Baada ya siku 100: Tunapoachana kwenye Mataa na Rais Samia

Kulalamika kila kukicha hakuongezi tija serikalini.

Mengi uliyoandika ni hisia tu, unao ushahidi kwamba wewe na mimi tusipolipa kodi bado serikali itashindwa kununua magari yanayotumiwa na viongozi wa serikali?.

Tatizo letu ni kujipatia haki mpaka kupitiliza, kwamba mimi na wewe tusipolipa kodi basi wale wabunge maisha yao hayataendelea kuwa kama yalivyo!. Naielewa concern yako kama mlipa kodi lakini maisha yanaendelea pasipo mimi na wewe kuwa sehemu ya walipa kodi.

Ufisadi upo tangu enzi za Yesu na Mohamed, sio jambo la kumalizika leo eti kwa mimi na wewe kuwa na uhuru wa kuhoji. Hasara za makampuni zipo dunia nzima, zipo kwenye mataifa yote.

Kodi hazikwepeki hata kama mimi na wewe tunaweza kuwa na mchango mdogo sana katika kuzilipa. Mataifa yote duniani hayawezi kujiendesha pasipo ukusanyaji wa kodi. Huo ndio ukweli na siku zote huwa unauma ukiutafakari kwa kina.
Si mbaya nikikumbusha tena kuwa hakuna ninapolalamika bali ninasema.

Kuna tofauti kubwa baina ya kulalamika na kusema.

Lipi la hisia baina ya haya?

IMG_20210716_182538_628.jpg


Kuhitaji "fair share" ya kodi haiwezi kuwa ni hisia au kulalamika. Kuhitaji accountability hakuwezi kuwa ni hisia au kulalamika.

Kwenye hili kitaumana na huo ndiyo ukweli wenyewe.

Ufisadi kuwepo tangu enzi za Yesu hakuwezi kuhalalisha wewe kuiba au awaye yote kuendelea kuiba na hasa kutuibia.

Makampuni kupata hasara hali kadhalika hakuwezi kuhalalishwa kuwa ni dhidi yetu wala si dhidi yenu wala mwingine awaye yote.

Hayupo anayekataa kodi za halali. Hatutaki kodi na tozo dhalimu. Ndiyo maana tozo ya miamala sitakaa nilipe.
 
Magufuli naye mlituambia alishachanjwa chanjo ya China ndio maana akawa haogopi corona hivyo alikuwa anatutoa kafara wananchi, ila alipofariki ni nyie tena mnatuambia kafa na corona.

Mama alikuwa anaoneka anajali ana upendo na anatumia njia za kisayansi kukabiliana na corona ila sasa anaoneka mbinafsi hajali tena wananchi et kachanja chanjo kisirisiri hivyo hajali tena wananchi wake kuhusu corona.
MATAGA na Sukuma Gang wanakomeshwa
 
Samia kaenda na ule msemo wa wema usizidi uwezo, mwanzo alifanya ili kurudisha imani kidogo kwake toka kwa wapinzani, na kweli wapinzani wakaingia kingi wakaanza kumsifia anaupiga mwingi.

Ila alipoona inatosha sasa ameamua kuanza kukaba tena, anajua akiwaachia moja kwa moja mtasababisha nguvu zake na chama chake zipotee na kuufufua upya upinzani.

Mkuu ninadhani Mama alikuwa na nia njema na angali nayo. Ninaamini hapa ni kukaza kamba tu. Tatizo letu kubwa ni hao wanyoa viduku:

IMG_20210704_051559_619.jpg


Humo kuna wahafidhina bila kuwasahau hawa hapa tameer Kitimoto Jumbe Brown na wenzao.

Ubinafsi wao uliopitiliza ndiyo unaowasumbua:


Ni wazi kuwa tunakokwenda kitaumana na wala si mbali.
 
Mkuu maadam moyo wako bado unapumua jifunze kukubaliana na hali halisi. Kodi ndio zimeshapitishwa na bunge kama sehemu ya bajeti ili kuzisitisha ni mpaka bunge lijalo likae.

Hakuna maendeleo yasiyo na gharama zake. Hao ambao wamekuwa wakijazilizia bajeti zetu kwa miaka mingi tangu tupate uhuru ni watu wanaofahamu maana ya kubana matumizi.

Huwezi kutaka uishi vizuri halafu wakati huo huo ukataka upate bure bure tu, lazima kuumia kukuhusu ili maisha yaboreshwe.

Moyo kupumua haina maana ya kuwa nikubaliane tu hata na nisivyokubaliana navyo.

Bajeti si msahafu. Mpaka bajeti nyingine hiyo watajua wao. Hiyo sasa sisi haituhusu.

