The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,951
- 12,535
Kwa kumteua Dkt. Philip Isdor Mpango kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni ishara muhimu ya kuonesha kuwa Madam President Samia Suluhu Hassani, atakuwa Rais wa namna gani.
Kumbukumbu zinaonesha kuwa Dkt. Philip I. Mpango ni mtu safi na mwadilifu.
Hana makando kando yanayoweza kuwa mjadala. Kama kuna makosa fulani fulani aliyatenda ktk kipindi chote cha uwaziri wa fedha, itakuwa ni kwa sababu ya nature ya uongozi wa boss wake aliyekuwa anafanya nae kazi yaani Mwendazake John Pombe Magufuli..
Binafsi sioni kama ni Rais atakayefuata nyayo za Mwendazake Hayati Pombe ambaye kila mtu anajua sifa zake, kuwa, alikuwa Rais asiyeambilika wala kushaurika , mwoneaji, katili na hakuona shida kumwaga damu ya wakosoaji wake.
Ni wazi kabisa kuwa, Rais Samia Suluhu Hassan hawezi kuchukuliana na viongozi wenye tabia na hulka za mwendazake.
Viongozi kama DC wa Hai Ole Sabaya; DC wa Arumeru Jerry Muro; aliyekuwa RC wa DSM Paul Makonda a.k.a Daudi Albert Bashite; RC wa Mbeya Chalamila, RC Iringa Ally Hapi na wengine kibao wanaofanana na hawa, hawana chao tena.
Wanaodhani kuwa hawa wanaweza kupata nafasi ya uongozi ktk utawala wake, wafikiri mara mbili mbili.
Hata hizi nafasi za uongozi wanazoshikilia kwa sasa, ni suala la muda tu kuwa wataziacha na kurudi walikotoka..
Tukumbuke kuwa, siku zote mpanda ngazi huwa ni lazima ashuke.
Kumbukumbu zinaonesha kuwa Dkt. Philip I. Mpango ni mtu safi na mwadilifu.
Hana makando kando yanayoweza kuwa mjadala. Kama kuna makosa fulani fulani aliyatenda ktk kipindi chote cha uwaziri wa fedha, itakuwa ni kwa sababu ya nature ya uongozi wa boss wake aliyekuwa anafanya nae kazi yaani Mwendazake John Pombe Magufuli..
Binafsi sioni kama ni Rais atakayefuata nyayo za Mwendazake Hayati Pombe ambaye kila mtu anajua sifa zake, kuwa, alikuwa Rais asiyeambilika wala kushaurika , mwoneaji, katili na hakuona shida kumwaga damu ya wakosoaji wake.
Ni wazi kabisa kuwa, Rais Samia Suluhu Hassan hawezi kuchukuliana na viongozi wenye tabia na hulka za mwendazake.
Viongozi kama DC wa Hai Ole Sabaya; DC wa Arumeru Jerry Muro; aliyekuwa RC wa DSM Paul Makonda a.k.a Daudi Albert Bashite; RC wa Mbeya Chalamila, RC Iringa Ally Hapi na wengine kibao wanaofanana na hawa, hawana chao tena.
Wanaodhani kuwa hawa wanaweza kupata nafasi ya uongozi ktk utawala wake, wafikiri mara mbili mbili.
Hata hizi nafasi za uongozi wanazoshikilia kwa sasa, ni suala la muda tu kuwa wataziacha na kurudi walikotoka..
Tukumbuke kuwa, siku zote mpanda ngazi huwa ni lazima ashuke.