Baada ya uchaguzi: Chadema tunaanza na vipaumbele vifuatavyo

Mpangamji

JF-Expert Member
May 12, 2010
540
140
:israel:Kwanza, niwapongeze wananchi wa Tanzania kwa kutumia haki yenu ya msingi kuchagua viongozi wenu, yote yaliyojiri katika harakati hizi tunayafahamu. wanotakiwa kuyafanyia kazi basi tunaomba wayafanyie kazi.
kwa sisi wengine natoa wito tuanze kuainisha vipaumbele vya kwanza kabisa ambavyo tutapenda wabunge wetu waanze navyo. ni ukweli usiopingika kuwa wana JF tuna utaalamu tofauti tofauti na mawazo tofauti ambayo kwa pamoja yatawezesha kuwapatia mwanga wabunge wote wapenda maendeleo na wapenda nchi hii, ili waanze nayo pamoja na mawazo yao ili tuanze utekelezaji wa kujikwamua angalau kidogo kutoka katika mikono hii mirefu ya mafisadi. wenye taaluma za uendeshaji wa halmashauri, wekeni jamvini nini kinaweza kufanyika ili wananchi wafaidi rasilimali zao, vivyo hivyo wenye taaluma zingine kama uhandisi, siasa za jamii na nyingine nyingi. nawakaribisha tuchangie mawazo yetu, tumepigana na tumefika hapa tulipo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom