Baada ya Uingereza, Tanzania sasa yaalikwa mkutano wa uwekezaji Norway

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
majaliwa-england_210_120.jpg


WAZIRI Mkuu wa Norway, Erna Solberg amemuomba Waziri Mkuu Kassim, Majaliwa ahakikishe Tanzania inatuma wawakilishi wa Serikali kwenye mkutano wa uwekezaji, unaopanga kujadili fursa za uwekezaji barani Afrika utakaofanyika jijini Oslo, Norway, Oktoba mwaka huu ambapo focus kubwa itakuwa Tanzania.

Waziri Mkuu wa Norway alisema mkutano huo umeandaliwa na taasisi binafsi ya Norway Africa Business Association (NABA) na kwamba anazo taarifa kuwa utalenga kujadili fursa za uwekezaji barani, lakini ‘focus’ ikiwa ni Tanzania.

“Ni vyema Tanzania ikatuma wawakilishi kwenye mkutano ili waje kuelezea fursa zilizoko nyumbani. Serikali ilete watu wa kuja kuelezea hali halisi ikoje nchini Tanzania,” alisema.

Alisema ili fursa za uwekezaji ziweze kutumika ipasavyo, ni vyema Tanzania ikawa na mfumo wa kimahakama unaotoa haki bila upendeleo (a fair judicial system), kwani utasaidia kujenga hali ya kujiamini kwa wafanyabiashara wanaokuja kuwekeza Tanzania.

“Mfumo huu utaleta hamasa kwa wawekezaji, kwani watajua kwamba mitaji yao iko salama na inalindwa kisheria, hivyo hawatakuwa na hofu,” alisema. “Hata hivyo, napenda kusisitiza kuwa makampuni yanayotoka nje na kuja kuwekeza Tanzania hayana budi kuheshimu sheria za nchi yenu pamoja na za huku wanakotoka,” alisisitiza.

Solberg ametoa kauli hiyo juzi alipokutana na Waziri Mkuu Majaliwa na kufanya naye mazungumzo ya ana kwa ana kwenye mkutano wa siku moja wa Wakuu wa Nchi ulioitishwa kujadili suala la kupambana na rushwa duniani.

Source: Habari Leo
 
Tanzania Yatakiwa Kushiriki Mkutano Wa Uwekezaji Norway.

WAZIRI MKUU wa Norway, Bibi Erna Solberg amemuomba Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ahakikishe Tanzania inatuma wawakilishi wa Serikali kwenye mkutano wa uwekezaji unaopanga kujadili fursa za uwekezaji barani Afrika utakaofanyika jijini Oslo, Norway, Oktoba mwaka huu.
Bibi Solberg ametoa kauli hiyo jana (Alhamisi, Mei 12, 2016) alipokutana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kufanya naye mazungumzo ya ana kwa ana kwenye mkutano wa siku moja wa Wakuu wa Nchi ulioitishwa kujadili suala la kupambana na rushwa duniani.
Akizungumzia kuhusu mkutano huo, Waziri Mkuu wa Norway alisema mkutano huo umeandaliwa na taasisi binafsi ya Norway Africa Business Association (NABA) na kwamba anazo taarifa kuwa utalenga kujadili fursa za uwekezaji barani lakini focus ikiwa ni Tanzania.
“Ni vema Tanzania ikatuma wawakilishi kwenye mkutano ili waje kuelezea fursa zilizoko nyumbani. Serikali ilete watu wa kuja kuelezea hali halisi ikoje nchini Tanzania,” alisema.
Alisema ili fursa za uwekeaji ziweze kutumika ipasavyo, ni vema Tanzania ikawa na mfumo wa kimahakama unatoa haki bila upendeleo (a fair judicial system) kwani utasaidia kujenga hali ya kujiamini kwa wafanyabiasha wanaokuja kuwekeza Tanzania.
“Mfumo huu utaleta hamasa kwa wawekezaji, kwani watajua kwamba mitaji yao iko salama na inalindwa kisheria, hivyo hawatakuwa na hofu,” alisema.
“Hata hivyo, napenda kusisitiza kuwa makampuni yanayotoka nje na kuja kuwekeza Tanzania hayana budi kuheshimu sheria za nchi yenu pamoja na za huku wanakotoka,” alisisitiza.
Akijibu hoja hiyo, Waziri Mkuu alisema usawa wa kisheria upo nchini kwa sababu Tanzania imesaini mikataba ya kimataifa ya MIGA na ICSID (International Centre for Settlement of Investment Disputes) ambayo inahusika na usuluhishi wa migogoro ya kibiashara.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Majaliwa alimweleza Bibi Solberg kuwa Tanzania inahitaji kujifunza kutoka Norway katika suala la uanzishwaji wa mfuko wa ili mapato yatokanayo na rasilmali za nchi yatunzwe kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Naye akaipongeza Serikali ya awamu kwa kuanzisha wazo la kutaka kuanzisha mfuko huo hata kabla ya kuanza kuuza rasilmali hizo. Pia alimtihibitishia Waziri Mkuu kuwa wao wako tayari kubadilishana uzoefu na Tanzania katika suala hilo.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
IJUMAA, MEI 13, 2016.
 
