Baadhi ya wabunge wa CCM na Upinzani wadaiwa kuhongwa na menejimenti ya TANESCO

Ukichambua vizuri, asilimia kubwa ya wana JF ni Chadema au wanaipenda CDM hata kama si wanachama. Nawaomba sana wana CDM na woote wanaoipenda CDM humu JF muwe makini sana kuchangia hizi hoja, manake kuna njia nyingi sana adui anazitumia kukulainisha. Chuki za wana CDM (baadhi yao) kwa Mh. Zitto Kabwe zinawafanya CCM wapate habari nyingi sana za kukichambua CDM na kupata data kamili za kukiangamiza 2015.

Kabla hamjashtuka, mtakuwa mmekwisha na umoja wa CDM utakuwa ni ndoto kuchukua nchi 2015. Ukifuatilia vizuri, CCM kwa sasa wanapigana sana kurudisha heshima ya chama iliyopotea miaka takribani saba iliyopita (kipindi cha Rais Kikwete) kutokana na makundi. Gharama ya kurudisha umoja huo ni kubwa sana na sometimes usipokuwa makini by the time unarudisha umoja huo, it will be too late, kinachobaki ni kusema TUNGEJUA!

Msiingie kwenye mtego wa kukipeleka chama cha CDM kwenye makundi, kwani itawagharimu sana kurudisha umoja huu. WATCH OUT!

Lakini hapa issue ni ufisadi,Zitto atoe tamo kama hahusiki, zitto alianza kubadilika alipopewa kuwa mwenyekiti kamati ya madini
 
Nimefurahishwa sana jinsi BUNGE lilivyo isambaratisha timu ya mafisadi wa TANESCO ndani ya BUNGE,kauli zangu zimetimia juu ya mtandao mpana wa MAFISADI kuweka mizizi ndani ya vyama PINZANI.....nawaombena wabunge muwe makini mnapopata ushawishi hasi katika kufanya maamuzi yenye masilahi kwa umma.Hata kura ya kutokuwa na IMANI kwa WAZIRI MKUU ulikuwa mpango wa MAFISADI kuivuruga SERIKALI ili waweza kuiba zaidi ,kwani kila mnapo badili uongozi wao wanapata nafasi ya kuweka watu wao !

Wote wanaotangaza nia ya kuwa MARAIS kwa sasa ni wahuni na MAFISADI wakuogopwa,watatumia vyombo vya habari kupata umaarufu ili wananchi wawaamini kwa dhamira za unafiki.Tuna miaka 3 zaidi ya kufanya kazi za maendeleo badala yakuleta attention za URAIS,mara Wanachama X wahamia chama X,huu ni ujinga.Wasitumie majina ya vyama kuwavuruga wananchi na kuwakatisha tamaa juu ya SERIKALI yao ili wapate kutawala.

Hongera sana Mh.Selasini,Anne Kilango,Mh.Lugola nk...
Najuta kumuona OLE SENDEKA kwenye kambi ya MAFISADI...shame upon u........Hawa ndiyo wasaliti wa mapambano ya ufisadi
 
Mbinu chafu za urais CDM, wa kaskazini wapo kazini.

Wewe kwenu singida achilia mbali iramba, ni lini mtatoa rais? Manake wewe first class ikonomisti uko hooooooooi bora ambao hawajakwenda shule. Halafu ukome kuwaandikia tamko la kanusho tiss, manake "umeripoti" kama uko igunga vile!!!!!
Tuambie hivi watakurudisha ukampeni meneja igunga? Manake ngoma inarudiwa ile!!!!! Mlipanda kwenye shamba sio lenu!!!!
Kwiiii!!!! Kwi kwii
 
Zitto kauli zake tata na za ubinafsi ndizo zinamponza anajifanya anajua kuliko wenzake wote pale CDM!
 
Hiv punde Bungeni, Vita Rashid Kawawa ametoa Hoja akiliomba Bunge liafiki Watuhumiwa wa Kuhongwa ili kumlinda CEO wa TANESCO aliyesimamishwa ndg. Muhando.

Hoja ya Rashid Kawawa inapendekeza kuwajadili wahusika na kuvunja Kamati zao yaani Kamati za Bunge wanazoziongoza. Wajumbe lukuki wamesimama kuiunga Hoja hiyo mkono japokuwa mbinu za Kikanuni huenda zikaathiri kujadiliwa kwa jambo hili kwani nilimsikia Spika wa Bunge akiweka kizuizi ktk kujadilika kwa Hoja ya Kawawa.

Endapo hoja ya Kawawa itapewa uzito huku Zitto akiwa miongoni mwa watuhumiwa, huenda yeye mwenyewe ama kamati yake wakaangamia ki-respect Bungeni.
 
