantuzu da!! nyama kwao ni haba,kwani wao pia ni wafugaji.

Hawa jamaa kwa rushwa ya nyama bwana wewe acha tu.

Pia unayajua maisha ya kjjni? kukiwa na kusanyiko kama hilo tu, basi watu mnajua mtashiba siku ile
 
Lakini na wewe mtoa mada umesahau, Wamasai wanavyopenda Nyama,je unajua ni ng'ombe wangapi walianguka? Wanyantuzu da!! nyama kwao ni haba,kwani wao pia ni wafugaji.

Hawa jamaa kwa rushwa ya nyama bwana wewe acha tu.

Pia unayajua maisha ya kjjni? kukiwa na kusanyiko kama hilo tu, basi watu mnajua mtashiba siku ile .

Napenda usiwalaumu haw watz wenzetu, ni njaa ndiyo inawafikisha hapo walipo na wala si vipofu kama unavyodhani.
 
Nakubaliana na mtoa mada kabisa watanzania wengi ni vipofu wa kifikra, magoigoi, mbumbumbu, wajinga, wapumbavu. Kama hao watu wa vijini wanajua uchafu wote unaofanywa na majambazi wa CCM halafu bado wanajipanga mistari kuwapigia vigelegele na kuwashangilia Mafisadi basi ni wapumbavu wa hali ya juu.

Inatia aibu kabisa ukichulia vijijini ndio waathirika wakubwa wa UFISADI unaofanywa na viongozi wetu, Maisha ya vijiji vingi ni ya kifukara sana, watu wako kwenye umasikini wa hali ya juu lakini leo hii bado wanawakumbatia hawa Majambazi. Kweli tuna safari ndefu sana.
 
Mkuu, naomba uelewe vizuri hii topic. bahati mbaya sijui wewe upo upande gani na upo kwaajili ya nini humu Jf. kwani, kuna wengine humu nimehisi ni makachelo wa selikali, na wengine wapo ili kuchangia na kuyafichua maovu tz kwa maslahi ya watz wote.

Nikija kwenye topic, mimi sijaja humu ndani ya JF mda mrefu, niliipenda kwasababu niliona mambo mengi ambayo hayaongelewi bayana mtaani,pamoja na kwamba watu wanajua, hapa yanaongelewe bayana. kuwepo humu si ufahari wowote kwangu, kwasababu hapa so ndo sehemu pekee napata information. ninafanya utafiti sana, na nipo kwenye jamii, najua kinachoendelea tz.

Ninaposema kuwa, watz wengi vijijini wana uelewa mdogo, nina uhakika na ninachoongea kwasababu nimeishi huko, nimefanya kazi na NGOs na kuishi na watu huko sana, na mara nyingi natembelea huko kwaajili ya shughuli zangu. hizo redio unazosema kuwa watu wanasikiliza, uwe na uhakika na unachoongea, na kwamba kila mtu ana afford kununua betri na hizo radio. Najua kati ya watu mia moja, mmoja anaweza akajua nusu ya kinachoendelea, ila asilimia 99 ya watu vijijini hawajui uhalisia juu ya nchi yetu. usifiche maovu bwana, hivyo vijisent ndo hela ingetosha kupeleka watu hao shule, na wangekuwa na broad knowledge ya kuelewa mambo. kama wanaelewa, kwanini walimpaparikia Chenge na Lowasa wakati wanajua ni mafisadi? cha kwanza hapa tz, inabidi tupigane na ujinga, halafu umasikini utajiengua wenyewe.

wewe jamaa unaonekana ni kada wa ccm.halafu, una uelewa sio mkubwa sana. hivi una uhakika na unachoongea kuwa watz vijijini wana access information vizuri na wanajua kinachoendelea selikalini vizuri na duniani vizuri?umeshawai kuishi village wewe, akili gani ya kuwa na uelewa kama huo wako?wewe uko wapi kwanza? duh!