Tunajua ipo lugha wanayoielewa. Tulipo mbona tutaelewana tu?
 
Moyo kupumua haina maana ya kuwa sikubaliani tu na nisivyokubaliana navyo.

Bajeti si msahafu. Mpaka bajeti nyingine hiyo watajua wao.

Tunajua ipo lugha wanayoielewa. Tulipo tutaelewana tu.
Kodi zitalipwa mpaka siku ambayo zitabadilishwa, haya mengine ni maongezi ya kufurahishana.
 
Mama Samia huko uliko pokea salamu hizi.

Katika siku 100 zako za mwanzo ulianza vizuri ukitupa matumaini mapya nasi tukakupongeza. Lakini baada ya hizo kupita ghafla umetubadilikia.

Ama kwa hakika unayoyafanya sasa si mageni hapa duniani na huu wimbo unakuhusu:




"Neema alimwambia Chidumule yule bwana aliyezaa naye kaja. Hivyo asifike nyumbani kwake wala kazini asimfuate. Hata akimwona njiani asimsalimie."

Tuna habari kuwa wenzetu serikalini kwa gharama zetu, nyie na jamaa zenu tayari mmeshapata chanjo tena ile adimu kabisa ya Pfizer kwa gharama zetu.

Kwa kuchanjwa kwenu sasa Corona ni suala la historia. Kwani hata mkiambukizwa, kwamba mtahitaji hata kufika hospitali tu, uwezekano huo ni mdogo sana. Corona haiwahusu tena na kimsingi sasa kwenu Corona haipo.

Bila shaka mliyezaa naye sasa yupo. Kama ilivyo kuwa kwa Neema hamtuhitaji tena. Kwa vitendo na hata kwa maneno mmeonyesha hivyo:

1. Mmetuongezea mzigo wa gharama za maisha kwa kuongeza kodi za mafuta ya magari.
2. Mmetuletea tozo mpya kwenye miamala ya simu:


3. Vigogo nyie kulipa kodi tu hakuwahusu.
4. Kuna wabunge 19 kinyume cha katiba mzigo wa malipo yao mmeuweka kwetu.
5. Wizi wa pesa tunazokamuliwa kama ripoti kadhaa za CAG zinavyoonyesha umeamua kuufumbia macho.
6. Mashirika yanayozalisha hasara mnazotuvisha sisi unaendelea kuyakumbatia.
7. Wenzetu mnaendelea kupeana takrima za magari na majumba ya mabilioni ya pesa kwa gharama zetu.
8. Waraka huu sasa unatuhusu sisi, bila shaka mnapopanga kutuokotezea chanjo kanjanja zisizowahusu nyie:


9. Ninyi mnapotumbua kwa gharama zetu:


10. Sisi ni mwendo wa kugumia:


Kwani uzalishaji unaongezeka au umeongezeka? Vipi basi hata mkaongeze kodi na tozo mpya mpya kama kuna janga linalotuhusu sote, achilia mbali kutokudhibiti matumizi ya vilivyopo?

Tumekuelewa mama yetu. Yule bwana yupo. Hata njiani tukikuona hatutakusalimia.
 
Wasisubiri msemo ule wa kizaramo ukafanya kazi,"mwana kulitafuta mwana kulipata"

Wanampango mkakati wa kulitafuta. Mbona wana watalipata.

Kwa mwendo huu kitaumana si muda mrefu.
 
Sasa kurudia njia mbaya tuliyokuwa tukiifuata na kutambua kuwa ilikuwa njia mbaya,je kwa hiyari tutairejea?

Kukaa na kudumu kwenye njia inayopaswa kwa hakuwezi kuwa hisani au utashi wa mtu binafsi.

Tunayo kazi takatifu mbele yetu ya kulifanyia taifa hili katika namna ambayo historia itatukumbuka.
 
Uzuri mmoja ni kuwa nchi hii ina msingi wa maelewano tofauti na baadhi ya mataifa ya afrika.

Mtanzania ni muelewa siku zote hata akilalamika siku au wiki nzima.

Naamini awamu ya sita haina nia mbaya.

Tate Mkuu palikuwa na uzi hapa:


Wanatuchukulia poa. Waache waendelee hivyo hivyo.
 
Mkuu maadam moyo wako bado unapumua jifunze kukubaliana na hali halisi. Kodi ndio zimeshapitishwa na bunge kama sehemu ya bajeti ili kuzisitisha ni mpaka bunge lijalo likae.

Hakuna maendeleo yasiyo na gharama zake. Hao ambao wamekuwa wakijazilizia bajeti zetu kwa miaka mingi tangu tupate uhuru ni watu wanaofahamu maana ya kubana matumizi.