Liwalo na Liwe! Liliwalo na Liliwe! Ukitaka KULA lazima ULIWE! Watanzania tuliwe hadi lini? I support Nyalutumbwi: We need ONE voice to prosecute in the court of law all those implicated in the matter!
 
Kwa jinsi suala hili lilivyofikia Zitto anahitaji kukaa na wadau ili aweze kupangua hoja hizi!! lakini Zitto alivyo mbinafsi na kujifanya mjuaji atakuja hapa na thread yake tata ambayo badala ya kutatua akaharibu kabisa>>akae na viongozi wake wajipange kupangua hii hoja!
 
Hiv punde Bungeni, Vita Rashid Kawawa ametoa Hoja akiliomba Bunge liafiki Watuhumiwa wa Kuhongwa ili kumlinda CEO wa TANESCO aliyesimamishwa ndg. Muhando.

Hoja ya Rashid Kawawa inapendekeza kuwajadili wahusika na kuvunja Kamati zao yaani Kamati za Bunge wanazoziongoza. Wajumbe lukuki wamesimama kuiunga Hoja hiyo mkono japokuwa mbinu za Kikanuni huenda zikaathiri kujadiliwa kwa jambo hili kwani nilimsikia Spika wa Bunge akiweka kizuizi ktk kujadilika kwa Hoja ya Kawawa.

Endapo hoja ya Kawawa itapewa uzito huku Zitto akiwa miongoni mwa watuhumiwa, huenda yeye mwenyewe ama kamati yake wakaangamia ki-respect Bungeni.

Wapiga kelele wote bungeni wameshtukiwa, tangu jana SELASINI ndiye aliyeanza. ZITTI, MNYIKA na wengine wanaojifanya wapiga domo sana sasa wameshtukiwa kuwa midomo yao inawezeshwa kwa kiasi kikubwa.
 
CCM wamepanga na kupika hili ili kuvuruga watu wasiibane hii wizara ya nishati! Thats why kila mbunge akisimaa anaipongeza hii wizara! Mimi naunga mkono iundwe tume huru kuchunguza hili sakata utakuta Mhando na hawa mawziri lao moja!
 
Duh Zitto kapendeza !.

GO9G9056.JPG
 
hizi shutuma za yeye kupewa hela ili kutetea maslahi flani ndani ya tanesco mbona zitto hazikanushi? mpaka tunaanza kufikiria ni za kweli...kuna wakati nafikiria cdm inaweza kuja kua worse than ccm..mana bora ccm wameshakula matumbo yamejaa wakiingia watu ambao wana njaa na wao wanataka kushiba itakuaje
Ndugu yangu weee....hakuna anayechoka kutafuta.! Hata Kina Gates wanatafuta bado, Kina Bakhresa wanabuni kupika mpaka maandazi, hata wabunge wataka waongezewe posho ambazo tayari ni kufuru.......huwa hazitoshi....
 
Ninajaribu kuunganisha dots ,urais ,utetezi wa dowans,utetezi wa richmond ,utetezi wa akina mhando ,nimejua ss kwamba zito yupo upande gani,kwa siku za karibuni badala ya kuimarisha chama chake ndio amekuwa akitumika kukisambalatisha,ss ambao kasaikolojia kapo kidogo tumeshajua zito yupo upande gani,zito wa leo ni tofauti na yule wa miaka 7 nyuma,sasa awe amepokea rushwa au hajapokea sisi wengine tunamjaji kwa matendo yake km kiongozi
 
mafisadi wapo pote sio sisiem peke yake hata CIDIEM pia wapo na ndo wanaanza kujionesha, tuwe makini sana na watu kama zito
 
Ishu ya ufisadi mkubwa uliofanyika Tanesco huku mh Zitto (mb-Chadema), ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mashirika ya umma, akipinga hatua zilizochukuliwa dhidi ya mkurugenzi mkuu wa Tanesco ndugu Muhando imemchafua sana kisiasa na kushusha "credibility" yake kwa umma kwani yeye na wabunge wenzake 'mafisadi' wametuhumiwa kupokea kupokea rushwa ili kumtetea Mkurugenzi huyo wa Tanesco. Ishu hii imeibuka bungeni ambapo wabunge wengi wamemsema sana. Akiwa mbunge ambaye aliaminika sana nchini, je hili linaweza kuashiria mwisho wake kisiasa?
 
watu wanajua kutumia karama zao!! watu rhetoric wanahitaji kuwasikiliza kwa umakini sana - iwe kwa mabaya au "mazuri".
 
Back
Top Bottom