Baada ya matukio haya (1962-2021) katika mkoa wa Ziwa Magharibi(Kagera) Serikali ilipaswa kuja na mpango maalumu wa maendeleo katika mkoa huu

Artificial intelligence

JF-Expert Member
Jan 28, 2021
1,262
2,191
Historia ya Mkoa kabla ya Uhuru

Kabla ya Uhuru na hadi kufikia mwaka 1961, eneo la sasa la Mkoa wa Kagera, lilikuwa ni moja ya maeneo yaliounda jimbo lililoitwa “Lake Province”. Jimbo hili lilijumuisha Wilaya za Bukoba, Musoma, Shinyanga na Tabora. Baada ya uhuru mwaka 1962 mkoa ulibadilishwa jina na kuitwa ‘West Lake Region’ (Ziwa Magharibi) na kujumuisha Wilaya 4 za Ngara, Biharamuro, Karagwe na Bukoba.

Kabla ya mwaka 1979, mkoa huu wa Kagera ulikuwa unaitwa “Ziwa Magharibi”. Jina hilo lilibadilishwa na kuwa “Kagera” mwaka 1979, mara baada ya vita kati ya Tanzania na Uganda, ambapo mkoa, chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa, aliyekuwepo wakati huo, Capt. Peter Kafanabo, ulipendekeza uitwe “Kagera”. Pendekezo la kuubadlisha jina Mkoa wa Ziwa Magharibi na kuitwa Kagera lilitokana na Mto Kagera kugusa sehemu kubwa ya wilaya zote zinazounda mkoa huu ukiwa unatiririsha maji yake kutoka Rwanda kupitia kaskazini na kumwaga maji yake katika Ziwa Victoria.

MATUKIO MAKUU 1962 – 2021
Katika kipindi cha miaka sitini tangu tupate uhuru yapo matukio mengi ya kihistoria ambayo yametokea katika mkoa wa Kagera. Mtiririko wa matukio hayo ni kama yanavyoainishwa hapa chini.

Mwaka 1962
Mafuriko: Mvua kubwa ilinyesha na mafuriko kutokea sehemu kubwa ya Mkoa, ambapo wananchi waliipa jina la “Mvua ya Uhuru” kwa sababu mvua kubwa ya masika ilinyesha baada ya Tanganyika kupata Uhuru.

Mwaka 1966
Ukame: Ukame mkubwa uliodumu hadi mwaka 1970 watokea na kusababisha njaa kali katika wilaya ya Karagwe. Hali hiyo ilisababisha baadhi ya watu kupoteza maisha, kupungua kwa nguvukazi, baadhi ya familia kukosa matunzo kwa ukaribu baada ya wanaume kwenda maeneo ya mbali kutafuta chakula.

Mwaka 1978
Vita kati ya Tanzania na Uganda: Mwezi Oktoba 1978 kulitokea vita kati ya nchi ya Tanzania na nchi ya Uganda. Vita hii ilijulikana kwa jina maarufu la “vita ya Kagera” iliitwa jina hilo kutokana kwamba ilipiganiwa katika ardhi ya Tanzania mkoani Kagera.

Vita hii ilisababishwa na kitendo cha Majeshi ya Uganda, chini ya Nduli Idd Amin Dada, kuvamia ardhi ya Tanzania katika eneo la Missenyi na kudai kuwa eneo lote lililo kaskazini mwa Mto Kagera ni ardhi ya nchi ya Uganda. Vita hivyo vilimalizika mwezi April, 1979 kwa Majeshi ya Tanzania kushinda vita na kumuondoa madarakani Nduli Idd Amin.Vita hivi vya Kagera vilikuwa na athari kubwa kwa mkoa wa Kagera. Athari hizo ni pamoja na vifo, wananchi kunyang’anywa mali zao na uharibifu wa miundombinu ya majengo na barabara.

Mwaka 1983
Operesheni Uhujumu Uchumi: Kutokana na kukosekana kwa bidhaa muhimu katika jamii na kupungua kwa uwianao wa kipato kati ya walio nacho na wasio nacho serikali iliendesha operesheni dhidi ya wahujumu uchumi nchi nzima. Wafanyabiashara wa Mkoa wa Kagera walitupa bidhaa zao kwenye Ziwa Victoria na mto Ngono ili kuhofia kukamatwa na Serikali.