Huwezi kutaka uishi vizuri halafu wakati huo huo ukataka upate bure bure tu, lazima kuumia kukuhusu ili maisha yaboreshwe.
Unayo yasema yana mantiki. Ni kweli kwamba ikiwa huwezi kutatua jambo, ishi nalo...wanasema "let go" na hivyo unajipunguzia chance ya kupata magonjwa...nk. Ati hakuna maendeleo yasiyo na gharama...nk. Maneno hayo ni mema yanapozungumzwa na mtu mwenye hekima na busara ambaye ni mwenye moyo safi anayependa kwa dhati kuwaona wanaoitwa wanyonge wanaishi kama binadamu wenye heshima na raha ya aina fulani pale wanapoishi.
Huenda ingependeza zaidi ikiwa yangesemwa bila chumvi wala ushabiki wowote ambao kuwepo kwake kunamfanya mtu huyo mnafiki. Anakuwa mnafiki ikiwa anajua anayoyasema ni uongo.
Yako maendeleo ya vitu na yako ya watu...nk na tofauti zinajulikana. Sasa, hizo gharama ni za vitu au watu? Unapopandisha kodi ili uongeze ndege au umjengee kiongozi hekalu wakati unampokonya mnyonge kuku au chochote kwa kushindwa kuchangia mabweni na huku mwanasiasa anaruhusiwa kutolipia baadhi ya anasa zake, utakuwa unazungumzia maendeleo ya yupi?
Unazijua shule zilizoko vijijini zikoje? Vituo vya afya vina hali gani? Barabara zikoje? Shule je?
Kwa sasa hivi, kwa kiasi kikubwa upinzani umedhibitiwa, nani atoe mawazo mbadala?
Huenda sasa umefika wakati waTz wakaweka ushabiki pembeni. Bei ya mafuta inapopandishwa kwa kiasi hicho, nani asiyeona kwamba itasababisha mfumuko wa bei ambao utawatesa waitwao wanyonge? Ati "wajifunze kukubaliana na hali halisi" - wakipata maumivu wasilie?!
Wanasema "if you live in a glass house, don't throw stones". Unapoishi katika nyumba ya vioo, usirushie watu mawe hovyo.
Wako wanaojengewa mahekalu bure, wanoingiza magari ya kifahari bila kodi, mamishahara yao makubwa...nk. Ikiwa wenye kuyapitisha hayo ni kwa ajili yao wenyewe wakilipiwa na wanyonge bila ridhaa yao, unapendekeza watu wakae kimya? Nafikiri, mojawapo ya sababu ya kupinga Katiba ya Warioba, sasa inajitokeza hadharani
Watu waachwe watoe ya moyoni kwa kuwa hawana mwingine wa kuwasemea.
Mungu awe nasi
 
Unayo yasema yana mantiki. Ni kweli kwamba ikiwa huwezi kutatua jambo, ishi nalo...wanasema "let go" na hivyo unajipunguzia chance ya kupata magonjwa...nk. Ati hakuna maendeleo yasiyo na gharama...nk. Maneno hayo ni mema yanapozungumzwa na mtu mwenye hekima na busara ambaye ni mwenye moyo safi anayependa kwa dhati kuwaona wanaoitwa wanyonge wanaishi kama binadamu wenye heshima na raha ya aina fulani pale wanapoishi.
Huenda ingependeza zaidi ikiwa yangesemwa bila chumvi wala ushabiki wowote ambao kuwepo kwake kunamfanya mtu huyo mnafiki. Anakuwa mnafiki ikiwa anajua anayoyasema ni uongo.
Yako maendeleo ya vitu na yako ya watu...nk na tofauti zinajulikana. Sasa, hizo gharama ni za vitu au watu? Unapopandisha kodi ili uongeze ndege au umjengee kiongozi hekalu wakati unampokonya mnyonge kuku au chochote kwa kushindwa kuchangia mabweni na huku mwanasiasa anaruhusiwa kutolipia baadhi ya anasa zake, utakuwa unazungumzia maendeleo ya yupi?
Unazijua shule zilizoko vijijini zikoje? Vituo vya afya vina hali gani? Barabara zikoje? Shule je?
Kwa sasa hivi, kwa kiasi kikubwa upinzani umedhibitiwa, nani atoe mawazo mbadala?
Huenda sasa umefika wakati waTz wakaweka ushabiki pembeni. Bei ya mafuta inapopandishwa kwa kiasi hicho, nani asiyeona kwamba itasababisha mfumuko wa bei ambao utawatesa waitwao wanyonge? Ati "wajifunze kukubaliana na hali halisi" - wakipata maumivu wasilie?!
Wanasema "if you live in a glass house, don't throw stones". Unapoishi katika nyumba ya vioo, usirushie watu mawe hovyo.
Wako wanaojengewa mahekalu bure, wanoingiza magari ya kifahari bila kodi, mamishahara yao makubwa...nk. Ikiwa wenye kuyapitisha hayo ni kwa ajili yao wenyewe wakilipiwa na wanyonge bila ridhaa yao, unapendekeza watu wakae kimya? Nafikiri, mojawapo ya sababu ya kupinga Katiba ya Warioba, sasa inajitokeza hadharani
Watu waachwe watoe ya moyoni kwa kuwa hawana mwingine wa kuwasemea.
Mungu awe nasi

