#COVID19 Baada ya mtu kupata chanjo ya Covid-19 miongoni mwa mambo ya kuzingatia ni kutopata kilevi cha aina yoyote kwa saa 72 (siku tatu)

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Wataalamu wa afya na watafiti wa chanjo wanasema pombe na dawa ya chanjo vyote vinakwenda kwenye ini, hivyo upo uwezekano wa ini kuongezewa mzigo na kulichosha lakini pia kilevi huingilia kazi ya dawa kama ilivyo kwa dawa zingine hivyo kupunguza ufanisi.

Mkurugenzi wa kuratibu na kukuza utafiti kutoka Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) Dk Paul Kazyoba amesema kilevi cha aina yoyote hakitakiwi baada ya kuchanja kwani kitaingilia mfumo wa uzalishaji wa kinga za mwili ambao unafanywa na chanjo kwa saa za mwanzo.

Dk Kazyoba amesema chanjo inapochomwa katika mwili wa binadamu, ikiingia inaenda kuzisisimua seli za kinga ‘antibodies’ zinazalishwa zikishajaa mwilini zinakua askari wa kupambana na kirusi kitakachoingia.

“Kuufanya mwili uzalishe hizi seli kinga, inatakiwa usiingiliwe na kitu chochote cha tofauti kwenye damu kwa saa 72. Kilevi cha aina yoyote kwa maana ya pombe, bangi, shisha au dawa za kulevya lazima kitaingilia mfumo na hivyo kuifanya chanjo kutofanya kazi yake vizuri.

“Ndani ya saa 72 ni muda ambao kazi kubwa inafanyika hapo na ndiyo maana maudhi madogo madogo mtu anayapata ndani ya huo muda, vilevi vitaathiri uzalishaji wa mwanzo wa seli za kinga, ambazo zitajitengeneza mwilini mwako kwa miezi kadhaa,” amesema Dk Kazyoba.
 
Wataalamu wa afya na watafiti wa chanjo wanasema pombe na dawa ya chanjo vyote vinakwenda kwenye ini, hivyo upo uwezekano wa ini kuongezewa mzigo na kulichosha lakini pia kilevi huingilia kazi ya dawa kama ilivyo kwa dawa zingine hivyo kupunguza ufanisi.

Mkurugenzi wa kuratibu na
Basi huu ndiyo utakuwa muda mrefu zaidi wa mimi kutokupata bia kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 iliyopita. Dah naweza nikaacha kabisa!
 
Baada ya mtu kupata chanjo miongoni mwa mambo ya kuzingatia yanayosisitizwa ni kutopata kilevi cha aina yoyote kwa saa 72 sawa na siku tatu.

Wataalamu wa afya na watafiti wa chanjo wanasema pombe na dawa ya chanjo vyote vinakwenda kwenye ini, hivyo upo uwezekano wa ini kuongezewa mzigo na kulichosha lakini pia kilevi huingilia kazi ya dawa kama ilivyo kwa dawa zingine hivyo kupunguza ufanisi.

Mkurugenzi wa kuratibu na kukuza utafiti kutoka Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) Dk Paul Kazyoba amesema kilevi cha aina yoyote hakitakiwi baada ya kuchanja kwani kitaingilia mfumo wa uzalishaji wa kinga za mwili ambao unafanywa na chanjo kwa saa za mwanzo.

Dk Kazyoba amesema chanjo inapochomwa katika mwili wa binadamu, ikiingia inaenda kuzisisimua seli za kinga ‘antibodies’ zinazalishwa zikishajaa mwilini zinakua askari wa kupambana na kirusi kitakachoingia.

“Kuufanya mwili uzalishe hizi seli kinga, inatakiwa usiingiliwe na kitu chochote cha tofauti kwenye damu kwa saa 72. Kilevi cha aina yoyote kwa maana ya pombe, bangi, shisha au dawa za kulevya lazima kitaingilia mfumo na hivyo kuifanya chanjo kutofanya kazi yake vizuri.

“Ndani ya saa 72 ni muda ambao kazi kubwa inafanyika hapo na ndiyo maana maudhi madogo madogo mtu anayapata ndani ya huo muda, vilevi vitaathiri uzalishaji wa mwanzo wa seli za kinga, ambazo zitajitengeneza mwilini mwako kwa miezi kadhaa,” amesema Dk Kazyoba.