Kugunduliwa kwa Mgonjwa wa UKIMWI: Ugonjwa ambao unadhoofisha kinga za mwili za kujikinga na maradhi ambao baadae ulikuja kujulikana zaidi kama UKIMWI (Ukosefu wa Kinga Mwilini) uligundulika kwa mara ya kwanza nchini Tanzania mkoani Kagera.

Mgojwa wa kwanza aligundulika kuwa na virusi vya UKIMWI alitoka katika Kijijini cha Kanyigo Wilaya ya Missenyi. Mwanzoni wananchi wa Mkoa wa Kagera waliuita ugonjwa huo “Juliana” au “Slim”. Uliitwa Juliana kwa sababu iliaminika kuwa ugonjwa huo uliingizwa nchini na vijana waliokuwa wakitokea Uganda wakiwa wamevaa mashati ya Juliana. Pia uliitwa ‘slim’ kwa sababu waathirika wa ugonjwa huo walikuwa wanakonda hadi kufa. Ugonjwa huu baadae ulienea Tanzania nzima na kuleta athari kubwa katika jamii. Mkoa wa Kagera ulikuwa wa kwanza kuathirika. Ugonjwa huu uliwakumba zaidi vijana, wanajamii ambao wanaotegemewa sana katika uzalishaji mali. Vijana wengi wakaangamia kwa UKIMWI na kufanya familia nyingi kubaki na wazee wakibeba mzigo wa kutunza watoto yatima. Pia muda mwingi wa kuzalisha mali ulipotea katika kuhudhuria mazishi na matanga ya ndugu na jamaa, kuuguza wagonjwa na kutunza yatima. Ugonjwa wa UKIMWI bado upo mpaka sasa katika mkoa wa Kagera na Tanzania kwa ujumla.

Mwaka 1994
Kuingia kwa Wakimbizi wa Rwanda na Burundi: Kutokana na mapigano ya kikabila nchini Burundi na mauaji ya kimbari nchini Rwanda, inakadiriwa kuwa Wanyarandwa na Warundi laki sita (600,000) waliingia mkoani Kagera wakikimbia mapigano hayo. Ujio wa wakimbizi ulisababisha madhara makubwa kwa mkoa wa Kagera
yakiwemo uharibifu wa mazingira na kushamili kwa uhalifu mwingiliano wa utamaduni na kuzaliana.

Mwaka 1995
Mvua kubwa: Mvua kubwa ilinyesha na kusababisha mafuriko na uharibifu wa mazao na miundombinu.Mafurikoyaliathiri sana Wilaya yote ya Bukoba na Missenyi. Madaraja yalisombwa na maji hivyo kuathiri watumiaji na baadhi ya nyumba za watu ziliharibiwa.

Mwaka 1996
Kuzama kwa MV Bukoba: MV Bukoba ikiwa safirini kutoka Bukoba kwenda Mwanza, ilizama katika Ziwa Victoria kilomita nane kabla ya kufika bandari ya Mwanza. Inakadiriwa kuwa watu mia nane (800), wengi wao walikuwa wakazi wa mkoa wa Kagera, walipoteza maisha huku mali yenye thamani ya mamilioni ya shilingi ilipotea. Sababu za kuzama kwa meli hiyo kulisababishwa na ujazaji wa abiria na miziko kupita uwezo wake.

Mwaka 2016
12 Septemba 2016
Tetemeko la ardhi la nguvu ya 5.7 katika vipimo vya Richter lilitokea eneo la Bukoba, kaskazini magharibi mwa Tanzania na kusababisha maafa.

Kitovu cha tetemeko hilo kilikuwa takriban kilomita 44 kutoka mji wa Bukoba, ambao ni mji mkuu wa mkoa wa Kagera, kwa mujibu wa taasisi ya jiolojia ya Marekani.Nyumba nyingi ziliporomoka na kuwaacha mamia ya watu wakiwa bila makao.Tetemeko hilo ndilo mbaya zaidi kukumba Tanzania katika kipindi cha zaidi ya mwongo mmoja.

