Baada ya mkataba huu mnono nini hatima ya soka la Zanzibar?

ibanezafrica

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,261
6,543
Baada ya majuzi Azam kupata haki ya kuonyesha VPL kwa mkataba wa miaka kumi walitamka na kiasi kitakacholipwa klabu zote shiriki
Kilichokuja nistua na kuniuma nilipokuja sikia kipindi cha michezo jioni hiyo cha wasafi fm wakitangaza habari ya mechi iliyochezwa huko unguja wikiendi ambapo mwisho wa mechi hiyo kila timu ilipata mgao wa Tsh 1,500/-. Kwa kwel hii kitu imeniumiza sana
Binafsi naelewa kuwa Zanzibar imejaaliwa vipaji hususan soka,najiuliza tatizo ni nini?

Kwanini Zanzibar tunashindwa kuitumia katika jamhuri ili tuwe na kikosi kizuri Taifa stars? Kwanini Isisaidiwe kama kuna changamoto zinazoifanya ibaki nyuma? Mbona zamani ilikua na tinu nzuri na zikaleta changamoto hadi huku bara?ninakumbuka enzi za KMKM,Small Simba nk...nini kilipelekea zikapotea?

Azam amemwaga pesa kwa klabu hizi za bara vipi Znz?basi hakuna jitihada zozote kati ya Azam/TFF/ZFF kuweka mambo sawa?
Tusiwaache ndugu zetu wazanzibar katika kukuza thamani na ubora wa soka letu.itasikitisha sana ikiwa tutaendelea kuishi hivi kama Jamhuri ya muungano.

Tusiiache Zanzibar.
 
Wafanyabisshara ni capitalists, haijadhamini ligi kutokana na kuipenda bara, industry ya burudani /sports inakuwa kwa kasi. Kupitia humo Azam anataka ajitangaze vizuri. Isinhekuwa kujitangaza kibiashara angetumia sehemu ya hizo pesa kuijenga Azam FC.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Mpira tunangalia bar kule mambo ya bia hawataki sasa utapataje coverage. Watoe kwanza masharti yao. Mpira ni mpira na dini ibaki kuwa dini.
 
Hapo kwny 1,500/= umekosea mkuu?

Naon kama ni masikhara haitosh hata kunnua glucose kwa wachezaji..
Mimi mwenyewe sikuamini na hadi watangazaji wakawa wanacheka,hivyo ndivyo ilivyokua labda kama kuna mdau toka zanzibar atuthibitishie hili
 
Wazanzibar wana haha sana wana nafasi mbili wacheze bara na kwao lakini roho mbaya waliyonayo ndio inawauwaa .

Sisi tukienda zanzibar watakubali hao watu na roho zao za paka.
 
Baada ya majuzi Azam kupata haki ya kuonyesha VPL kwa mkataba wa miaka kumi walitamka na kiasi kitakacholipwa klabu zote shiriki
Kilichokuja nistua na kuniuma nilipokuja sikia kipindi cha michezo jioni hiyo cha wasafi fm wakitangaza habari ya mechi iliyochezwa huko unguja wikiendi ambapo mwisho wa mechi hiyo kila timu ilipata mgao wa Tsh 1,500/-. Kwa kwel hii kitu imeniumiza sana
Binafsi naelewa kuwa Zanzibar imejaaliwa vipaji hususan soka,najiuliza tatizo ni nini?

Kwanini Zanzibar tunashindwa kuitumia katika jamhuri ili tuwe na kikosi kizuri Taifa stars? Kwanini Isisaidiwe kama kuna changamoto zinazoifanya ibaki nyuma? Mbona zamani ilikua na tinu nzuri na zikaleta changamoto hadi huku bara?ninakumbuka enzi za KMKM,Small Simba nk...nini kilipelekea zikapotea?

Azam amemwaga pesa kwa klabu hizi za bara vipi Znz?basi hakuna jitihada zozote kati ya Azam/TFF/ZFF kuweka mambo sawa?
Tusiwaache ndugu zetu wazanzibar katika kukuza thamani na ubora wa soka letu.itasikitisha sana ikiwa tutaendelea kuishi hivi kama Jamhuri ya muungano.

Tusiiache Zanzibar.
Soka ni biashara, na linahitaji wafanyabiashara wawekeza, na watu ambao uchumi wao ni mzuri watalipa viingilio kwa bei ya juu na wanaweza kununu products ambazo zitatangwazwa, Lazima tuwe wakweli tuachane na viongozi wanaofuata mifumo ya kijamaa inawafanya watu masikini.
 
Nadhani kosa kubwa au mwanzo wa league ya Zanzibar kufa ligi ya muungano ilivyokufa sijui ilikuwa kwa lengo ya Zanzibar kuwa na uwakilishi CAF bila kupitia league ya muungano iliyokuwa inajumuisha team tatu bara na 3 visiwani, wakati huo Malindi, Small Simba, Miembeni na KMKM zilikuwa zinaleta upinzani na walikuwa vizuri sana tu sasa fikiria ile league ingekuwepo na pesa kuingizwa team zingejijenga na kuleta ushindani mkubwa na bingwa angekuwa kweli bingwa wa Tanzania. Mimi nadhani kosa lao kubwa uroho wa pesa kuwa watapata direct kutoka CAF bila team kupitia ushindani wa kweli matokeo ni haya league wameuwa ila viongozi wanatumia jina tu Zanzibar kula pesa ya CAF.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom