KWELI Baadhi ya Mihogo huwa na sumu inayoweza kuua

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Kwa mujibu wa mdau mmoja, Disemba 12, 2019 aliona kwenye taarifa ya habari ya chombo kimoja wakitangaza kuwa familia moja imepoteza watoto wao wanne kwa kile kinachodaiwa kuwa walikula mihogo yenye sumu.

Cassava.jpg

Aidha, mada hii imekuwa inazungumzwa sana mitaani, huku ikiacha mashaka makubwa kwa kuwa mihogo ni chakula kinachotumika kwa kiasi kikubwa, kama kingekuwa na sumu basi watu wengi wangekuwa wamepoteza maisha.

Tuelewe nini kuhusu madai haya? Ni kweli kuwa mihogo huwa na sumu, au ni uzushi tu unaopaswa kupuuzwa?
 
Tunachokijua
Mhogo ni mzizi wenye nishati nyingi ambao kwenye mgawanyiko wa makundi ya viumbe hai na mimea huwekwa kwenye familia ya Euphorbiaceae. Kitaalam huitwa Manihot esculenta.

Vyanzo vya kihistoria vinataja asili ya mhogo kuwa ni bara la America ya kusini, kwa sasa mmea huu hupatikana kwenye zaidi ya nchi 80 duniani.

Kwa mujibu wa USDA, mhogo huwa na wanga, protini, vitamini C, aina mbalimbali za madini muhimu kwa afya, viondoa sumu na folate hivyo ni chakula chenye manufaa makubwa kwa afya ya binadamu.

Kuhusu sumu
Mihogo michanga (ambayo haijakomaa vizuri), michungu pamoja na ile isiyopikwa (mibichi) huwa na kemikali sumu za Cyanide.

Wingi wa kemikali hizi hutegemea na aina husika ya mhogo pamoja na sehemu ilipolimwa, hivyo kwa kiasi kikubwa aina nyingi ya mihogo tunayotumia kila siku huwa na kiwango kidogo sana cha kemikali hizi kisichoweza kuleta madhara kwa afya ya mlaji.

Katika mazingira machache, baadhi ya mihogo inaweza kuwa na kiwango kikubwa cha kemikali hii kinachoweza kuleta madhara kwa afya. Ulaji wa sumu hii huambatana na dalili zifuatazo-
  • Uchovu mkubwa na kuweweseka
  • Kiungulia
  • Maumivu makali ya kichwa
  • Maumivu ya kifua na kushindwa kupumua
  • Kifafa na kupoteza fahamu
  • Shinikizo la chini la damu
  • Shambulio la moyo na kifo
JamiiForums imebaini kuwa ulaji wa mihogo yenye kiwango kikubwa cha kemikali hizi unaweza kusababisha kifo.

Ukubwa wa dalili na athari za sumu hii hutegemea wingi wa dozi iliyotumika, aina ya cyanide iliyohusika kwa wakati huo pamoja na kiasi cha muda aliotumia mhusika kwenye kuikusanya sumu hii mwilini mwake.

Ushauri
Ni muhimu kuweka mkazo kuwa siyo kila mhogo huwa na sumu hii, pia ile ambayo huwa nayo huwa ipo kwenye kiwango himilivu kwa mwili.

Hata hivyo, hii haitoi tafsiri kuwa hakuna kabisa mihogo yenye kiwango kikubwa cha cyanide kinachoweza kuua, au kuleta madhara mengine makubwa kwa afya.

Hivyo basi kwa kuzingatia hali hizi zote tatu, ni muhimu kufanya mambo yafuatayo-
  1. Epuka ulaji wa mihogo mibichi hasa ile yenye ladha ya uchungu
  2. Loweka mihogo kwenye maji kabla hujaipika
  3. Kabla ya kutengeneza unga wake inapaswa kumenywa, kulowekwa na kukaushwa vizuri
Kwa mujibu wa Center for Food Safety, tendo la kuipika, kuloweka kwenye maji au kukausha kwenye jua huharibu sumu hii na kuifanya isiwe na madhara yoyote kwa afya. Pia, mihogo yenye ladha chungu huwa na sumu nyingi zaidi inayoweza kuleta athari na madhara ya haraka kuliko ile isiyo na ladha hiyo.
Mimi ni mtaalamu wa Kilimo. Nifahamuvyo, kiwango cha Cynade kinabadilika kulingana na aina ya udongo na altitude ya eneo husika.

Kwenye high altitude Cyanide inakuwa nyingi na ndio maana hatushauri kupanda mihogo kwenye high altitude pia maeneo yenye "Volcanic Soil" kama baadhi ya Wilaya za Kilimanjaro si vyema kupanda mihogo kwani itakuwa na "high level of Cyanide "
 
mihogo ya kisamvu cha mpira kile kinachopenda kustawi makaburini ukila safari
 
Mimi ni mtaalamu wa Kilimo. Nifahamuvyo, kiwango cha Cynade kinabadilika kulingana na aina ya udongo na altitude ya eneo husika.

Kwenye high altitude Cyanide inakuwa nyingi na ndio maana hatushauri kupanda mihogo kwenye high altitude pia maeneo yenye "Volcanic Soil" kama baadhi ya Wilaya za Kilimanjaro si vyema kupanda mihogo kwani itakuwa na "high level of Cyanide "
Uko sahihi kabisa.

