Baada ya Panga la EU kuishukia Tanzania, Shoka la Muingereza hilo njiani linakuja!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,582
Ukiona mwenzako ananyolewa, wewe tia maji kichwa chako ndicho kitakachofuatia.
Panapofuka moshi, chini kuna moto, na ukiona kwa mwenzako kunaungua, kwako kunateketea!

Nimeangalia breaking news ya Sky News, Serikali ya Uingereza imeamua kubana matumizi, mawaziri hakuna fungu la mafuta (fuel allowance) na badala yake ni lazima kutumia public transport. Hakuna tena kusafiri daraja la kwanza, first class, kwa watumishi wote wa umma!.

Hizi ndizo hizo dalili za kufuka kwa moshi, ama huko kunaungua, basi kwetu kunateketea.

Uingereza ndiyo nchi inayochangia fungu kubwa kuliko nchi nyingine yoyote kwenye lile kapu kubwa la hazina kwa jina la General Budget Support, kama mtoaji anaanza kubana matumizi, sidhani kama ataendelea kuchangia bajeti yetu ambapo mawaziri bado wanajivinjari kwa ma 4-wheel huku mwenye pesa akipanda dala dala. Au wanene wetu wakisafiri 1st Class huku mwenye pesa akisafiri Economy, au Bussiness.

Taarifa hii ni angalizo tuu kufuatia dalili ya mvua.

Pia sio vibaya kujiuliza kama wenye hela, wameamua hakuna kupata 1st Class, sisi masikini wa kutupwa tunapandia nini hizi 1st Class?!.

Kama Tanzania imepata uhuru wake zaidi ya miaka 46 iliyopita, kitendo cha kuendelea kutegemea bajeti tegemezi, sio kipimo tosha cha failed economy ya chama kilichoshika nchi, tufike mahali tukiweke pembeni na kufungua ukurasa mpya?.

Pamoja na utajiri mkubwa wa ardhi yenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, kuanzia maziwa, mito, vijito, chemchemi, mifereji mpaka mabwawa, lakini kilimo chetu kwanini bado kinategemea mvua mpaka leo?!.

Tumezungukwa na madini ya kila aina, kuanzia Almasi, dhahabu, Tanzanite, chuma, shaba, fedha, vito kedekede, nk, nk huu umasikini unatokana na nini?!.

Watanzania tufike mahali tuseme basi!, imetosha!.

Mungu Ibariki Tanzania,
 
Kama Tanzania imepata uhuru wake zaidi ya miaka 46 iliyopita, kitendo cha kuendelea kutegemea bajeti tegemezi, sio kipimo tosha cha failed economy ya chama kilichoshika nchi, tufike mahali tukiweke pembeni na kufungua ukurasa mpya?.

Pamoja na utajiri mkubwa wa ardhi yenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, kuanzia maziwa, mito, vijito, chemchemi, mifereji mpaka mabwawa, lakini kilimo chetu kwanini bado kinategemea mvua mpaka leo?!.

Tumezungukwa na madini ya kila aina, kuanzia Almasi, dhahabu, Tanzanite, chuma, shaba, fedha, vito kedekede, nk, nk huu umasikini unatokana na nini?!.

Watanzania tufike mahali tuseme basi!, imetosha!.

Mungu Ibariki Tanzania,

Japan waliamua basi, USA waliamua basi, UK wameamua basi, Zambia waliamua basi, Tz ndo usingizi tororooooooooooo! Kama kuna mabadiliko labda yaletwe na Mungu...
 
Japan waliamua basi, USA waliamua basi, UK wameamua basi, Zambia waliamua basi, Tz ndo usingizi tororooooooooooo! Kama kuna mabadiliko labda yaletwe na Mungu...
Kwa vile muda wa maamuzi ya kusema basi au la ni Octoba, Watanzania, wakiamua, wanaweza kuamua kusema Basi, tatizo sijui ni kwa nini hawaamui, tuhamasishe October waseme basi, INAFU!.
 
