Baadhi ya Sheria ambazo zinaiangusha Serikali ya CCM

Loxodona

JF-Expert Member
Apr 3, 2019
354
618
Katika kipindi cha Utawala wa CCM kuna Sheria zilitungwa na kupitishwa na Wabunge wa CCM bila kutumia Busara. Leo hii zinaigharimu Serikali ya CCM.

1) Sheria ya FAO LA KUJITOA na KIKOKOTOO KIPYA. Sheria hii ni Sheria yakipuuzi Sana. Sheria hii haimuhusu Rais wala Mbunge Ila inawahusu watumishi wa Umma na wa Private Sekta Tu. Kama Sheria hii ni Nzuri Kwanini isiwahusu Wabunge waluoitunga na Rais aliyeisign?? Kwa Sheria hii ukiacha kazi leo Kwa hiari yako Ili ujifanyie Mambo yako, mafao yako hupati Hadi ufikishe umri wa Miaka 60. Ikumbukwe hii ni fedha ya Mfanyakazi, anapaswa kuwa na Uhuru nayo mana ni Haki yake. Ila wabunge wa CCM Kwa majigambo na Kebehi nyingi wakaipitisha na Rais Akaisaini Ili itumike. Aidha, kuhusu KIKOKOTOO Kwa wastaafu. Huu ni Mwiba mwingine Kwa watumishi wastaafu wa sekta zote isipokuwa Wabunge na Marais.

2) Sheria ya "MALUPULUPU" ya Viongozi wa Kisiasa. Tumeona juzi Maraisi wetu wanajengewa Majumba ya Kifahari, wanalipwa mshahara 80% ya mshahara wa Rais aliyepo madarakani, wanatibiwa nje ya Nchi Kwa mabilioni ya Wananchi fukara kama alivyotibiwa Ndugai Kwa Kulala hotelini. Mishahara Yao mikubwa Ila haikatwi Kodi. Sheria hizi ni kandamizi na ni za kinyonyaji. Nchi zilizoendelea hazina upuuzi huu wa kifalme, Mathalan, Kwanini wasikatwe Kodi wkt kila mwananchi ana wajibu wa Kulipa Kodi??? Viongozi wa kisiasa ni watumishi kama wengine so wanachofanyiwa wao wafanyiwe pia na watumishi wengine. Otherwise, tuachane na Sheria za kinyonyaji hizi. Yani mumuhudumie mtu akiwa madarakani, na akistaafu pia mumuhudumie? Pension yake inafanya kazi gani? Mbaya zaidi wawapo madarakani hawawagi waaminifu, wanatuibia via mikataba ya kishenzi.

3) Sheria ya Vyombo vya Habari. Hapa pia kuna Sheria ya Kikoloni. Kimsingi Sheria hii inaviziba mdomo Vyombo vyetu vya habari. Wabunge wa CCM walipitisha Sheria hii Kwa dharau na Kebehi nyingi na kujisahau kuwa Nchi hii ni Mali ya Wananchi.

4) Sheria ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Sheria hii ilipitishwa kibabe na kupandisha makato Hadi kufikia 15% ya mshahara Kwa Mwezi kinyume na mikataba. Aidha, kuna urasimu na ubaguzi mwingi wakati wa kuomba hiyo Mikopo. Sheria hii inagusa familia nyingi za wafanyakazi na waombaji wa Mikopo (Wanafunzi).

Wakati tunaikaribia Siku ya tarehe 28/10/2020. Tutafakari namna Sheria hizi kandamizi zilivyotungwa, wahusika waliozitunga na kuzipitisha na Malengo Yao hasa. Halafu tupime kama wanasifa ya kuendelea kutuongoza.

Haiwezekan ujinasibu kiwa unawapenda wafanyakazi halafu unapitisha Sheria ya FAO la KUJITOA au LiKIKOKOTOO la ajabu. Tena ni Kwa watumishi wa chini Tu na sio wabunge waliotunga Sheria hiyo.

Huwezi sema unawapenda wananchi wakati Unawanyonya Kwa kupitishwa Sheria za kinyonyaji na zenye kuakisi ubinafsi mkubwa.

