Uliza_Bei
JF-Expert Member
- Feb 17, 2011
- 3,216
- 988
Kwa ufupi tumeiona kwa mwelekeo huu Zanzibar Maalim ameongoza lakini huenda akatangazwa Mwinyi (CCM itashangilia na ACT wazalendo na kambi ya upinzani watabaki wenye huzuni).
Upande wa Madiwani na Wabunge hali inaonyesha asilimia 98% watatoka CCM bila kujali walipita bila kupingwa, wameshinda au wametangazwa kibabe. Tamu itakuwa shamrashamra na bashasha za Chama tawala wakijimwambafai kwa ushindi bila kujali nani ameumizwa kufikia hapo. Chungu ni kuwa kambi ya upinzani itaendelea kulia, kuhuzunika na kulalamika ndani na nje ya nchi.
Chungu hii itamwagika na kuathiri hasi (negative effect) kwa serikali ya Zanzibar na ile ya Muungano ya Tanzania kwa miaka yote mitano ijayo 2020-2025 kiasi cha kuharibu mipango ya maendeleo kwa kiasi kikubwa nchini.
Tamu kwa sababu serikali itakuwa huru bila kuhojiwa na hata bunge litakuwa la kupitisha na kujibu "ndiyooooo" bila hoja mbadala.
Chungu kwasababu wananchi hawatakuwa na wawakilishi wa kuwasemea shida zao. Tamu kwa CCM miaka 5 na chungu kwa kambi ya wananchi na upinzani miaka 5. Huenda ikawa tiketi ya CCM kuondoka madarakani baada ya kuwa wananchi wamejilaumu kwa miaka 5 wakipitia machungu.
Ninatabiri kwa miaka 5 Watanzania wote tutakuwa wapinzani wa serikali maana kambi ya upinzani ya kisiasa itakuwa haipo. Tujiandae kwa hayo.
Upande wa Madiwani na Wabunge hali inaonyesha asilimia 98% watatoka CCM bila kujali walipita bila kupingwa, wameshinda au wametangazwa kibabe. Tamu itakuwa shamrashamra na bashasha za Chama tawala wakijimwambafai kwa ushindi bila kujali nani ameumizwa kufikia hapo. Chungu ni kuwa kambi ya upinzani itaendelea kulia, kuhuzunika na kulalamika ndani na nje ya nchi.
Chungu hii itamwagika na kuathiri hasi (negative effect) kwa serikali ya Zanzibar na ile ya Muungano ya Tanzania kwa miaka yote mitano ijayo 2020-2025 kiasi cha kuharibu mipango ya maendeleo kwa kiasi kikubwa nchini.
Tamu kwa sababu serikali itakuwa huru bila kuhojiwa na hata bunge litakuwa la kupitisha na kujibu "ndiyooooo" bila hoja mbadala.
Chungu kwasababu wananchi hawatakuwa na wawakilishi wa kuwasemea shida zao. Tamu kwa CCM miaka 5 na chungu kwa kambi ya wananchi na upinzani miaka 5. Huenda ikawa tiketi ya CCM kuondoka madarakani baada ya kuwa wananchi wamejilaumu kwa miaka 5 wakipitia machungu.
Ninatabiri kwa miaka 5 Watanzania wote tutakuwa wapinzani wa serikali maana kambi ya upinzani ya kisiasa itakuwa haipo. Tujiandae kwa hayo.