Ni kwa Serikali ya JK kubana matumizi ktk maeneo yafuatayo:
1. Ununuzi (procurement) ambako kuna leakage 30% ya bajeti ya taifa;
2. Misamaha ya kodi inayolingana na 30% ya bajeti ya taifa;
3. Magari ya kifahari. Grand Vitara na Rav4 zinawatosha Mawaziri wetu wanaoishi hapo Makumbusho; na
4. Kupunguza safari pamoja na Posho lukuki za Waheshimiwa wetu.

Kwa kufanya hayo manne kikamilifu nchi itakwenda murua kabisa:angry:
 
Hakuna tena kusafiri daraja la kwanza, first class, kwa watumishi w
Pia sio vibaya kujiuliza kama wenye hela, wameamua hakuna kupata 1st Class, sisi masikini wa kutupwa tunapandia nini hizi 1st Class?!.

Bahati nzuri au mbaya huwa nasafiri sana na waheshimwa nikiwa kwenye shughuli zangu. Unajuwa huwa nasikia hasira nikiwaona business wakati naeleka zangu economy. Si kwamba huwa nawaonea wivu no nahisi kwamba hawajuwi walitendalo infact huwa natamani kuwazaba vibao. Eti waziri, waziri unawangoza watu hata mlo mmoja unawashinda, hospital wakienda kujifungua wanalala kitanda kimoja watatu wewe unaona raha kabisa kupanda business class kama sio kuumwa ni nini huku? Nani amewambia sisi tunaopanda economy tunapungua?

Hili linanikumbusha kile kisa cha wahisani ambacho viongozi wetu na ujumbe wa wahisani toka nchini walisafiri pamoja nadhani kwenda Paris kwenye meeting ya namna ya kutusaidia. Mmoja katika ujumbe wa wahisani alishikwa na butwaa alipoona kigogo wetu mmoja akiwa business class wakati yeye mfadhili yuko economy. Ilibidi aulize hivi yupi anaenda kusaidiwa hapa yeye aliyepanda economy au kigogo wetu aliyepanda business class? hii ndio bongo tumeweka pamba masikioni, huku ni zaidi ya kulogwa sio bure.
 
Bahati nzuri au mbaya huwa nasafiri sana na waheshimwa nikiwa kwenye shughuli zangu. Unajuwa huwa nasikia hasira nikiwaona business wakati naeleka zangu economy. Si kwamba huwa nawaonea wivu no nahisi kwamba hawajuwi walitendalo infact huwa natamani kuwazaba vibao. Eti waziri, waziri unawangoza watu hata mlo mmoja unawashinda, hospital wakienda kujifungua wanalala kitanda kimoja watatu wewe unaona raha kabisa kupanda business class kama sio kuumwa ni nini huku? Nani amewambia sisi tunaopanda economy tunapungua?

Hili linanikumbusha kile kisa cha wahisani ambacho viongozi wetu na ujumbe wa wahisani toka nchini walisafiri pamoja nadhani kwenda Paris kwenye meeting ya namna ya kutusaidia. Mmoja katika ujumbe wa wahisani alishikwa na butwaa alipoona kigogo wetu mmoja akiwa business class wakati yeye mfadhili yuko economy. Ilibidi aulize hivi yupi anaenda kusaidiwa hapa yeye aliyepanda economy au kigogo wetu aliyepanda business class? hii ndio bongo tumeweka pamba masikioni, huku ni zaidi ya kulogwa sio bure.
.
Hii ya Waingereza kupunguza fungu la budget support itaiamsha serikali yetu kupunguza matanuzi na matumizi yasiyo ya lazima.

Shirika la misaada la Uswisi, SwissAid, liliwachukua Watanzania masikini kwenda kuishi nyumba za matajiri wa Uswiss, jamaa ni matajiri kikukweli kweli, lakini amini usiamini, kuna wanaokwenda makazini kwa baikeli na public transport huku ma Ferasri yao yamepaki nyumbani yakisubiri week-end.

