chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 19,685
- 22,694
Habari wana-MMU!!
Kutokana na tatizo la FISTULA kushika kasi hapa nchini mwetu kuna wadau mbalimbali wamejitokeza wakitambulika kama mabalozi wa FISTULA huku wakiwaamasisha wanawake mara waonapo dalili za tatizo hili waripoti katika vituo husika vilivyopendekezwa kwa ajili ya kutoa huduma ya tatizo hili,.
Tatizo linakuja hapa kwenye namna wanavyohamasisha wahanga wa tatizo hili,.
Kuna mwanamke anasikika akimsema mwanamke mwenzake aliyepatwa na tatizo hili eti ''amelowa kama kuku mwenye kideri''
Kwa kweli tunatambua kuwa lengo lenu ni zuri ambalo linapaswa kuungwa mkono na kila mtu mwenye kujali ila Jaribuni kubadilisha maudhui ya tangazo lenu lililobeba maudhui ya udhalilishaji dhidi ya wanawake!!
Kutokana na tatizo la FISTULA kushika kasi hapa nchini mwetu kuna wadau mbalimbali wamejitokeza wakitambulika kama mabalozi wa FISTULA huku wakiwaamasisha wanawake mara waonapo dalili za tatizo hili waripoti katika vituo husika vilivyopendekezwa kwa ajili ya kutoa huduma ya tatizo hili,.
Tatizo linakuja hapa kwenye namna wanavyohamasisha wahanga wa tatizo hili,.
Kuna mwanamke anasikika akimsema mwanamke mwenzake aliyepatwa na tatizo hili eti ''amelowa kama kuku mwenye kideri''
Kwa kweli tunatambua kuwa lengo lenu ni zuri ambalo linapaswa kuungwa mkono na kila mtu mwenye kujali ila Jaribuni kubadilisha maudhui ya tangazo lenu lililobeba maudhui ya udhalilishaji dhidi ya wanawake!!