Kwahiyo badala ya serikali kuendelea kuugawa mkoa wa Kagera, ni vyema ingekuja na mpango wa maendeleo katika mkoa yaani "Special Economic Rehabilitation program" ili kuchochea maendeleo zaidi katika mkoa huu unao kwamishwa na majanga zaidi licha ya wakazi wake kujitahidi kujikwamua kiuchumi.
 
Kama hujui historia ungeuliza kwanza kwa wanaojua kabla ya kutoa uzi.
Usahihi ni kwamba kabla ya uhuru wa Tanganyika mkoa wa Kagera ulikuwa katika Jimbo la Ziwa lenye Wilaya za Bukoba, Ngara, Biharamulo, Karagwe, Geita, Mwanza, Kwimba, Maswa, Ukerewe, Shinyanga, North Mara na South Mara na makao makuu ya Jimbo hili yalikuwa katika mji wa Mwanza.

Ilipofika mwaka 1959 Jimbo la Ziwa liligawanywa na kupata Jimbo la Ziwa Magharibi lenye Wilaya za Bukoba, Biharamulo, Ngara na Karagwe na kuifanya Tanganyika kuwa na majimbo Tisa badala ya manane yaliyokuwepo kabla ya mwaka 1959.

Tabora ilikuwa iko Jimbo la magharibi lenye wilaya za Tabora, Mpanda, Nzega, Kahama, Kigoma, Kasulu na Kibondo na makao makuu ya Jimbo hili yalikuwa mjini Tabora. Hadi kufikia mwaka 1959 Majimbo ya Tanganyika yalikuwa ni:-

Mashariki
Kusini
Nyanda za juu kusini
Kaskazini
Kati
Tanga
Ziwa
Magharibi
Ziwa Magharibi
 
Kama hujui historia ungeuliza kwanza kwa wanaojua kabla ya kutoa uzi.
Usahihi ni kwamba kabla ya uhuru wa Tanganyika mkoa wa Kagera ulikuwa katika Jimbo la Ziwa lenye Wilaya za Bukoba, Ngara, Biharamulo, Karagwe, Geita, Mwanza, Kwimba, Maswa, Ukerewe, Shinyanga, North Mara na South Mara na makao makuu ya Jimbo hili yalikuwa katika mji wa Mwanza. Ilipofika mwaka 1959 Jimbo la Ziwa liligawanywa na kupata Jimbo la Ziwa Magharibi lenye Wilaya za Bukoba, Biharamulo, Ngara na Karagwe na kuifanya Tanganyika kuwa na majimbo Tisa badala ya manane yaliyokuwepo kabla ya mwaka 1959. Tabora ilikuwa iko Jimbo la magharibi lenye wilaya za Tabora, Mpanda, Nzega, Kahama, Kigoma, Kasulu na Kibondo na makao makuu ya Jimbo hili yalikuwa mjini Tabora. Hadi kufikia mwaka 1959 Majimbo ya Tanganyika yalikuwa ni:-
Mashariki
Kusini
Nyanda za juu kusini
Kaskazini
Kati
Tanga
Ziwa
Magharibi
Ziwa Magharibi
Hapa nimezungumuzia historia ya mkoa kwa ufupi, sijataka kuzunguka kote huko, lengo la uzi ni mkoa sio historia ya nchi. Nahisi wewe Kwa kujua kwako, umekimbilia kukoment ili uonyeshe umwamba wako katika historia anyway asante kwa kuchangia na sipo huko.

Na lengo kubwa, zaidi ni kuikumbusha serikali kuwa na mpango maalumu wa maendeleo kwenye mkoa, kutokana na majanga yaliyo ukumba mkoa.
 
Nimeshituka ulipoandika kwamba Tabora ilikuwa Kanda ya Ziwa. Nikaona nikurekebisha kidogo.
Hapa nimezungumuzia historia ya mkoa kwa ufupi, sijataka kuzunguka kote huko, lengo la uzi ni mkoa sio historia ya nchi. Nahisi wewe Kwa kujua kwako, umekimbilia kukoment ili uonyeshe umwamba wako katika historia anyway asante kwa kuchangia na sipo huko.

