Baadhi ya viongozi wa DRC wakatazwa kuingia Marekani

Fang

Content Manager
Nov 5, 2008
509
322
Marekani imesema Ijumaa kuwa iko pamoja na watu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kufuatia zoezi la kihistoria la kukabidhiana madaraka na kutangaza katazo la kuingia Marekani kwa maafisa kadhaa kutoka tume huru ya uchaguzi (INEC), serikali na jeshi la nchi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo anaweka wazi kwamba, kutokana na kujihusisha katika ufisadi mkubwa unaohusiana na mchakato wa uchaguzi, watu wafuatao: Corneille Nangaa, Mwenyekiti wa Tume huru ya uchaguzi (CENI) ya DRC, Norbert Basengezi Katintima, Makamu mwenyekiti wa CENI; Marcellin Mukolo Basengezi, Mshauri wa Mwenyekiti wa CENI; Aubin Minaku Ndjalandjoko, Spika wa Bunge la Taifa la DRC; na Benoit Lwamba Bindu, Rais wa Mahakama ya Katiba DRC, na familia zao za karibu hawataruhusiwa kuingia nchini Marekani.

Taarifa hiyo ya wizara imesema kuwa Kifungu 7031 cha Sheria ya Wizara ya Mambo ya Nje, operesheni za nje ya nchi imempa madaraka wakati wowote Waziri wa Mambo ya Nje akiwa na taarifa za uhakika kuwa maafisa wa serikali za kigeni wamejihusisha na ufisadi mkubwa au kuvunja kabisa haki za binadamu, watu hao na familia zao wasiruhusiwe kuingia Marekani.

Waziri huyo wa Mambo ya Nje pia ameweka katazo la viza kwa maafisa wa uchaguzi na maafisa wa serikali na jeshi ambao wanasadikiwa kuwa wamehusika kwa kusaidia, au kujihusisha na uvunjifu wa haki za binadamu au unyanyasaji au ukandamizaji wa mchakato wa demokrasia nchini DRC.

Taarifa hiyo ya wizara imesema kuwa watu hawa wamejitajirisha kupitia ufisadi, wameamrisha au kusimamia uvunjifu wa amani dhidi ya raia, wakati wananchi hao walipokuwa wanatekeleza haki zao za kukusanyika kwa amani na uhuru wa kujielezea. Walikuwa wanaendesha mambo bila ya kujali kwamba wanawaathiri wananchi wa Congo na wamekuwa wakionyesha waziwazi kutojali kwao misingi ya demokrasia na haki za binadamu.

Wizara ya Mambo ya Nje imesisitiza kuwa hatua hii iliyotangazwa leo inaelekezwa kwa maafisa maalum na siyo kwa wananchi wa Congo au serikali mpya iliyoingia madarakani.

Uamuzi huu unaonyesha nia ya Wizara ya Mambo ya Nje kuendelea kushirikiana na serikali mpya ya DRC katika kutekeleza ahadi zake za kutokomeza ufisadi na kuimarisha demokrasia na kuwajibika, na kuheshimu haki za binadamu.

Uchaguzi uliofanyika unaonyesha nia ya watu wa DRC kuleta mabadiliko na kuwa na taasisi za serikali zenye kuwajibika. Lakini hata hivyo kuna malalamiko ya kisheria juu ya mchakato wa uchaguzi jinsi ulivyoendeshwa na uwazi wake.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marekani yapiga marufuku baadhi ya viongozi wa DRCongo na familia zao kuingia nchini humo. Wanadai walipika matokeo ya uchaguzi. Yumo MK wa Tume, Jaji Mkuu, Rais wa Bunge, Rais wa Mahakama ya Katiba, baadhi ya Wanajeshi Waandamizi na Serikali.

-------------
The United States said Friday it will refuse visas to the Democratic Republic of Congo's election chief and top judge on charges that they undermined long-awaited presidential polls.

Washington said it wanted to send a clear signal of the need for accountability in the conflict-torn nation but stressed that it will still work with the controversially elected new president, Felix Tshisekedi.

The United States said it would refuse visas to five senior figures as well as their immediate family members over "involvement in significant corruption relating to the election process."

