Baadhi ya mawaziri wakiongea hawatofautiani na viongozi wa vyuo vikuu kwa hoja za kitoto

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,273
21,387
Kuna mawaziri wengine sijui kama huwa wanajisikiliza wakiongea!

Nasema hivi kwasababu, ukisikiliza presentation ya baadhi ya mawaziri utagundua kabisa inchi yetu hii ni kichwa cha mwendawazimu kila mtu anajifunzia kunyoa na kutuacha na mabarango.

Waziri wa fedha kila nikimsikiliza naona hatoshi kabisa, nashindwa kumtofautisha waziri wa inchi na wale mawaziri wa vyuo vikuu!

Yaan tunaendeshaje inchi kwa majaribio kama vile hatuna wachumi na wataalam wa kuchakata mambo kabla halijawa jambo la kitaifa?

Viongozi mnapopitisha jambo la kitaifa tumieni watalaam wenu kisomi.

Acheni kuufanya uongozi wa inchi kama uongozi wa chuo kikuu!

Mawaziri idara kama Fedha, tamisemi, uchukuz na wengineo tumieni wataalam wenu wawapatieni ushauri mzuri kabla hamjademka!
 
Bora wewe unaweza kumsikiliza mimi toka kitambo akiwa anaongea nahamisha channel naumia mno kuona msomi hana uwezo wowote kama vichwa Tito Mboweni.
 
Back
Top Bottom