Baadhi ya Lecturers wa Mzumbe wana degree Feki - VC wao naye FEKI

FairPlayer

JF-Expert Member
Feb 27, 2006
4,145
716
Jamani hii ni serious ukizingatia kuwa hawa jamaa wanatoa Phd wakati hawana hata hiyo Phd.

Naomba serikali ikimulike hiki chuo. huu ni mwendelezo wa topic ya Degree mills:

Nanukuu member wa board wa hapa alivyowataja:

FD,

Hapo Mzumbe Uni kwa "Dr" Kamala mbona hizo bogus Phds ndio HQ. Kuanzia VC na baadhi ya senior members of academic staff wamekula doctoraat kutoka Pacific Western University (PWU) kama wamesimama! If I'm not mistaken, baraza la ithibati halikitambui hiki chuo. How comes leo watu ambao wana digrii feki wanaruhusiwa kufundisha manpower ya taifa? I find this absolutely ridiculous! Katika kupitia prospectus ya mzumbe http://www.mzumbe.ac.tz/propectus.htm, walimu wenye digrii from PWU na commonwealth open university ni hawa wafuatao:

Associate Professors
1. Moses M.D. Warioba DPA (IDM), Dip. Publ. Sect. Mgt (Aston), MBIM- (London), M.Sc. Publ. Sec. Mgt (Birmingham), Ph.D. (Public Admin.) PWU, (USA) NB: Huyu ndio Vice Chancellor!

2. Leonard .J. Shio B.A (Ed) Hons. (UDSM.), M.A. (Econ. Dev.) (UDSM), Ph.D(Management) PWU, (USA)

3. M.N. Chao B.A (Ed.) Hons. (UDSM), M.A. (Dev. Studies) (UDSM), Ph. D. (PWU), USA

Senior Lecturers
1. Raphael J.M. Habi ADPA (IDM), M.Sc.(Pers. Mgt) (Aston) (UK), MIPM (U.K.), Dip. T. & D. (Manchester) (UK), Ph.D(Management) PWU, (USA)

2. Christopher M. Sotta DPA (IDM), PG.D.(Gen.Mgt.)(IDM), MPA (IDM), Ph.D (Public Admin) PWU, U.S.A.

3. Aristarch K. Kiwango B.A. (Soc. Econ Admin) Makerere, M.Sc. (Econ.) Wales, Ph.D. (Econ.) PWU, (USA) PGD. (Project Planning)ISS,The Hague, PGD. (Pop & Dev Plan) ISS, The Hague

4. Colman Riwa B.A. (Education) (UDSM), PGD (Tesol) London, M.A. (Public Policy and Admin.) ISS, The Hague, Ph.D. (Public Administration) PWU, USA. (On leave of absence)

Lecturers
1. Diodorus Kamala Adv. Dip (Econ. Planning), (IDM), M.Sc. (Organization Syts), Linconshire Humberside,(UK), M.Sc. (Agric Development and Rural Finance) Bradford, (UK), Ph.D Commonwealth Open University (On Leave of Absence)

2. Prosper H. Ngowi Adv. Dip (Econ. Planning) (IDM), Norwegian Language and Civilization (Telemark University College, Norway, MBA (Project Mgt) Agder University College, Norway Ph.D Econ. (Norwegian School), Econ and Business Administratin(Commonwealth Open University)

Waziri wa MSTHE lipigwa mkwara wakati anapokea ofisi lakini mpaka sasa mbona kimya? http://www.kikweteshein.com/tanzania...kiona---Msolla

Je tuwaamini wasomi wanaotokea Mzumbe "university"????!!!!!!

FD
 
Someni Topic ya degree za Commonwealth ili tuendelee hapa, nilitaka kuwa more specific, maana Mzumbe ni taifa letu.

FD
 
DrWHO,

Mambo ya udini hayana nafasi, be it mkristo au muislamu kama ni bomu basi ni bomu tu!
 
DrWho,

Tuangalie hili moja la ufeki wa shahada, tafadhali. Unajuwa tena ukileta maswali ya dini zao hapa tutapoteza lengo. Usisahau pia saa nyingine majina yanapotoa. Unakumbuka Tariq Azizi wa Iraq, na bondia Mike Tyson utasema yupi ni dini ipi kama usingejuwa? Pengine hao jamaa hawana hata dini. Watu wenye imani ya dini yeyote huwa wazito kufanya mambo maovu kama hayo.
 
