Baada ya RC Makonda kugawa Mtaa kwa Pengo,Sheikh Mohamed Said asema hakuna padre wala askofu aliyepigania Uhuru wa Tanganyika

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,710
3,669



Baada ya Mkuu wa mkoa wa Dsm kuibuka na kusema kuwa ameagiza mtaa uitwe jina la Kardinal Pengo,mchambuzi wa Historia na nguli wa mambo ya uhifadhi wa habari za harakati za Uhuru,Sheikh Mohamed Said ameibuka na kusema hakuna mahali ambapo katika historia ya nchi hii kanisa katoliki wakiwemo Mapadre na maaskofu waliombea uhuru upatikane haraka.

Mzee Mohamed Said anasema katika mikutano yote ya TANU nchi nzima,ni Sheikh Takadiri pekee ndio alizunguka na Nyerere na kuomba dua kabla na baada ya kila mkutano.Mzee Said anasisitiza kuwa hata katika hotuba zake,Nyerere mwenyewe alikiri kukaa na kufunga na Wazee wa Kiislam ili kuombea Uhuru upatikane haraka,na wala hakukuwa na mahali ambapo Mapadre au Maaskofu walionekana kuambatana na Nyerere katika harakati za Uhuru.

Kisa cha Nyerere Bagamoyo kuombewa dua na wazee wa Kiislam na kuchinja mbuzi,ni moja ya uthibitisho wa wazee wa kiislamu wengi wakiwa masheikh kuunga mkono harakati za uhuru na sio mapadre wala maaskofu.

Mzee Said anasema kura 3 iliyofanyika Tabora ambapo ilimuondoa jemedari wa Siasa za TANU Sheikh Zubeir Mtevu ndio ulikuwa mwanzo wa kuuzika mchango wa Waislamu katika harakati za uhuru,na baada ya Uhuru Nyerere aliwaweka kando wazee wote wa Kiislam na kuwajumuisha wakristo ambao hawakuwa na mchango wowote katika siasa za kudai Uhuru.

Huyu Zubeir Mtevu ndio alitumwa Mafia na Nyerere kwenda kueneza TANU,maana kwa aina ya watu wa MAFIA kisiwani,Nyerere alijua hataweza kuingia na kukubalika.Mzee Said anasema hali hii ya kuwaondoa masheikh na kuingiza wengine ilishagunduliwa na Sheikh Takadiri na kuna siku alishawahi mnyooshea Nyerere kidole mbele za watu kuwa kuna dalili baada ya uhuru akawatenga wazee wa Kiislamu na kuingiza watu wake ambao hawakutoa mchango owowte katika harakati za Uhuru.

Hii hoja ya Mzee Mohamed Said inakuja baada ya Makonda kusema kuwa ameagiza Kardinali Pengo apewe mtaa Dsm kwa mchango wake,sasa bingwa huyu wa Historia anajenga hoja,ni mchango upi alioutoa Pengo katika nchi kuwashinda watu kama Zuberi Mtevu,Mshume Kiyate,Sheikh Katadiri na wengine ambao mpaka leo hawajaenziwa??
 
Sijaelewa hasa ni ipi point yake ila kama anataka mashehe nao wapewe mtaa aende akaongee na huyo mgawa mitaa ampe huyo takadiri mtaa wake tuone atafaidika nao nini?

Maana mimi kama Mkristo Mkatoliki sioni wala sijui faida itakayopatikana kiimani kutokana na Pengo kupewa mtaa as long as namjua Pengo ni mtetezi mzuri sana wa chama dola so naye wameona wamfariji kwa kumpa jina lake mtaa,nilikuwa hata sijui hii habari.

Watanzania tunajisahaulisha sana hii nchi ina mambo mengi sana ya kuyaanzishia mijadala tuachane na hizi hoja mfu zisizokuwa na kichwa wala miguu.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Hawa mashehe sijui kama hata wanaweza kuandika majina yao

Sent using Jamii Forums mobile app
Waliopigania na kuchangia mali zao, hawakuwa wanajua kuandika. Wengi ya waliokuwa wamesoma, walikuwa vibaraka wa mkolini, na walikuwa makarani wa kuvaa kaptula.

Babu zetu wengi sana hawakujua kuandika. Hiyo sio hoja kijana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Angesema mtaa upewe jina la shehe fulani mngechonga sana na kusema udini
Ila kwa kuwa upande fulani.mnawadhihaki waislamu sio

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kujishtukia,mmepawa chuo Moro,mmejengewa msikiti Kinondoni(BAKWATA)wakristk wapo kimya tena wanamtazama Yesu tegemeo lao ila nyie kitu kidogo mnalia lia sana,

Haya basi Dae kuanzia leo iitwe "Al haji Dar"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesikiliza clip unampa maagizo afisa elimu mkoa shule zote zirudishe vipindi vya dini...

Hivi unajua kama masomo ya dini yapo shuleni na mtaani? Shuleni kunasomo la Elimu ya dini ya kiislamu nakumbuka nilifanya mtihani nikiwa kidato cha pili...

Pia kuna somo la bible knowledge lipo,pia katika kila shule za serikali kuna vipindi vya dini ambavyo wanafunzi wanavitumia kupeana elimu.

Katika shule za boarding huko ndio vipindi vipo kuna jumuiya za kidini km Ukwata,Tycs,na jumuiya za waislamu TAMS..

Nafikiri na nilitegemea ungesema vipindi vilivyopo viongezewe mda au ufuatiliaji uongezeke.

Hoja zako ni muhimu sana ila ungetumia mda kidogo kuhoji nini kinaendelea shuleni.

Pia nimeona umependekeza barabara ipewe jina la porcap cardinal pengo.,kwa upande wangu ni jambo jema sana tena sana kuenzi majina ya viongozi waliofanya vuzuri.

Ila nakupa angalizo mambo ya dini magumu sana hasa katika nchi yetu ya Tz ambayo ina waumini wengi wa pande mbili..

Kivyovyote itakuhitaji kubalance mchezo nao upande wa pili watahitaji...je utakubali kuwapa mtaa? kikubwa nakushauri ongeza umakini hasa masaala ya dini..unaweza jikuta unacreat mgogoro ngumu kuuzima

Inshaallah mwenyezi Mungu akutangualie....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata Dick Turpin Way ipo London na alikuwa haramia na mwizi mkubwa na muuwaji lakini wakaamua kumuweka katika historia
Barabara ipo maeneo ya Heathrow airport
Kwa hiyo na huyu atabaki na sifa yake pia

Sent from my SM using Tapatalk
 
Back
Top Bottom