Utasikia rais yuko Burundi au somalia......naona Sera ya kutosafiri nje inamuelemea sasa.....wanaomualika wako tayari hata kumlipia nauli......ukiona kujifunza elimu juu ya uwekezaji ni gharama,jaribu ujinga,dunia ya sasa ni knowledge...maarifa,mtume aliagiza tuyafate mpaka China,sisi tumeweka zuio la kuyafata maarifa!!tunakiuka hata maandiko,najua akienda akarudi,hatakuwa na maswali kuhusu dunia ya biashara na uwekezaji,NA atakutana na watendaji wakuu wa makampuni wanaolipwa pesa mingi NA atajua kwa nini wanalipwa,atajua kwamba wafanyabiashara si mashetani,atawauliza wenzie kama huwa wanafukuzana majukwaani huku wakipigiwa vigelegele
 
Hiyo picha ingeondolewa, maana si mzuri kimaadili. hayo mapaja naona kama ile ya Chura. by the way kila la heri kwa awamu ya Tano maana ni dalili mzuri hizi.
 
Utasikia rais yuko Burundi au somalia......naona Sera ya kutosafiri nje inamuelemea sasa.....wanaomualika wako tayari hata kumlipia nauli......ukiona kujifunza elimu juu ya uwekezaji ni gharama,jaribu ujinga,dunia ya sasa ni knowledge...maarifa,mtume aliagiza tuyafate mpaka China,sisi tumeweka zuio la kuyafata maarifa!!tunakiuka hata maandiko,najua akienda akarudi,hatakuwa na maswali kuhusu dunia ya biashara na uwekezaji,NA atakutana na watendaji wakuu wa makampuni wanaolipwa pesa mingi NA atajua kwa nini wanalipwa,atajua kwamba wafanyabiashara si mashetani,atawauliza wenzie kama huwa wanafukuzana majukwaani huku wakipigiwa vigelegele
Mzee wa msoga anatamani kweli kupewa hiyo trip
juzi juzi tu ulikuwa unamsifia
 
Hiyo picha ingeondolewa, maana si mzuri kimaadili. hayo mapaja naona kama ile ya Chura. by the way kila la heri kwa awamu ya Tano maana ni dalili mzuri hizi.
Mhh, hadi huko! Watu mnaangalia kwa macho mapana sana!
 
kumbe hata Norway walituma waziri mkuu Uingereza! vp nao rais wao hajui kiingereza?
Norway ni Constitutional Monarchy.. Inaongozwa na Mfalme. Though waziri mkuu ndio kiongozi wa serikali na ana madaraka zaidi.
 
Utasikia rais yuko Burundi au somalia......naona Sera ya kutosafiri nje inamuelemea sasa.....wanaomualika wako tayari hata kumlipia nauli......ukiona kujifunza elimu juu ya uwekezaji ni gharama,jaribu ujinga,dunia ya sasa ni knowledge...maarifa,mtume aliagiza tuyafate mpaka China,sisi tumeweka zuio la kuyafata maarifa!!tunakiuka hata maandiko,najua akienda akarudi,hatakuwa na maswali kuhusu dunia ya biashara na uwekezaji,NA atakutana na watendaji wakuu wa makampuni wanaolipwa pesa mingi NA atajua kwa nini wanalipwa,atajua kwamba wafanyabiashara si mashetani,atawauliza wenzie kama huwa wanafukuzana majukwaani huku wakipigiwa vigelegele
Burundi na Somalia za Ludewa?
 
sijui mama mzungu kawachekesha nini Mawaziri wetu? wanacheeeeekaa! tujipange waende watu wazuri basi!!
 
Ukienda nje maneno usipo enda nje maneno ukiwa chadema akili yako inakuwa kama kamasi vile
 
Back
Top Bottom