Hailekei kama kuna mtu Tanzania anayeshughulikia hizi digrii feki. Wale wanaotoa ajira bila kuwa na uwezo wa kuhakiki CV za watu ndio wanatupa matatizo.

Wajinga ndio waliwao. Kwa sasa, kila mtu anasubiri mtu mwingine atatue hili tatizo la udanganyifu katika CV za watu. Ni tatizo kweli kweli maana safu za uongozi nazo zimejaa vihiyo.

Naamini chuo chenye wasomi wa kweli kwenye uongozi, kama UDSM, hakiajiri hawa vihiyo wa PhD za PWU. Au nimekosea?

Augustine Moshi
 
huyo DR, ASSAD MUSSA si mkweli anachuki binafsi na mzumbe kwani hapo UDSM kwenye kitengo chake yupo Baisi ambaye alikwenda marekani akarudi na phd feki na hadi sasa yupo pale. wapo wengi udsm
naleta data soon.
 
Nungwi,

Hakuna mwenye chuki na Mzumbe, watu wameazisha hiimada kwa mapenzi mema kwa TAIFA LETU na kulitakia mema, ukisoma vema makala ya Mussa Assad, utagundua hakuwaacha hata wengine watakaokuwa kwenye vyuo vingine iwe IFM, Mzumbe, Nyegezi, Tumaini, na hakusema UDSM wapo au hawapo,

Mzumbe imekuwa topic kubwa kwani, kuna ex-wake ambao ni mawaziri ambao u-DR. umekuja ghafla mno!!

Wewe kama unajua wapo UDSM na hata vyuo vingine, wamwage hapa.
 
Nungwi,

Naona kijana huna DATA kabisa, Baisi aliporudi kutoka marekani UDSM ilikataa U Dr wake!! nina vithibitisho!! Baisi akachukia. Walimwambia U Dr wake ni feki. Baisi yupo idara ya Finance, Assad yupo Accounting, Yes wote wapo Faculty of Commerce and Management.

Lete Data hapa na nakuomba KIJANA ACHA MAJUNGU.

Narudia tena kwa UHAKIKA, Baisi U Dr wake ULIKATALIWA UDSM.

FD
 
Firaduni
siwezi kulinganisha jina lako na hoja hii itakuwa nakutukana na humu tumekatazwa matusi.
mbona unanitaa Mtoto mwenye majungu? mbona Dr. Assad alipolileta hili suala kwa kuwakomalia Mzumbe hukusema majungu?
hata katika makala yake hakugusia kama UDSM case namna hiyo ilitokea na hao pumba bado wanao.
je nisingembana DR.Assad wenu mngeweza kuja kwa hamaki kiasi hiki kama unachoonesha wewe? unataka kutumbia UDSM ni clean? mimi nilichangia baada ya kuona AUGUSTINO Moshi alipodai suala hilo UDSM halipo.
sasa MZEE WANGU FIKIRADUNI naomba usije kukimbia hapa.
wakati nakuja na file ya Baisi naomba pia umtie maji mheshimiwa NGIRWA najua unamfahamu vyema kama umemjua baisi WHY NOT NGIRWA wote wewe na Assad mnaficha uchafu wao.
kweli muweze kuyaona ya Mzumbe ya hapo kwenu yasionekana?
All in all mzee wetu WARIOBA kafanya makubwa.
nakwenda kuanda misile subiribini wana forum.
 
Nungwi,

FD keshakueleza kuwa Baisi u-Dr wake ulikataliwa, tatizo liko huko Mzumbe na kwingineko ambako bado wamekumbatia hizo PhD FEKI.

Shusha hizo misiles Ndg Nungwi zote zote i.e. za UDSM, Mzumbe, IFM, Sokoine, hapa hakuna kubagua, ELIMU FEKI NI FEKI popote pale ulipo, iwe SIASA, KAZI SERIKALINI, MAFICHONI, CHUONI etc etc
 
Nungwi,

Ahahahaaa poa bro. Hamna shida. No pun intended. Kuhusu kukimbia hiyo sahau mzee. Tumesakama mzumbe sana kwasababu wapo wengi sana wenye Phd feki. hata kiongozi wenu naye ana Phd feki. UMEELEWA?.