katika utafiti wangu kila ninapopita iwe mjini au vijijini redio zinatumiwa kwa burudani zaidi kuliko habari
 
Jamani hili sio suala la kulifanyia mchezo,nikiangalia kwa kina naona heshima hii inatumika aidha kutoa onyo na kuisababishia CCM woga na kuiacha serikali kutotimiza wajibu wake wa kuwashughulikia watu ,vilevile uamsho mdogo wa kuwaelezea wananchi kupitia vyama vya upinzani kwa kumuanika kwanza kule anakotoka ,hili lilikuwa lifanywe pale tu mtuhumiwa anapoonekana ana madhambi ya ufisadi ,ilikuwa wananchi wa anakotoka mbunge walishwe maneno ya ukweli na athari alizozisababisha mbunge wao, hapa kuna kitu kimoja ambacho kama fisadi alikuwa anawasaidia watu wa anakotoka kwa kila kitu kuanzia ,kuwajengea zahanati kuwasaidia katika miradi mbali mbali na hata fedha ya mkononi na vile vile siku anazowapitia huko huwachinjia vijikuku na vijigombe watu wakajisikia kuwa wamefikiwa na mbunge wao ,kusema kweli hapo watakuwa hawana lawama ya kulaumiwa ni haki yao wampokee kwa vifijo na nderemo na ni shujaa wao kwa ufadhili wake hapo kijijini,mbunge wa aina hiyo ni tishio kwa serikali kwani hata akienguliwa katika Chama chake basi chama chochote atakachojiunga ataondoka na wafuasi wake na ndio maana huwa hawana wasiwasi na sokomoko ndani ya Chama anachotoka kwani Chama kinamtegemea kuwepo hapo.
Kwa ufupi ikiwa kumetokea kuvuja kwa siri za mbunge kama walivyozipata akina Zitto na wenziwe basi hawa walikuwa watumie underground ya kueneza habari hizi kule kwa mbunge mwenyewe wamwage na kumwagilia mbolea machafu ambayo ,wanakijiji hawana habari nayo hata kuwaeleza kuwa hivi vijikuku na vigombe si lolote si chochote kwa fedha anayoiba ,huyu anawalisha kwa kutumia fedha ya wizi ni shetwani anatafuta wa kumsaidia kubeba dhambi maana anahusika na wizi huu na huu na ule na mwisho hata likiripuka bomu jamaa wa vijijini watatamani watapike walichokula ila mtawapoza kwa kuwaambia mlikuwa mnakula feza yenu na hivyo hakuna cha kubabaika.Sio rahisi lakini mbinu za kisiasa zinaweza kuwafungua macho wanao ishi huko vijvijini kwa fedha kidogo wanayoiba mafisadi ambayo hutengea fungu kulipeleka kwa wapiga kura wao ili mambo yakiharibika waweze kupata sapoti ya kiasi fulani na kuwa tishio kwa serikali na serikali ndipo inaposhindwa kutrekeleza majukumu yake kwa wahujumu uchumi waliobobea ambao hawaibi mafuta ya taa na dizeli bali wanaingia huko huko kunakokusanywa vijisenti vya walala hoi na kuvishughulikia kwa mkupuo.
Moja ya siri za vyama vya siasa ni kuwa kuna watu hamuwezi kuwafukuza ,kwa mfano mwenyekiti mnaweza mkamfukuza ,Katibu na wengine wengine lakini linapoingia suala la kumfukuza mbunge hapo kuna tabu na si mara nyingi kutokea kumfukuza mbunge aliechaguliwa kwa kura za wananchi kwani mbunge wa kuchaguliwa na wananchi ni hazina ya Chama sasa kuiondoa hazina ni kusababisha kupunguza nguvu ya Chama.Hivyo msitegemee CCM kuwafukuza watu hawa ,CCM itangojea sheria ichukue mkondo wake lakini si kuwafukuza hilo nina uhakika nalo .kwani kisiasa ndivyo inavyofanyika kwa vyama vyote.
 
Back
Top Bottom