Huwezi sema nchi ipo Huru wkt mnatunga Sheria zinazodhibiti Uhuru wa wananchi wa kuexpress hoja zao.

Haiwezekan useme unawapenda Wanafunzi halafu unawabagua kwenye kupata Mikopo wakati Baba zao wanalipa Kodi kubwa kuliko wale wanaopata Mikopo kisa Tu walisoma Private.

Sheria hizi ni mfano wa Sheria nyingi zilizotungwa na Bunge letu linaloongozwa na idadi kubwa ya Wabunge wa CCM ambazo zinaashiria hawajui wajibu wao na wawapo Bungeni mana wanadhani wapo pale Kwa NIABA Yao wenyewe. Yaani wanasahau kupigania maslahi ya Wananchi waliowatuma. Hivyo, tukumbuke Sheria hizi wakati tunasogelea sanduku la Kura tarehe 28/10/2020.
 
Ccm wameshindwa kutatua suala dogo la migogoro ya ardhi kweli?!
Suala la kulipa fidia nalo hawaliwezi,
 
Mleta mada uko sahihi kabisa na kwa asilimia mia moja, serikali hii imejaa dhuluma kwa wananchi na haifai kabisa kuachwa iendeleze dhuluma yake kwa wananchi ambao wamegeuzwa watumwa ktk nchi yao.

Wanafunzi wanaohitimu kujiunga na elimu ya juu wanabaguliwa kupewa mikopo kwa kisingizio cha kijinga kama kusomea private nk.

Huwezi kumwambia mtu anayeacha kazi eti asubiri hadi afikishe miaka 60 eti ndio apate mafao yake, na akifariki je si ndio anakuwa kalaliwa hivyo.

It's high time this government is voted out and start again from zero.
 
Katika kipindi cha Utawala wa CCM kuna Sheria zilitungwa na kupitishwa na Wabunge wa CCM bila kutumia Busara. Leo hii zinaigharimu Serikali.

1) Sheria ya FAO LA KUJITOA na KIKOKOTOO KIPYA. Sheria hii ni Sheria yakipuuzi Sana. Sheria hii haimuhusu Rais wala Mbunge Ila inawahusu watumishi wa Umma na wa Private Sekta Tu. Kama Sheria hii ni Nzuri Kwanini isiwahusu Wabunge waluoitunga na Rais aliyeisign?? Kwa Sheria hii ukiacha kazi leo Kwa hiari yako Ili ujifanyie Mambo yako, mafao yako hupati Hadi ufikishe umri wa Miaka 60. Ikumbukwe hii ni fedha ya Mfanyakazi, anapaswa kuwa na Uhuru nayo mana ni Haki yake. Ila wabunge wa CCM Kwa majigambo na Kebehi nyingi wakaipitisha na Rais Akaisaini Ili itumike. Aidha, kuhusu KIKOKOTOO Kwa wastaafu. Huu ni Mwiba mwingine Kwa watumishi wastaafu wa sekta zote isipokuwa Wabunge na Marais.

2) Sheria ya "MALUPULUPU" ya Viongozi wa Kisiasa. Tumeona juzi Maraisi wetu wanajengewa Majumba ya Kifahari, wanalipwa mshahara 80% ya mshahara wa Rais aliyepo madarakani, wanatibiwa nje ya Nchi Kwa mabilioni ya Wananchi fukara kama alivyotibiwa Ndugai Kwa Kulala hotelini. Mishahara Yao mikubwa Ila haikatwi Kodi. Sheria hizi ni kandamizi na ni za kinyonyaji. Nchi zilizoendelea hazina upuuzi huu wa kifalme, Mathalan, Kwanini wasikatwe Kodi wkt kila mwananchi ana wajibu wa Kulipa Kodi??? Viongozi wa kisiasa ni watumishi kama wengine so wanachofanyiwa wao wafanyiwe pia na watumishi wengine. Otherwise, tuachane na Sheria za kinyonyaji hizi. Yani mumuhudumie mtu akiwa madarakani, na akistaafu pia mumuhudumie? Pension yake inafanya kazi gani? Mbaya zaidi wawapo madarakani hawawagi waaminifu, wanatuibia via mikataba ya kishenzi.

3) Sheria ya Vyombo vya Habari. Hapa pia kuna Sheria ya Kikoloni. Kimsingi Sheria hii inaviziba mdomo Vyombo vyetu vya habari. Wabunge wa CCM walipitisha Sheria hii Kwa dharau na Kebehi nyingi na kujisahau kuwa Nchi hii ni Mali ya Wananchi.

4) Sheria ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Sheria hii ilipitishwa kibabe na kupandisha makato Hadi kufikia 15% ya mshahara Kwa Mwezi kinyume na mikataba. Aidha, kuna urasimu na ubaguzi mwingi wakati wa kuomba hiyo Mikopo. Sheria hii inagusa familia nyingi za wafanyakazi na waombaji wa Mikopo (Wanafunzi).

Wakati tunaikaribia Siku ya tarehe 28/10/2020. Tutafakari namna Sheria hizi kandamizi zilivyotungwa, wahusika waliozitunga na kuzipitisha na Malengo Yao hasa. Halafu tupime kama wanasifa ya kuendelea kutuongoza.

Haiwezekan ujinasibu kiwa unawapenda wafanyakazi halafu unapitisha Sheria ya FAO la KUJITOA au LiKIKOKOTOO la ajabu. Tena ni Kwa watumishi wa chini Tu na sio wabunge waliotunga Sheria hiyo.

Huwezi sema unawapenda wananchi wakati Unawanyonya Kwa kupitishwa Sheria za kinyonyaji na zenye kuakisi ubinafsi mkubwa.

Huwezi sema nchi ipo Huru wkt mnatunga Sheria zinazodhibiti Uhuru wa wananchi wa kuexpress hoja zao.

Haiwezekan useme unawapenda Wanafunzi halafu unawabagua kwenye kupata Mikopo wakati Baba zao wanalipa Kodi kubwa kuliko wale wanaopata Mikopo kisa Tu walisoma Private.

Sheria hizi ni mfano wa Sheria nyingi zilizotungwa na Bunge letu ambazo zinaashiria hawajui wajibu wao na wawapo Bungeni wanadhani wapo pale Kwa NIABA Yao wenyewe. Yaani wanasahau kupigania maslahi ya Wananchi waliowatuma. Hivyo, tukumbuke Sheria hizi wakati tunasogelea sanduku la Kura tarehe 28/10/2020.
Sheria ya vyama vya siasa
Sheria ya madini nako ni kituko kinachoshangiliwa
 
Mungu aiepushie mbali ccm, imeikandamiza sana nchi yetu......kilio kila mahali, siyo wakulima, siyo wafanyabiashara, siyo wafanyakazi, siyo wavuvi. Tufanye maamuzi ya Hekima trh 28.10 Twende na Mpenda HAKI, UHURU na MAENDELEO YA WATU...Tundu Lissu
 
Sheria ya vyama vya siasa
Sheria ya madini nako ni kituko kinachoshangiliwa
Ni kweli Sheria ya Vyama vya Siasa ipo Kwa ajili ya kukandamiza vyama pinzani na kustawisha chama Tawala. Sheria hii nayo inapaswa kufutwa mana ni Sheria ya kikaburu. Haipwasi kutumika katika nchi Huru yenye Katiba inayotambua Uhuru ktk association.

Hali kadhalika, Sheria ya Madini pia inampa mamlaka mgeni flan kumiliki Leseni ya uchunguz wa Madini bila kum-consult mmiliki wa ardhi.

Kule kisarawe, wanyeji wamepoteza Haki zao kisa TWYFORD wameshapewa PL ya Caolin eneo kubwa la Kisarawe. Matokeo yake wazawa wanaishia kuwa ombaomba Kwa Wachina ndani ya ardhi yao wenyewe badala ya kuwa wamiliki/partners. Hivi unaweza fanya udwanzi huu huko China??
 
Back
Top Bottom