Baadhi ya desturi za kitanzania tunazopaswa kubadili au kuachana nazo!

Cesar Saint

JF-Expert Member
Nov 18, 2016
424
725
Habari Great Thinkers ....

Katika jamii zetu za kiafrika kumekuwa na mambo(desturi) kadha wa kadha ambazo kwa namna moja au nyingine zimekuwa zikitudumaza ama kutuchelewesha kwenye maendeleo katika nyanja ya kifamilia na jamii kwa ujumla .

Leo ningependa kuongelea desturi moja ambayo hurudisha nyuma jitihada za kimaendeleo ya kifamilia hasa upande wa uchumi.

Tuanze na maana ya maneno haya;

* Jamii ni istilahi inayoelezea uwepo wa pamoja wa mwanadamu hivyo basi katika kukua na kuendelea kwa mwanadamu kuna matendo au mitazamo ambayo inampasa kubadilisha au kuachana nayo kutokana na kujifunza zaidi ama kupata taarifa zaidi ya jambo husika.

* Desturi (kutoka Kiarabu) ni jambo la kawaida linalotendwa na jamii fulani mara kwa mara. Neno hilo ni sawa na mazoea, ada au kaida.

Katika mambo(desturi) haya mengi tunayopaswa kuondokana nayo miongoni ni UTARATIBU WA KUGAWA MALI ZA MAREHEMU (MIRATHI).

Kumekuwa na taratibu mbali mbali zinazoongoza swala hili kuanzia katika sheria za nchi,mila na hata kwa upande wa dini . Mwisho wa siku familia hufikia kwenye kugawiana sehemu ndogo ya mali au mirathi katika yale yalioachwa na marehemu .

Wengi wao huonelea njia hii kama mbadala wa kuepusha magomvi katika familia na kutenda hali kwa kila mwenye stahiki na mirathi husika.

Lakini Swali la kujiuliza Je, Tendo hili au desturi Hii ni jambo lenye tija kwa ustawi wa familia husika? Je, Kugawana mali kunachagiza ukuaji wa uchumi wa familia husika?

Kwa mtazamo wangu nafikiri ni ngumu sana au inahitaji mapambano makali kufikia kilele cha mafanikio katika nyaja ya kiuchumi (Utajiri).

Lakini ni njia rahisi endapo familia au ukoo utapitia mchakato wa “Generational building of wealth “ ambapo kila generation itakuwa na jukumu inalotekeleza katika kujenga uchumi wa familia au ukoo.

Kwa mfano ni rahisi sana kwa mjukuu kujenga kama babu alinunua na kuwekeza katika Ardhi au kwa namna nyingine ni rahisi sana kwa mtoto kuanzisha kiwanda na kampuni ya kuchakata mazao ya kilimo kama baba aliwekeza katika kilimo cha biashara.

Katika hatua hizi zote utaona ukuaji wa uchumi kutoka generation moja kwenda nyingine . Hapa ndio inakuja tofauti ya “Being Rich and Being Wealthy” familia iliojenga uchumi wake ni ngumu kuyumba kiuchumi hata pale kiongozi wa familia anapoanguka (Kufariki).

Sasa tukirudi kwenye ile desturi yetu ya kugawana mali za mwendazake inanyong’onyeza hatua za ukuaji wa uchumi wa familia husika na kuwarudisha nyuma zaidi au kupunguza matokeo chanya ambayo wangepata.

Nafikiri ni wakati sasa jamii zetu kuamka na kuanza kutengeneza kampuni ambazo wana familia watakuwa sehemu ya bodi za hizi kampuni na kusimamia biashara au miradi au vyazo vyovyote vile ambavyo mwendazake aliacha kuviendeleza badala ya kuvigawa (kuvitawanya) .

Hili litawaimarisha kiuchumi na kuleta tija zaidi. Umoja ni nguvu na utengano ni dhaifu na huu ndio umoja thabiti .Kila hatua za maamuzi zina changamoto zake lakini faida uliyopo kwenye uamuzi wa aina hii ni kubwa kuliko kugawana kidogo kidogo katika kile kingi.

Naomba kuwasilisha.
 
Hapa kidogo Kaka Mkubwa naomba kutia neno, kwa kuzingatia busara na upendo.

Inawezekana mchango wangu ukawa tofauti kidogo, lakini hii ni kwa sababu kila mtu ana utofauti wake na mimi ninao wangu pia.Na tofauti ya kila mtu inahitajika kuboresha mawazo yetu wote.