Inawezekana hata Sua au Udsm wapo ila sio wengi kama Mzumbe. Imefikia hatua tunaanza kujiuliza credibility ya elimu ya Mzumbe. kama VC anaweza kuitambua elimu feki ..inakuwaje kwa wanafunzi?.

Kuna kitu unahitaji kukifahamu. Unapojadili issue kwanza onyesha umeelewa aliyozungumza mjumbe/mwana board aliyetangulia. Baisi aliporudi aliambiwa afanye paper tena/a present tena kwa UDSM kutetea uhalali wa Phd yake. Akakataa, jamaa alipewa hela kwenda kusoma yeye akarudi na Benzi na elimu feki kama ya VC warioba wa Mzumbe.

Ngirwa aliwahi kuwa head wa dept ya General Mgt. Ngoja niangalie degree yake.

Fikiraduni sio lazima ziwe zangu, zinaweza zikawa za wengine:)
Peace bro.

FD
 
UDSM sio rahisi hata kidogo wadanganyike na digrii ya mtu. Wakubwa wa pale ni wasomi waliobobea mno. Nawaelewa vizuri, kwani nimeshafundisha sana pale.

Ukija na ka PhD UDSM, huwa wakubwa wa pale wanawasiliana moja kwa moja na chuo ulichotoka. Hawaangalii tu vyeti vyako. Na kama umepata cheti mahali pasipoeleweka kama PWU, wala hawatakutazami.

I know for a fact that UDSM has a strict vetting system. I was vetted in the same way when I returned there, in 1987, with a PhD in Mathematics. They verified everything with my university, Carleton (Canada) before accepting my PhD.

Hakuna vihiyo UDSM. Wakijitokeza wanafukuzwa kazi, hawaachwi pale. Vyuo vipya vinavyoanzishwa viige mfumo wa UDSM

Augustine Moshi
 
Nungwi: Nimesubiri data zako kuhusu UDSM kwa hamu sijaziona. Ukweli ni kwamba UDSM ina mapungufu yake mengi, lakini sio katika hili la digrii fake. Pale Mzumbe hata walimu wanajuana. Ukisema wana PhD wanauliza ni original au PU-yaani PU ni PhD yeyote iliyopatikana katika vyuo vya aina ya PWU-halafu wanacheka sana. Nimemuonesha jamaa wa mzumbe hii sample ya mzumbe Prospectus, alishtuka sana kwamba kumbe watu wameshtukia.

Tulikosea namna tulivyoanzisha Mzumbe. Chuo hiki kilipaswa kiwe-affiliated to one credible university kwanza kabla ya kuwa full fledged University. Nakumbuka pale UCLAS kabla hakijawa chini ya UDSM kulikuwa na watu waliojiita maprofesa na madokta lundo. Kilipoingizwa UDSM wakabaki watu wawili tu waliotambuliwa kuwa wana PhD halali. There is a serious vetting system at UDSM; there is no way you can cross with your fake PhD. You will be nabbed and shamed.
 
Habari za leo wanaforum!
kama nilivyoahidi kuchimba zaidi kuhusu uchafu wa UDSM ambapo wametokea mawakili ya bure kutetea hoja ya Dr.Assad iliyojaa ubaguzi wakati hapo alipo tena kitengo kimoja yuko na bogus anamuhifadhi.
Narudi kwenye mada yetu ya Baisi.