Expression ya hiyo gene inahitaji mazingira maalumu.

Hii ipo hata kwenye zao la mpunga, baadhi ya mbegu huwa na harufu (aroma) pale kwenye aina fulani ya udongo na hali ya hewa.
 
Mimi ni mtaalamu wa Kilimo. Nifahamuvyo, kiwango cha Cynade kinabadilika kulingana na aina ya udongo na altitude ya eneo husika.

Kwenye high altitude Cyanide inakuwa nyingi na ndio maana hatushauri kupanda mihogo kwenye high altitude pia maeneo yenye "Volcanic Soil" kama baadhi ya Wilaya za Kilimanjaro si vyema kupanda mihogo kwani itakuwa na "high level of Cyanide "
Ni kweli kihistoria kule kwetu Kilimanjaro kuna mwaka watu walikula hiyo mihogo na ilipelekea vifo vya watu wengi hivyo kufanya mihogo iwe ni zao linalopingwa kuliwa na kabila la wachaga(Food Taboo)
 
JF inatakiwa wawe wanatoa na Tuzo za mambugila na Vilaza humu waliosoma vyuo na kozi za mambugila humu. Mwaka jana na mwaka huu ungepewa wewe Popoma.
Umekumbuka lakini kumeza Kidonge chako cha Ugonjwa wa Akili ( Maniac Bipolar ) ulionao na unaokusumbua kwa muda mrefu?
 
Uko sahihi kabisa.

Expression ya hiyo gene inahitaji mazingira maalumu.

Hii ipo hata kwenye zao la mpunga, baadhi ya mbegu huwa na harufu (aroma) pale kwenye aina fulani ya udongo na hali ya hewa.
Pia kuna baadhi ya majani ya mpunga hutoa gesi ya methane ambayo sio rafiki kwa afya...
 
MADAI
Kwa mujibu wa mdau mmoja, Disemba 12, 2019 aliona kwenye taarifa ya habari wakitangaza kuwa familia moja imepoteza watoto wao wanne kwa kile kinachodaiwa kuwa walikula mihogo yenye sumu.


Aidha, mada hii imekuwa inazungumzwa sana mitaani, huku ikiacha mashaka makubwa kwa kuwa mihogo ni chakula kinachotumika kwa kiasi kikubwa, kama kingekuwa na sumu basi watu wengi wangekuwa wamepoteza maisha.

Tuelewe nini kuhusu madai haya? Ni kweli kuwa mihogo huwa na sumu, au ni uzushi tu unaopaswa kupuuzwa?
Wasukuma wanaitaga CHOGHO sina hakika kama nmeandika vizuri, niliona wakilima mihongo mwanzoni na mwisho mwa shamba ndo wanaipanda ili kuzuia mifugo kula, wanapaka majani yake asali mfugo akila hatoboi masaa au majani wanayafunga mifuko ya rambo (kwa zamani wakati haijapigwa marufuku) akila majani ngombe au mbuzi na ule mifuko kinachofata___................
 
Uku kwetu tunauita dide au tandika ukiufanya kua makopa hufi yani uoze mpaka sumu itoke ila ukila mbichi umeisha ila pia huu muogo unamaajabu yake kipindi Cha njaa kwelikweli hufi ata ule mbichi ila kipindi Cha mavuno usijalibu kuula utaenda upo kama mdudu ule unaoliwa mizizi kipindi Cha njaa
 
MADAI
Kwa mujibu wa mdau mmoja, Disemba 12, 2019 aliona kwenye taarifa ya habari wakitangaza kuwa familia moja imepoteza watoto wao wanne kwa kile kinachodaiwa kuwa walikula mihogo yenye sumu.


Aidha, mada hii imekuwa inazungumzwa sana mitaani, huku ikiacha mashaka makubwa kwa kuwa mihogo ni chakula kinachotumika kwa kiasi kikubwa, kama kingekuwa na sumu basi watu wengi wangekuwa wamepoteza maisha.

Tuelewe nini kuhusu madai haya? Ni kweli kuwa mihogo huwa na sumu, au ni uzushi tu unaopaswa kupuuzwa?
Asante Kwa ujumbe mzuri🙏🙏.
 
MADAI
Kwa mujibu wa mdau mmoja, Disemba 12, 2019 aliona kwenye taarifa ya habari wakitangaza kuwa familia moja imepoteza watoto wao wanne kwa kile kinachodaiwa kuwa walikula mihogo yenye sumu.


Aidha, mada hii imekuwa inazungumzwa sana mitaani, huku ikiacha mashaka makubwa kwa kuwa mihogo ni chakula kinachotumika kwa kiasi kikubwa, kama kingekuwa na sumu basi watu wengi wangekuwa wamepoteza maisha.

Tuelewe nini kuhusu madai haya? Ni kweli kuwa mihogo huwa na sumu, au ni uzushi tu unaopaswa kupuuzwa?
nimewah kusikia hii kitu moshi kuwa imeua,lakin kuna mtu mmoja alisema ukigundua kua umekula muhogo wa aina hiyo basi ukila sukari inaondoa hiyo sumu,je lina ukweli?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom