Baada ya teuzi, sasa Media za Tanzania zimeshawekwa 'Mfukoni' na Mamlaka

kuua bila watu kujua unaua inapendeza kuliko kuua mpaka mtoto mdogo anajua unaua, mama anatumia akili kuwaweka mfukoni kuliko kuwaweka mfukoni kwa kuwaua, kuwateka kuwablackmail na kusababisha diplomasia ife...
 
Naona poti Kheri kalushiwa ndoano...mama anajifanya anasukuma kete....JK bwana....
 
Amemaanisha nini hapo kwa ulivyomuelewa?.
Mnayemuona mbele ni Rais Samia Suluhu Hassan lakini kwa nyuma kuna kivuli cha Magufuli kipo bado kinaendesha mambo.

Mama anaonekana kaja kivingine, lakini nyuma kuna u Magufuli unaendelea.

Mimi nimesikitika habari za BOT kuagizwa kupunguza riba na rais. Ingawa riba inawezekana inatakiwa ipunguzwe, lakini inatakiwa ipunguzwe na BOT, bila kuingiliwa na wanasiasa, kwa sababu za kiuchumi.

This is such a Magufuli move.

Haya ndiyo mambo ya Idi Amin kuagiza benki kuchapisha fedha nyingi ili watu wapate fedha mtaani, matokeo yake Shilingi ya Uganda imeanguka na haija recover mpaka leo.
 
Kuanzia sasa Media za Tanzania zitakuwa zinaweka bidii katika 'Kujipendekeza' kwa Mamlaka ( Serikali ) na Kusifia ( Kupanba ) mno ili Waandishi wake 'waule' katika 'Teuzi' na wala siyo katika Kuibua Taarifa Muhimu na yenye Tija kwa Maslahi na Maendeleo ya nchi.

Maziko ya Media Tanzania yamefana.
Hizo fikra zako mkuu
 
Kuanzia sasa Media za Tanzania zitakuwa zinaweka bidii katika 'Kujipendekeza' kwa Mamlaka ( Serikali ) na Kusifia ( Kupanba ) mno ili Waandishi wake 'waule' katika 'Teuzi' na wala siyo katika Kuibua Taarifa Muhimu na yenye Tija kwa Maslahi na Maendeleo ya nchi.

Maziko ya Media Tanzania yamefana.
Kuna mwandishi kateuliwa?
Maana nyangasa, na mwaipaya ni watangazaji tu hata sjui kama wamesoma

Sent from my SM-G973U using JamiiForums mobile app
 
Naendelea kujiuliza hizi course za POLITICAL SCIENCE zinakazi gani kama tunaokoteza okoteza tu viongozi kwa kuangalia umaarufu wao!

Kwann wasibebe wasomi/malecture ama watumishi wa serikali kwa nafasi hizi Zaid ya kuwajaza WAUZA sura na wapiga picha na kushinda instagram muda wote!

Hivi jokate kweli ni wa kupelekwa Temeke!
Kweli Nicki wa pili ndo mkuu wa wilaya?

Vyeo hivi havina hadhi tena labda Sasa tuseme ni mabalazo wa kuitangaza serikali na si wakuu wa wilaya
Kwa Jokate yupo vizuri usimfananishe na hao Wengine mkuu
 
Kuna mwandishi kateuliwa?
Maana nyangasa, na mwaipaya ni watangazaji tu hata sjui kama wamesoma

Sent from my SM-G973U using JamiiForums mobile app
Hivi unaweza kuwa Aircraft Engineer halafu usiwe Flight Pilot? Kwahiyo Super Brands kama IPP na Azan wanaweza Kuajiri Watangazaji ila wasiwe wamefuzu Kozi za Uandishi wa Habari? Kuna Watu huwa mnanilazimisha niwajibuni Kunya ( Shombo ) kutokana na IQ's zenu Kiduchu.
 
Kwanza Katika Hili sidhani Kama Uko sahihi...Sio lazima kwamba Media house zote zitakua na kazi ya Kusifia...Cha Mhimu cha kujiuliza ni Je Media Hizi zina watu wabobevu kwenye Maeneo yapi na Yapi..Mwandishi aliebobea kwenye Idara za Elimu,Uchumi , siasa...Biashara na Mazingira kwa hapa Tanzania Ni nani??

JE ANA UZOEFU UPI?? UKIANGALIA WOTE TU Kazi ya Habari ni kama Leo Hutampata Tido Mhando na Maswali Magumu sana kwa Mtu anaemhoji...Na wala Kwa Miaka ijayo Mingi Hutampata Charles Hillary na Maswali magumu sana...Ndio Kusema Media Yenyewe inatakiwa kujiangalia...ACHILIA mbali kusema watakua wanasifu tu...Wana mapungufu mengi ya kujijenga...

Ni nani tunamjua anafanya habari za Uchunguzi??? Ni Gazeti Gani tunalitegemea akina Salva Rweyemamu na Rai ya kipindi kile wako wapi leo...

IKO WAPI Raia Mwema iliyoshiba nondo za akina Dilunga..Joseph Mihangwa na Jenerali Ulimwengu Twaha??

TUNA OMBWE kubwa sana eneo hilo la Habari....Ipo kazi ya kufanya na ndio kusema walioteuliwa ni sahihi na wao ni Watanzania na Mm naona wao sio shida shida ni Industry kujijenga na watu imara sana kusaidia kuongoza nchi....

MAMA ameteua hao tuwaunge mkono maana angeteua UVCCM tungelalama pia...tumuache aongoze.
 
Back
Top Bottom