Baada ya wachezaji wa timu tajiri nchini ya Simba SC kukabidhiwa pikipiki, hivi ndivyo mchezaji wa Yanga SC Fei Toto alivyopewa makavu yake

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,426
108,530
Yafuatayo ni Mawasiliano ‘ Kiduchu ‘ kwa njia ya Meseji ( SMS ) kati ya Mchezaji Mwandamizi wa Simba SC Hassan Dilinga ( HD ) na Kiungo wa Timu Masikini na inayoenda Kushuka daraja nchini kwa Msimu huu Yanga SC hasa baada ya Kusikia kuwa Rafiki yake huyo pamoja na Wenzake wa Simba SC leo wamekabidhiwa ‘ Zawadi ‘ zao za Pikipiki na ‘ Mwekezaji ‘ wao Mohammed Dewji.

Fei Toto ( 0717…..9 )

Oya HD Kaka ni Mimi hapa Fei Toto kwa leo natumia namba hii ili Watu wa Yanga SC wasijue na wasisikie hili Kilio change Kwako kwani kwa Njaa kali iliyoko hapa Kambini Mwanza hata Wananchi wa Somalia wana afadhali. Naomba unipe Pikipiki kwa Mkataba hali ni mbaya Kaka na nitakuwa naipigia Kazi mwenyewe.

Hassan Dilunga ( 0763…..1 )

Kwa jinsi ulivyo lege lege kama ‘ Urojo ‘ wa Kwenu Zanzibar si watakupora tu? Hebu acha Kunitafutia matatizo Dogo. Kwani kuna Mtu alikutum na Kukulazimisha uchezee hiyo Timu Njaa Njaa Dhiki FC? Siku zingine na nyie muwe mnaangalia na Timu za Kuzichezea ona sasa unavyotaabika. Nikupe Hela kidogo ununue Nyavu uvue Vyura pale Bwawani Jangwani?

Halafu kwa Dhiki hii ndiyo mnajipa Moyo na Kujidanganya kabisa kuwa mtamfungwa ' Mwarabu ' akina Pyramids Jumapili hii?
 
Back
Top Bottom