Anasema serikali yake ni Sikivu lakini yasikia nusu nusu:

 
Mama Samia huko uliko pokea salamu hizi.

Katika siku 100 zako za mwanzo ulianza vizuri ukitupa matumaini mapya nasi tukakupongeza. Lakini baada ya hizo kupita ghafla umetubadilikia.

Ama kwa hakika unayoyafanya sasa si mageni hapa duniani na huu wimbo unakuhusu:




"Neema alimwambia Chidumule yule bwana aliyezaa naye kaja. Hivyo asifike nyumbani kwake wala kazini asimfuate. Hata akimwona njiani asimsalimie."

Tuna habari kuwa wenzetu serikalini kwa gharama zetu, nyie na jamaa zenu tayari mmeshapata chanjo tena ile adimu kabisa ya Pfizer kwa gharama zetu.

Kwa kuchanjwa kwenu sasa Corona ni suala la historia. Kwani hata mkiambukizwa, kwamba mtahitaji hata kufika hospitali tu, uwezekano huo ni mdogo sana. Corona haiwahusu tena na kimsingi sasa kwenu Corona haipo.

Bila shaka mliyezaa naye sasa yupo. Kama ilivyo kuwa kwa Neema hamtuhitaji tena. Kwa vitendo na hata kwa maneno mmeonyesha hivyo:

1. Mmetuongezea mzigo wa gharama za maisha kwa kuongeza kodi za mafuta ya magari.
2. Mmetuletea tozo mpya kwenye miamala ya simu:


3. Vigogo nyie kulipa kodi tu hakuwahusu.
4. Kuna wabunge 19 kinyume cha katiba mzigo wa malipo yao mmeuweka kwetu.
5. Wizi wa pesa tunazokamuliwa kama ripoti kadhaa za CAG zinavyoonyesha umeamua kuufumbia macho.
6. Mashirika yanayozalisha hasara mnazotuvisha sisi unaendelea kuyakumbatia.
7. Wenzetu mnaendelea kupeana takrima za magari na majumba ya mabilioni ya pesa kwa gharama zetu.
8. Waraka huu sasa unatuhusu sisi, bila shaka mnapopanga kutuokotezea chanjo kanjanja zisizowahusu nyie:


9. Ninyi mnapotumbua kwa gharama zetu:


10. Sisi ni mwendo wa kugumia:


Kwani uzalishaji unaongezeka au umeongezeka? Vipi basi hata mkaongeze kodi na tozo mpya mpya kama kuna janga linalotuhusu sote, achilia mbali kutokudhibiti matumizi ya vilivyopo?

Tumekuelewa mama yetu. Yule bwana yupo. Hata njiani tukikuona hatutakusalimia.

Hii imekaa vizuri.
 
Kulalamika kila kukicha hakuongezi tija serikalini.

Mengi uliyoandika ni hisia tu, unao ushahidi kwamba wewe na mimi tusipolipa kodi bado serikali itashindwa kununua magari yanayotumiwa na viongozi wa serikali?.

Tatizo letu ni kujipatia haki mpaka kupitiliza, kwamba mimi na wewe tusipolipa kodi basi wale wabunge maisha yao hayataendelea kuwa kama yalivyo!. Naielewa concern yako kama mlipa kodi lakini maisha yanaendelea pasipo mimi na wewe kuwa sehemu ya walipa kodi.

Ufisadi upo tangu enzi za Yesu na Mohamed, sio jambo la kumalizika leo eti kwa mimi na wewe kuwa na uhuru wa kuhoji. Hasara za makampuni zipo dunia nzima, zipo kwenye mataifa yote.

Kodi hazikwepeki hata kama mimi na wewe tunaweza kuwa na mchango mdogo sana katika kuzilipa. Mataifa yote duniani hayawezi kujiendesha pasipo ukusanyaji wa kodi. Huo ndio ukweli na siku zote huwa unauma ukiutafakari kwa kina.
Siyo hisia kaandika ukweli mtupu! Labda wewe ni mbunge ndiyo maana unaona hayakuhusu.
 
Back
Top Bottom