Ilipofika zamu ya Matajiri hao wa Uswisi kutembelea Tanzania, tukawatembeza Jumba la Makumbusho pale Mtaa wa Shaaban Robert, siku hiyo pia ilikuwa ni siku ya semina fulani kwa Wabunge wa Bunge letu, wageni wetu wakauliza haya magari ya nani na kuna nini?.

Tukawajibu haya ni magari ya Wabunge wetu na Mawaziri wetu. Wageni walishangaa, wakasema hata serikali ya Uswisi, ambao ni matajiri, hawawezi kuwa na fleet kubwa hivyo ya Ma 4-Wheels!, wakauliza kwa mtaji huu, Tanzania mnavyojiita nchi masikini, mna umasikini gani?.

Pamoja na hitaji halisi la 4 whells kutokana na mabarabara yetu, Land Cruser Hard Top (Mkonga) zingetosha kabisa, ma- VX na GX ni total laxury, tena Mkulu ndio kafunga kazi kabisa, kanunua fleet ya 10 BMW X5 kwa ajili ya Ikulu, barabara za matope haiwezi, ndio mambo ya jana kurudia gazi za zamani hazina servise, kazi ikawa kubadili badili magari, huku mengine yakichomoka tairi!.

Tanzania sio masikini, its only poor planing ya vipaumbele vyetu ni nini.

Lazima tufike mahali tuseme, Inatosha!.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Kwa vile muda wa maamuzi ya kusema basi au la ni Octoba, Watanzania, wakiamua, wanaweza kuamua kusema Basi, tatizo sijui ni kwa nini hawaamui, tuhamasishe October waseme basi, INAFU!.

Huge proposition. As someone said somewhere in JF -- tunmejaliwa makundi ya kondoo badala ya binadamu! Just bad luck!
 
Ni ajali tu wala msiunde TUME jamani, hiyo hela ya tume pelekeni Amana Hospital
 
Si mtakii mtu mabaya lakini kwa hili lazima niseme, jana ningetamani gari la KIFAHARI la ikulu lingechomoka tairi wakati JK yumo humo akaona na kupata kile watanzania walala hoi wanavyoteseka na kuumia kila siku kwa barabara mbovu huku wakubwa wakinunua ma-4 wheels ili wasipata tabu kwenye hizo barabara mbovu. Watanzania tunapenda starehe mno kuliko kazi, mfano hapa job kijana kaajiriwa juzi anakula mkopo crdb na kununua GX 100 6 cylinder la kwendea job na sokoni, niambie mtu kama huyu na mafuta yalivyopanda bei hatachukua rushwa kweli na unatarajia akapata ukurugenzi serikalini si atataka anunuliwe nae VX V8 la kwendea kazini, sokoni, kupeleka mama saluni na watoto shule? Inabidi tubadili jinsi ya matumizi yetu kuanzia ngazi ya familia mpaka ngazi ya juu kwani "TABIA NI SAWA NA RANGI YA NGOZI KUIBADILI KAZI".

Nawakubali rwanda na kenya kwa afrika na uingereza kwa ughaibuni kwa kuamua kuondoa na kuuza magari makubwa yanayoiletea hasara serikali ili hela ziende zaidi kwenye kuboresha huduma za kijamii kama barabara, hospital na maji nk.Sisi kama wabongo ndo kwanzaaaa VX V8 tunanunua kama nyugu matokeo yake matumizi ya serikali ni makubwa kuliko kuboresha huduma kwa wananchi.

Tuungane ili tuitoe madarakani serikali ya CCM ambayo imeshindwa kupunguza matumizi ya serikali na kuwafanya wananchi wawe na maisha maguma kuliko maelezo.

Mkereketwa....
 
Back
Top Bottom