Kwanza kabisa nitangulize maneno yangu kwa kusema nawatakia wazazi/ wazee wote maisha marefu na ya afya nzuri, wafurahie walichochuma wao wenyewe. Ikiwezekana vijana wao tujikite zaidi kwenye kuwasaidia kuliko mawazo ya kufaidika na urithi wa mali walizochuma wao.

Mimi nafikiri watu wengi wanapenda maisha ya urahisi zaidi na wao kupata kutoka mali za familia kuliko maisha ya kujenga uchumi na kuchangia maendeleo ya mali za familia.

Na pengine nisilaumu watu sana bila kusema kwamba uchumi wetu nao, kama nchi Tanzania, kwa watu walio wengi, umewanyanyapaa, ni mdogo na umekaa kubanana banana watu hawana fursa nyingi. Hivyo matokeo yake wengi wanaishia kutumbulia macho mali za familia ziwafae wao, badala ya kuchangia kuongeza ustawi wa mali za familia.

Kingine tunazaana sana, baba mmoja ana watoto wengi, hawaelewani, pengine wamezaliwa kwa mama tofauti, familia ina mparaganyiko, hapo habari ya mirathi inakuwa na tabu.

Katika kipindi cha takriban miaka 20 iliyopita, idadi ya watu Tanzania imeongezeka kutoka takribani milioni 30 mpaka sasa takribani milioni 60. Tume double population katika miaka 20 tu!

Tukiendelea na kasi hii, mwaka 2040 tutafikia idadi ya watu milioni 120.

Tatizo linaanzia hapo.

Kwa familia zenye watu wanaopenda kujenga uchumi, na wenye fursa, tatizo linakuwa nani atarithi mali, kila mtu yuko busy na maisha yake kuendeleza mali na biashara zake, si kugombania mali za familia.

Mfano, mimi nilitaka kukataa kurithi mali za nyumbani kwa sababu za kifalsafa zaidi. Kwanza, nilishahama Tanzania miaka zaidi ya ishirini, kwa nia ya kuhama kimoja, si kuishi nje na kurudi tena. Wazo langu lilikuwa si kurithi nyumba za familia (nitaongelea sana nyumba kwa sababu ni kitu basic kwenye mirathi nyingi), bali, kama familia ina nyumba Tanzania, mimi nitaongeza nyumba za familia Marekani, ili kusudi vijana wadogo wanaozaliwa wakifika umri wa kuanza vyuo Marekani, au wakihitaji kuja Marekani kutembea, wawe na sehemu za kufikia nyumba ya familia Marekani, wasihitaji kuanza maisha kwa ugumu au kutegemea hoteli/ watu baki. Ndugu na marafiki wakiwa na safari za kuja Marekani waweze kusema wana sehemu ya kufikia. Ukienda kuomba viza ya Marekani una sehemu ya kueleweka ya kufikia ni tofauti na mtu asiye na sehemu ya kueleweka ya kufikia. Na kwa kweli nimefanya hivyo tayari, nimetimiza hilo. Nimeongeza nyumba za familia Marekani. Ndugu na marafiki wamepata kufikia kwangu na kufurahia kutohitaji kufikia hotelini.

Nikaona kwamba, katika urithi, kiutamaduni, kukataa kabisa urithi ni kama tusi kwa familia. Kwa hiyo nisikatae kabisa. Ila, niombe nitolewe kurithi kitu kikubwa kama nyumba, mashamba etc (our family has a considerable real estate portfolio), nipewe kitu sentimental, kama intellectual property kama michoro, vitabu, Biblia ya familia etc. Hizo mali niwachie wadogo zangu, hususan wale wachache waliobaki Tanzania, warithi.

Warumi wa kale walikuwa na msingi mmoja katika sheria zao za urithi, urithi ulikuwa ni kwa watoto waliokuwa physically karibu na ilipo familia tu, waliosafiri mbali hawakupata urithi. Na mimi kama mtoto niliyeamua kuanza maisha yangu Marekani nakubaliana sana na hii falsafa na pia nina falsafa ya kutaka kila kizazi kijikite zaidi kwenye kujitafutia kuliko kurithi.

Lakini, kama mtoto wa kwanza katika familia, nikatatizwa sana na wazo kwamba, urithi unaweza kuwa na maana ya kusimamia kilichoachwa kiendelee vizuri kwa manufaa ya familia, si kwa manufaa yako. Mathalani, nyumba zinaweza kuachwa kaka mkubwa ukakataa usipewe urithi, halafu zikaharibika kwa kukosa mtu wa kuzisimamia. Hili ni jambo la muhimu kwa kuwa muelekeo unaweza kuanza kuonekana hata kabla wazazi hawajatuacha.