-Kaingia UDSM 1979 na kumaliza B.Com Finance 1982.
-Akaajiriwa kama Tutorial Assistant faculty ya commerce 1982.
-kafanya masters ANTERWEP-Belgium.
-Kaenda marekani kufanya PhD 1992 LAKINI alipofika USA masters yake hawakuitambua akalazimishwa kufanya nyingine MBA-1992-1994
-Feb 1994 kamaliza MBA na kuanza phd na september 1994 baada ya miezi saba kamaliza PHd.
mwishoni 1994 karudi tz kufundisha Udsm wakamjia juu na kufukuzwa kazi kwa phd feki.
-Wahaya hawakukubali wakaja juu kumsaidia Baisi(home boy) vita ikawa baina ya wahaya na wachagga. kumbuka wakati huo Dean wa faculty ni mchagga Dr.Mboya lakini Head wa FINANCE department(idara ya Baisi) ni mhaya dr, Kaijage.
-Hapo kesi ikaenda senate na prof.ISHUMI(MHAYA) akasimama kidete kumtetea baisi hadi akarudishwa kazini kwa madai eti baisi kadanganywa na chuo na si Baisi aliyeidanganya UDSM kwa kuleta phD feki.
lakini kabla ya hapo wakati kesi inaendelea DR.Kaijage(MHAYA) akaamua kumuajiri BAISI kama part-time lecturer
sasa huyo mtu kafukuzwa kazi kwa kukidanganya chuo(kuja na phd feki huku akijua ni feki) vipi tena anaajiriwa kama part-time lecturer? na huo umakini wa UDSM ambao Moshi, FIKIRADUNI,Dr.Assad mnatulazimisha tuamini kuwa upo UDSM mbona baisi bado anatesa? na nimekupa in details hadi masters yake ya Belgium ilivyokataliwa huko marekani.
Warioba makini sana ameweza kukitoa chuo toka kwenye Institute hadi university je Baisi kafanya nini?
huo ni wivu wa kijinga akina Fikiraduni, AUGOSTINO MOSHI NA DR, wenu Assad mussa mnachuki na mzumbe. hilo ni donge tu na mmetoka mbali na chuki hizi tena sasa hivi Mzumbe ngangari kinoma tuna BAF bachelor of Accounting and Finance jee huko UDSM na BAisi wenu na akina NGIrwa wamefanya nini?
Pandeni juu mkazibe na mtakufa nanyo kijicha cha roho Mzumbe ishakuwa University na tumegundua kuna watu kama akina moshi walikuwa wanaweka usiku ili mzumbe isiwe university mlitaka kuendeleza ukiritimba wenu.watu hawatizami certificate ulizobandika juu ya ukuta wanatiza ufanisi wa kazi nzito kama za Dr. Warioba(kiona mbali) kwa leo. naleta data zaidi za VIBAISI wengine wa UDSM
 
Mwanasiasa
jibu hilo hapo juu nazidi kuchimba VIBAISI wengine hapo UDSM.TIZAMA PRODUCT YA MZUMBE waliomaliza PUBLIC ADMIN. walivyokuwa makini. na wamejaa katika wizara mbalimbali kutokana na umahiri wao. na si uhaya kama ulivyofanya kazi kwa baisi na vibaisi wengine.huwezi kumfananisha mtu aliyemaliza Mzumbe na UDSM kwani graduate wa mzumbe wana soko kubwa kuliko waliomaliza UDSM. fanyeni utafiki, msipoteze muda kuhoji prospectus za Mzumbe University huo ni uvivu wa kufikiri.
 
kumbe ndio maana hatuendeleiii, kwa kuwa watu walioko serikalini wengi wametoka Mzumbe, kumbe ndio maana, vijana smart wanaomaliza UDSM hawapati ajira serikalini kwa sababu ni tishio kwa zile Diploma za Mzumbe, kumbe ndio maana.................

Nungwi,
hebu kumbuka zile score zako za form six kama ungeweza hata kujaribu kuingia UDSM wakati wako.
Hakuna aliyekataa kuwa Baisi alipata degree feki, Angalia action iliyochukuliwa na utawala wa UDSM, je Mzumbe wamechukua hatua gani kudhibiti jambo kama hilo? Nungwi soma hoja za watu na uzielewe kisawasawa

Wazee wa UDSM
Binafsi sijapitia UDSM, lakini historia ya watu waliokuwa wakiingia pale naijua, na kutokana na uandishi wa Nungwi, nawaomba msipoteze muda na yeye.

JKN (RIP) alisema
...........ni vema ukijua kuwa hujui na ukakubali kuwa hujui, kuliko kujiona unajua kumbe hujui.......hii ni HATARI!!!
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom