Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,888
- 143,986
Kwa tafsi rahisi naweza kusema Vicoba ni vikundi vya watu/wajasiriamali kwa madhumuni ya kuweka akiba na kukopeshana na pia kugawana faida/gawio.
Hata hivyo,hili la kugawana faidi kwangu mimi naliona si jambo sahihi sana pale vikundi hivi vinapokuwa bado ni vichanga kwa maana ya uwezo wa kukopeshana kulingana na mahitaji.
Kwa mfano,wanasema kila baada ya mwaka mmoja,kikoba kinapaswa kuvunjwa na watu kugawana faida iliyopatikana kama ambavyo mabenki hutoa gawio kwa wana hisa wake.
Hapa kinachonishangaza watu kuwa tayari kuvunja na kugawana faida kila mwaka wakati vikundi hivi baadhi haviwezi hata kukopeshana kulingana na mahitaji ambapo wakti mwingine watu hulazimika kupewa mikopo kwa zamu kutokana na mahitaji kuzidi makusanyo ya vikao husika.
Sasa hap ndio huwa najiuliza katika hali hii watu waridhikaje kuvunja hivi vikoba kisa tu ni mwaka umetimia?
Kwanini wasifikirie kuongeza hisa/akiba wanazotoa kwa kila kikao na badala yake wanawaza tu kuvunja?
Kama ni kugawana faida,kwanini isiwe ni hatu ya baadae baada ya kikoba kuwa na mtaji wa kutosha kiasi kwamba wakati mwingine hela zinabaki nyingi tu baada ya wanakikundi kukopa?
Jambo au taratibu zingine za kushangaza ni zile za kuweka ukomo wa kutoa hisa/akiba kwenye kila kikao.
Kwa mfano,kuna vikoba vingine huweka kiwango cha juu(maximumu) ambachi katika kikao kimoja,mtu hutaruhusiwa kuweka zaidi ya kiasi kilichowekwa ili kuongeza akiba/hisa zako katika chama/kikundi.
Na utaratubu wa baadhi ya vikoba kuruhusu watu kukopa au kuweka hela siku ya vikao tu nao ni sahihi?
Kwanini wanakikundi wasiwe huru kuweka na kukopa wakati wowote kama hela ipo mradi tu kuna kuwa na records nzuri zinazowesha kujua nani kaweka kiasi gani leo na nani amekopa kiasi gani siku fulani,n.k?
Vikundi vingine zikiwemo Saccos,haviruhusu mtu kuchukua mkopo mpaka ule wa mwanzo uishe hata kama mtu amebakiza rejesho moja au mawili eti shariti ni mpaka amalize deni lote.
Kwangu mimi,utaratibu huu una maana tu pale kikundi kinapokuwa na mtaji mdogo ambapo inategemea wenye mikopo walipe na wengine waweze kukopeshwa ila si utaratibu sahihi kwa kikundi ambachon teyari kina mtaji mkubwa na fedha nyingi inabaki badala ya kukopeshwa kwa wanachama kisa tu taratibu haziruhusu hata kama utaratibu unazuia watu kukopa.
Sometimes huwa nahisi huenda watu wa mabenki na taasisi zingine za kifedha labda ndio zilizo nyuma ya baadhi ya taratibu/sheria hizi ambazo zinadumaza vikoba kwani vikoba ni tishio kwa kwa taasisi hizi zinazotoa mikopo kwa riba kubwa tofauti na hivi vikoba.
Naomba mawazo yenu juu ya mambo haya hasa kwa wataalamu wa mambo ya biashara,fedha au banking,n.k kwa lengo la kuboresha kwani penye watu wegi,hapaaribiki neno.
Naandikia nikiwa katika mkoa mmoja wa kaskazini mwa nchi hii.
Hata hivyo,hili la kugawana faidi kwangu mimi naliona si jambo sahihi sana pale vikundi hivi vinapokuwa bado ni vichanga kwa maana ya uwezo wa kukopeshana kulingana na mahitaji.
Kwa mfano,wanasema kila baada ya mwaka mmoja,kikoba kinapaswa kuvunjwa na watu kugawana faida iliyopatikana kama ambavyo mabenki hutoa gawio kwa wana hisa wake.
Hapa kinachonishangaza watu kuwa tayari kuvunja na kugawana faida kila mwaka wakati vikundi hivi baadhi haviwezi hata kukopeshana kulingana na mahitaji ambapo wakti mwingine watu hulazimika kupewa mikopo kwa zamu kutokana na mahitaji kuzidi makusanyo ya vikao husika.
Sasa hap ndio huwa najiuliza katika hali hii watu waridhikaje kuvunja hivi vikoba kisa tu ni mwaka umetimia?
Kwanini wasifikirie kuongeza hisa/akiba wanazotoa kwa kila kikao na badala yake wanawaza tu kuvunja?
Kama ni kugawana faida,kwanini isiwe ni hatu ya baadae baada ya kikoba kuwa na mtaji wa kutosha kiasi kwamba wakati mwingine hela zinabaki nyingi tu baada ya wanakikundi kukopa?
Jambo au taratibu zingine za kushangaza ni zile za kuweka ukomo wa kutoa hisa/akiba kwenye kila kikao.
Kwa mfano,kuna vikoba vingine huweka kiwango cha juu(maximumu) ambachi katika kikao kimoja,mtu hutaruhusiwa kuweka zaidi ya kiasi kilichowekwa ili kuongeza akiba/hisa zako katika chama/kikundi.
Na utaratubu wa baadhi ya vikoba kuruhusu watu kukopa au kuweka hela siku ya vikao tu nao ni sahihi?
Kwanini wanakikundi wasiwe huru kuweka na kukopa wakati wowote kama hela ipo mradi tu kuna kuwa na records nzuri zinazowesha kujua nani kaweka kiasi gani leo na nani amekopa kiasi gani siku fulani,n.k?
Vikundi vingine zikiwemo Saccos,haviruhusu mtu kuchukua mkopo mpaka ule wa mwanzo uishe hata kama mtu amebakiza rejesho moja au mawili eti shariti ni mpaka amalize deni lote.
Kwangu mimi,utaratibu huu una maana tu pale kikundi kinapokuwa na mtaji mdogo ambapo inategemea wenye mikopo walipe na wengine waweze kukopeshwa ila si utaratibu sahihi kwa kikundi ambachon teyari kina mtaji mkubwa na fedha nyingi inabaki badala ya kukopeshwa kwa wanachama kisa tu taratibu haziruhusu hata kama utaratibu unazuia watu kukopa.
Sometimes huwa nahisi huenda watu wa mabenki na taasisi zingine za kifedha labda ndio zilizo nyuma ya baadhi ya taratibu/sheria hizi ambazo zinadumaza vikoba kwani vikoba ni tishio kwa kwa taasisi hizi zinazotoa mikopo kwa riba kubwa tofauti na hivi vikoba.
Naomba mawazo yenu juu ya mambo haya hasa kwa wataalamu wa mambo ya biashara,fedha au banking,n.k kwa lengo la kuboresha kwani penye watu wegi,hapaaribiki neno.
Naandikia nikiwa katika mkoa mmoja wa kaskazini mwa nchi hii.