Aaaah, wazazi kutuacha.Hili ni wazo ambalo nafikiri ni moja ya sababu zangu kutotaka kufikiria urithi. Nakuwa naona kama kufikiria urithi ni kufikiria kuwaharakisha wazazi kutuacha. Ni bora nisijipe fikra za urithi, kwa kuwa ni kama zinaleta fikra za msiba mkubwa.Ukiwa mkubwa wa kuondokewa na wazazi. Lakini kiuhalisia, haya mambo ni muhimu kupanga tangu awali.

Hapo nimetatizwa sana na suala hili la kukataa urithi, kwa sababu binafsi sina nia ya kurithi mali, naamini katika kila kizazi kutafuta mali yake, lakini suala la kuendeleza vilivyoachwa ni muhimu. Na hili kulitekeleza bila ya some sort of ownership ni vigumu.

Suluhisho nililoliona ni kuanzisha kampuni ya kuendesha miradi ya familia halafu washikadau wote kuwa wanahisa na wakurugenzi katika kampuni.

Mali za familia zitaendelea vizuri kibiashara zaidi kama kuna usimamizi mzuri, na watu wasiotaka kurithi mali wataweza kuchangia ustawi wa mali za familia bila kurithi mali.

Kwa mpango huo, mali za familia zinaweza kuendelea kustawi kizazi hata kizazi.
 
Hapa kidogo Kaka Mkubwa naomba kutia neno, kwa kuzingatia busara na upendo.

Inawezekana mchango wangu ukawa tofauti kidogo, lakini hii ni kwa sababu kila mtu ana utofauti wake na mimi ninao wangu pia.Na tofauti ya kila mtu inahitajika kuboresha mawazo yetu wote.

Kwanza kabisa nitangulize maneno yangu kwa kusema nawatakia wazazi/ wazee wote maisha marefu na ya afya nzuri, wafurahie walichochuma wao wenyewe. Ikiwezekana vijana wao tujikite zaidi kwenye kuwasaidia kuliko mawazo ya kufaidika na urithi wa mali walizochuma wao.

Mimi nafikiri watu wengi wanapenda maisha ya urahisi zaidi na wao kupata kutoka mali za familia kuliko maisha ya kujenga uchumi na kuchangia maendeleo ya mali za familia.

Na pengine nisilaumu watu sana bila kusema kwamba uchumi wetu nao, kama nchi Tanzania, kwa watu walio wengi, umewanyanyapaa, ni mdogo na umekaa kubanana banana watu hawana fursa nyingi. Hivyo matokeo yake wengi wanaishia kutumbulia macho mali za familia ziwafae wao, badala ya kuchangia kuongeza ustawi wa mali za familia.

Kingine tunazaana sana, baba mmoja ana watoto wengi, hawaelewani, pengine wamezaliwa kwa mama tofauti, familia ina mparaganyiko, hapo habari ya mirathi inakuwa na tabu.

Katika kipindi cha takriban miaka 20 iliyopita, idadi ya watu Tanzania imeongezeka kutoka takribani milioni 30 mpaka sasa takribani milioni 60. Tume double population katika miaka 20 tu!

Tukiendelea na kasi hii, mwaka 2040 tutafikia idadi ya watu milioni 120.

Tatizo linaanzia hapo.

Kwa familia zenye watu wanaopenda kujenga uchumi, na wenye fursa, tatizo linakuwa nani atarithi mali, kila mtu yuko busy na maisha yake kuendeleza mali na biashara zake, si kugombania mali za familia.

Mfano, mimi nilitaka kukataa kurithi mali za nyumbani kwa sababu za kifalsafa zaidi. Kwanza, nilishahama Tanzania miaka zaidi ya ishirini, kwa nia ya kuhama kimoja, si kuishi nje na kurudi tena. Wazo langu lilikuwa si kurithi nyumba za familia (nitaongelea sana nyumba kwa sababu ni kitu basic kwenye mirathi nyingi), bali, kama familia ina nyumba Tanzania, mimi nitaongeza nyumba za familia Marekani, ili kusudi vijana wadogo wanaozaliwa wakifika umri wa kuanza vyuo Marekani, au wakihitaji kuja Marekani kutembea, wawe na sehemu za kufikia nyumba ya familia Marekani, wasihitaji kuanza maisha kwa ugumu au kutegemea hoteli/ watu baki. Ndugu na marafiki wakiwa na safari za kuja Marekani waweze kusema wana sehemu ya kufikia. Ukienda kuomba viza ya Marekani una sehemu ya kueleweka ya kufikia ni tofauti na mtu asiye na sehemu ya kueleweka ya kufikia. Na kwa kweli nimefanya hivyo tayari, nimetimiza hilo. Nimeongeza nyumba za familia Marekani. Ndugu na marafiki wamepata kufikia kwangu na kufurahia kutohitaji kufikia hotelini.

