Tetere Enjiwa
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 217
- 65
Wengi wetu tumeshuhudia kitimutimu cha uchaguzi huko Igunga kilichosababishwa na kujivua gamba kwa RA. WanaJF hebu tudadavue kuwa huu mkakati ulikuwa ni muafaka kweli katika kuleta taswira bora ya ccm kwa jamii. Uchaguzi huu umeiimarisha ccm au umeidhoofisha mbele ya macho ya waTZ. Naomba tutoe maoni yetu kuhusu uwezo wa wabunifu wa mkakati huu wa kujivua gamba. Je mkakati huu utakua endelevu au ndio umekufa kifo cha asili baada tu ya kuanza kutekelezwa?