Kitu kingine ambacho amekisema ni mwili kuutayarisha kabla ya chanjo ambapo alisema ni muhimu mwili ukawa na sawa na wenye nguvu za kutosha.

“Muda huo unaingiza kitu kipya mwilini, unaposhtuka na kuanza kupata uchovu na maudhi pale ndiyo unazalisha seli kinga kuuandaa mwili ili adui akijaribu kuingia akutane na kinga muda huo kama ukiona maudhi yanazidi mtafute daktari japokuwa wanaopata hali hiyo ni wachache,” amesema.

Kati ya mambo ya kuzingatia baada ya kuchoma chanjo, inatakiwa mtu aushughulishe mwili kwa kipindi cha saa 72 za awali kwani kwa kufanya hivyo seli za kinga huzalishwa kwa wingi na huwa na manufaa zaidi tofauti na kinyume chake.

Nipashe Gazeti
 
Daaaaaaa Yani bia izuiwe na chanjo haiwezekani kumbe ndiyo maana Gwaji boy anapinga chanjo kwani kuacha bia kwa siku 3 labda yesu afufuke Tena.
 
Dah yaani juzi tulichoma asubuhi jioni tukaenda club kujipongeza.. Na tuligida ulabu hasa


Na wewe umechanja???, Hivi umeshindwa kutumia tunguli zako dhidi ya Covid??!---- kweli mzungu ni zaidi ya tunguli,🤣
 
Wanaoenda kuchanjwa wote wanapewa elimu hii au wengine washanjwa ila hawakuwa wakijua na leo ndio wamejua?
 
Wataalamu wa afya na watafiti wa chanjo wanasema pombe na dawa ya chanjo vyote vinakwenda kwenye ini, hivyo upo uwezekano wa ini kuongezewa mzigo na kulichosha lakini pia kilevi huingilia kazi ya dawa kama ilivyo kwa dawa zingine hivyo kupunguza ufanisi.

Mkurugenzi wa kuratibu na kukuza utafiti kutoka Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) Dk Paul Kazyoba amesema kilevi cha aina yoyote hakitakiwi baada ya kuchanja kwani kitaingilia mfumo wa uzalishaji wa kinga za mwili ambao unafanywa na chanjo kwa saa za mwanzo.

Dk Kazyoba amesema chanjo inapochomwa katika mwili wa binadamu, ikiingia inaenda kuzisisimua seli za kinga ‘antibodies’ zinazalishwa zikishajaa mwilini zinakua askari wa kupambana na kirusi kitakachoingia.

“Kuufanya mwili uzalishe hizi seli kinga, inatakiwa usiingiliwe na kitu chochote cha tofauti kwenye damu kwa saa 72. Kilevi cha aina yoyote kwa maana ya pombe, bangi, shisha au dawa za kulevya lazima kitaingilia mfumo na hivyo kuifanya chanjo kutofanya kazi yake vizuri.

“Ndani ya saa 72 ni muda ambao kazi kubwa inafanyika hapo na ndiyo maana maudhi madogo madogo mtu anayapata ndani ya huo muda, vilevi vitaathiri uzalishaji wa mwanzo wa seli za kinga, ambazo zitajitengeneza mwilini mwako kwa miezi kadhaa,” amesema Dk Kazyoba.
Tumbaku je kwa maana nayo tumbaku ni kama ulevi, pia kahawa , cocacola, vinywaji vya kutia nguvu je?
 
Kwa sisi ambao hatuna maini je? Tunaruhusiwa kunywa bia mara tu baada ya kuchanjwa? Masaa 72 ni mengi mjue.
Pana swahiba wangu yeye aliwahi kuniambia angekuwa anaweza basi angetengenezewa kijimfuko hapo tumboni kuwe na zip yaani unafungua unaweka chakula ili mdomo ubaki wa kunywea bia tu sasa Kwa sharti hili wacha niwasiliane nacho nitawajuza mrejesho.
 
sababu kuu ni kuwa chanjo hii uenda moja kwa moja kwenye ini hivyo ukinywa pombe ndani ya huo muda basi itaharibu ini
 
Back
Top Bottom