Nikaona kwamba, katika urithi, kiutamaduni, kukataa kabisa urithi ni kama tusi kwa familia. Kwa hiyo nisikatae kabisa. Ila, niombe nitolewe kurithi kitu kikubwa kama nyumba, mashamba etc (our family has a considerable real estate portfolio), nipewe kitu sentimental, kama intellectual property kama michoro, vitabu, Biblia ya familia etc. Hizo mali niwachie wadogo zangu, hususan wale wachache waliobaki Tanzania, warithi.

Warumi wa kale walikuwa na msingi mmoja katika sheria zao za urithi, urithi ulikuwa ni kwa watoto waliokuwa physically karibu na ilipo familia tu, waliosafiri mbali hawakupata urithi. Na mimi kama mtoto niliyeamua kuanza maisha yangu Marekani nakubaliana sana na hii falsafa na pia nina falsafa ya kutaka kila kizazi kijikite zaidi kwenye kujitafutia kuliko kurithi.

Lakini, kama mtoto wa kwanza katika familia, nikatatizwa sana na wazo kwamba, urithi unaweza kuwa na maana ya kusimamia kilichoachwa kiendelee vizuri kwa manufaa ya familia, si kwa manufaa yako. Mathalani, nyumba zinaweza kuachwa kaka mkubwa ukakataa usipewe urithi, halafu zikaharibika kwa kukosa mtu wa kuzisimamia. Hili ni jambo la muhimu kwa kuwa muelekeo unaweza kuanza kuonekana hata kabla wazazi hawajatuacha.

Aaaah, wazazi kutuacha.Hili ni wazo ambalo nafikiri ni moja ya sababu zangu kutotaka kufikiria urithi. Nakuwa naona kama kufikiria urithi ni kufikiria kuwaharakisha wazazi kutuacha. Ni bora nisijipe fikra za urithi, kwa kuwa ni kama zinaleta fikra za msiba mkubwa.Ukiwa mkubwa wa kuondokewa na wazazi. Lakini kiuhalisia, haya mambo ni muhimu kupanga tangu awali.

Hapo nimetatizwa sana na suala hili la kukataa urithi, kwa sababu binafsi sina nia ya kurithi mali, naamini katika kila kizazi kutafuta mali yake, lakini suala la kuendeleza vilivyoachwa ni muhimu. Na hili kulitekeleza bila ya some sort of ownership ni vigumu.

Suluhisho nililoliona ni kuanzisha kampuni ya kuendesha miradi ya familia halafu washikadau wote kuwa wanahisa na wakurugenzi katika kampuni.

Mali za familia zitaendelea vizuri kibiashara zaidi kama kuna usimamizi mzuri, na watu wasiotaka kurithi mali wataweza kuchangia ustawi wa mali za familia bila kurithi mali.

Kwa mpango huo, mali za familia zinaweza kuendelea kustawi kizazi hata kizazi.

Kila la Kheri na mipango hiyo ndugu na wazazi wawe na uhai mrefu .

Swala hili la miparaganyiko kwenye familia ndio changamoto haswa kwenye maswala ya kuendeleza mirathi lakini hii solution ya kampuni inabeba wote nafikiri yaani hata kama mzee anawatoto ishirini! Wote wanaweza kuwa member wa bodi na kujenga kampuni.

Ikumbukwe hapa swala si lazima kuwe na mahusiano ya kindugu (kupendana nk) bali yawezekana kukawa na uhusiano wa kibiashara na kukua zaidi kiuchumi.
 
Tanzania kuna culture ya upigaji na hii ni kikwazo kikubwa cha ushirikiano. Kwenye mali za ushirikiano kila mtu anawaza kupiga akiona ndiyo ujanja. Hata mtaani wanasema 'hata mi nikiwa na kitengo nitapiga tu.' watu wenye mentality hii ni ngumu kushirikiana hata wakiunda kampuni.

Sijui hasa tulikotoa huu utamaduni wa kipigaji ila labda ujamaa ulichangia, watu waliona kusimamia mali za ujamaa ni fursa ya upigaji na wale walio nje waliona kumiliki mali kwa ujamaa ni kutafuta kudhulumiwa na kufaidisha wengine. Paradoxically, ujamaa unawafanya watu wasipende/wasiweze kushirikiana.
 
Back
Top Bottom