Confederate Spy
JF-Expert Member
- Sep 6, 2012
- 426
- 144
Leo ilikua siku ya kuaga mwili wa askari wa usalama barabarani aliyepata ajali maeneo ya New Sokoine Road. Katika zoezi hili la kuaga mwili wa Marehemu Mbunge wa Arusha Mjini Mh.Godbless Lema alikuwepo na MC alitangaza ratiba kuwa muwakilishi wa wananchi na kiongozi pekee aliyekuwepo Godbless Lema ataongea kutoa salamu za rambirambi.
Pia alitangaza kuwa Mkuu wa Mkoa na RPC walikua njiani kuja mahali hapo lakini alifika RPC pekee na Mkuu wa Mkoa aliingia mtini.Umati uliokuwepo ulipigwa na butwaa baada ya kuona MC anabadili utaratibu wote uliokuwepo na miongoni mwa viongozi waliotoa salamu za Rambirambi jina la Mbunge wao Godbless Lema halikuwepo.Ratiba ilibadilika baada ya MC kuitwa na Kamanda wa polisi wa mkoa na kumpa maelekezo yalioliengua jina la mbunge wa Arusha.
WAOMBOLEZAJI WACHACHAMAA:
Waombolezaji walinung'unika sana na hapa kuna mjadala mkali. Ni jambo la ajabu sana kuona viongozi wa jeshi la polisi wanaingia katika fitna za kisiasa na hasa mkoa wa Arusha ambako jeshi hili linatumika na viongozi wa kisiasa. Mzee mmoja alijikuta akipaza sauti ‘Vipi Mbunge wetu'? Polisi acheni siasa,tena mnafanya siasa msibani?
MH.GODBLESS LEMA ATOA RAMBIRAMBI SH.500,000/=
Hata hivyo Mh.Godbless Lema alitoa Rambirambi ya Sh.500'000. Alitoa laki 3 kwa ajili ya majeruhi walioko hospitali hadi muda huu na Sh.Laki 2 kwa familia ya traffic aliyefariki.
MKUU WA MKOA ATIA AIBU
Mkuu wa mkoa baada ya kugundua Mh. Lema yupo eneo hilo aliishia kwenye parking na kugeuza. Wananchi waliangua kicheko baada ya kutafsiri kitendo hicho kama njia mojawapo ya kumkimbia Mh.Lema. Mkuu wa mkoa alisikika akiwaambia maofisa walioenda kumpokea kuwa ‘Nimepata dharura,nitarudi kabla shughuli haijamalizika'
My Take: Sijui kwa siasa hizi na utendaji huu wa jeshi la polisi Arusha chini ya RPC Sabas tunaupeleka wapi mkoa huu? Aibu walizotia leo mkuu wa mkoa na kamanda Sabas zimewafanya wadharaulike sana na wananchi.
Pia alitangaza kuwa Mkuu wa Mkoa na RPC walikua njiani kuja mahali hapo lakini alifika RPC pekee na Mkuu wa Mkoa aliingia mtini.Umati uliokuwepo ulipigwa na butwaa baada ya kuona MC anabadili utaratibu wote uliokuwepo na miongoni mwa viongozi waliotoa salamu za Rambirambi jina la Mbunge wao Godbless Lema halikuwepo.Ratiba ilibadilika baada ya MC kuitwa na Kamanda wa polisi wa mkoa na kumpa maelekezo yalioliengua jina la mbunge wa Arusha.
WAOMBOLEZAJI WACHACHAMAA:
Waombolezaji walinung'unika sana na hapa kuna mjadala mkali. Ni jambo la ajabu sana kuona viongozi wa jeshi la polisi wanaingia katika fitna za kisiasa na hasa mkoa wa Arusha ambako jeshi hili linatumika na viongozi wa kisiasa. Mzee mmoja alijikuta akipaza sauti ‘Vipi Mbunge wetu'? Polisi acheni siasa,tena mnafanya siasa msibani?
MH.GODBLESS LEMA ATOA RAMBIRAMBI SH.500,000/=
Hata hivyo Mh.Godbless Lema alitoa Rambirambi ya Sh.500'000. Alitoa laki 3 kwa ajili ya majeruhi walioko hospitali hadi muda huu na Sh.Laki 2 kwa familia ya traffic aliyefariki.
MKUU WA MKOA ATIA AIBU
Mkuu wa mkoa baada ya kugundua Mh. Lema yupo eneo hilo aliishia kwenye parking na kugeuza. Wananchi waliangua kicheko baada ya kutafsiri kitendo hicho kama njia mojawapo ya kumkimbia Mh.Lema. Mkuu wa mkoa alisikika akiwaambia maofisa walioenda kumpokea kuwa ‘Nimepata dharura,nitarudi kabla shughuli haijamalizika'
My Take: Sijui kwa siasa hizi na utendaji huu wa jeshi la polisi Arusha chini ya RPC Sabas tunaupeleka wapi mkoa huu? Aibu walizotia leo mkuu wa mkoa na kamanda Sabas zimewafanya wadharaulike sana na wananchi.