They include Corneille Nangaa, president of the Independent National Election Commission, Benoit Lwamba Bindu, the president of the Constitutional Court and Aubin Minaku Ndjalandjoko, president of the National Assembly.

The State Department said it was also imposing visa restrictions on an unspecified number of other military and government officials over human rights abuses related to the election.

"These individuals enriched themselves through corruption, or directed or oversaw violence against people exercising their rights of peaceful assembly and freedom of expression," the State Department said in a statement.

"They operated with impunity at the expense of the Congolese people and showed a blatant disregard for democratic principles and human rights," it said.

The United States and other international players had been closely watching the December 30 election, which marked the first peaceful transfer of power in sub-Saharan Africa's most vast country since independence from Belgium in 1960.

Martin Fayulu, a former oil executive considered a favorite, alleged widespread fraud and accused Tshisekedi of collaborating with outgoing president Joseph Kabila.

Despite recognizing concerns over the election, regional and world powers led by South Africa quickly coalesced behind Tshisekedi in hopes of preventing greater instability.

US bans DRC election chief, top judge over vote conduct
 
Nilitaka nijibu kama wewe,umeniwahi tu....
Ngoja waje vibaraka wa pro mabeberu!

Sent using Jamii Forums mobile app

Wewe mvuta Bangi lazima uwe na majibu kama hayo kwani Akili yako ni ya kiwendawazimu kama ya cyprian Musiba aliyewakaririsha neno mabeberu na nyie vilaza kukariri pasipo kujua hao mabeberu ndiyo wafadhili wa CCM wanatoa 40% ya Bajeti ya Tanzania, mkiwaita Barrick ikulu mnawaita wanaume na wazungu wakiwapa pesa mnawaita wafadhili Nchi rafiki lakini cha ajabu hao wazungu wakiongea na Wapinzani mnawaita mabeberu yaani CCM yote mmekariri Akili finyu za cyprian Musiba bila aibu.
 
Wewe mvuta Bangi lazima uwe na majibu kama hayo kwani Akili yako ni ya kiwendawazimu kama ya cyprian Musiba aliyewakaririsha neno mabeberu na nyie vilaza kukariri pasipo kujua hao mabeberu ndiyo wafadhili wa CCM wanatoa 40% ya Bajeti ya Tanzania, mkiwaita Barrick ikulu mnawaita wanaume na wazungu wakiwapa pesa mnawaita wafadhili Nchi rafiki lakini cha ajabu hao wazungu wakiongea na Wapinzani mnawaita mabeberu yaani CCM yote mmekariri Akili finyu za cyprian Musiba bila aibu.
Huyo msiba mumeo brother? Para yote unamtaja taja,kama haja kuachia pesa ya mboga kamfuate ofisini akupe pesa...



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marekani yapiga marufuku baadhi ya viongozi wa DRCongo na familia zao kuingia nchini humo. Wanadai walipika matokeo ya uchaguzi. Yumo MK wa Tume, Jaji Mkuu, Rais wa Bunge, Rais wa Mahakama ya Katiba, baadhi ya Wanajeshi Waandamizi na Serikali.

US bans DRC election chief, top judge over vote conduct
Ukiona wa Tanzania hapigwi ban ujue uchaguzi ni huru na haki.
Plus, mkongo mzuie asiende ubelgiji au ufaransa utakuwa umemkomoa, sio usa.
 
Watetezi wa CCM kwa 100% ni mbumbumbu zuzu juha na vilaza wa kutupwa na wengi wapo Gheto kwa Le mutuz na cyprian Musiba wakiwalisha maharage kuwavutisha Bangi kuwakaririsha upumbavu wao kisha kuwatuma kuja mitandaoni kuwasumbua watu ni Aibu kwa chama kikubwa kama CCM kuwategemea watu mapunguani kama Le mutuz na cyprian Musiba kuwaandalia vijana wa kuwatetea mitandaoni ndiyo maana utetezi wa CCM unafanana maana wote wamekariri kitu kimoja na hawana uwezo wa kujiongeza kutokana uvutaji Bangi wa kutisha.
 
Back
Top Bottom