Na lengo kubwa, zaidi ni kuikumbusha serikali kuwa na mpango maalumu wa maendeleo kwenye mkoa, kutokana na majanga yaliyo ukumba mkoa.
 
Mbona vita vya Kagera serikali ilipambana sana sisi wasukuma kila familia ilichanga ng'ombe mmoja.
Ni kweli wakati wa vita taifa zima lilishikamana kwa umoja kushinda vita ile, ila baada ya vita athari kubwa ilibaki kwenye mkoa wa Kagera, kwahiyo sio vibaya Serikali ingekuja na mpango wa kuukwamua mkoa hasa baada ya kutokea hayo majanga mengine.
 
Kama hujui historia ungeuliza kwanza kwa wanaojua kabla ya kutoa uzi.
Usahihi ni kwamba kabla ya uhuru wa Tanganyika mkoa wa Kagera ulikuwa katika Jimbo la Ziwa lenye Wilaya za Bukoba, Ngara, Biharamulo, Karagwe, Geita, Mwanza, Kwimba, Maswa, Ukerewe, Shinyanga, North Mara na South Mara na makao makuu ya Jimbo hili yalikuwa katika mji wa Mwanza.

Ilipofika mwaka 1959 Jimbo la Ziwa liligawanywa na kupata Jimbo la Ziwa Magharibi lenye Wilaya za Bukoba, Biharamulo, Ngara na Karagwe na kuifanya Tanganyika kuwa na majimbo Tisa badala ya manane yaliyokuwepo kabla ya mwaka 1959.

Tabora ilikuwa iko Jimbo la magharibi lenye wilaya za Tabora, Mpanda, Nzega, Kahama, Kigoma, Kasulu na Kibondo na makao makuu ya Jimbo hili yalikuwa mjini Tabora. Hadi kufikia mwaka 1959 Majimbo ya Tanganyika yalikuwa ni:-

Mashariki
Kusini
Nyanda za juu kusini
Kaskazini
Kati
Tanga
Ziwa
Magharibi
Ziwa Magharibi
Kiongozi soma vizuri kabla ya kuchangia, ingawa mchango wako pia ni muhimu ila hauna uhusiano na hoja ya mdau. Yeye hazungumzii historia ya mkoa wa kagera. Bali anazungumzia matukio haribufu yaliyowahi ukumba mkoa wa kagera baada ya uhuru. Na mapendekezo kuwa serikali ingefanya jambo kutokana na matukio hayo.
 
Bukoba iko overated sana ila kwangu mimi morogoro ni mkoa wa maana kuliko kagera,siku mkiacha masifa na kukubali kuwa zama zimwbadilika mtafika mbali,ile stendi ya mabasi ya mkoa au zizi la ngombe
 
Tumeshawekana sawa. Kuna mahali alisema Tabora ilikuwa Jimbo la Ziwa wakati wa ukoloni, hivyo ilibidi niweke sawa taarifa hiyo.
Kiongozi soma vizuri kabla ya kuchangia, ingawa mchango wako pia ni muhimu ila hauna uhusiano na hoja ya mdau. Yeye hazungumzii historia ya mkoa wa kagera. Bali anazungumzia matukio haribufu yaliyowahi ukumba mkoa wa kagera baada ya uhuru. Na mapendekezo kuwa serikali ingefanya jambo kutokana na matukio hayo.
 
Kiongozi soma vizuri kabla ya kuchangia, ingawa mchango wako pia ni muhimu ila hauna uhusiano na hoja ya mdau. Yeye hazungumzii historia ya mkoa wa kagera. Bali anazungumzia matukio haribufu yaliyowahi ukumba mkoa wa kagera baada ya uhuru. Na mapendekezo kuwa serikali ingefanya jambo kutokana na matukio hayo.
Uko sahihi, lakini hata yeye tulishawekana Sawa. Ni kweli lengo kuu ni kuikumbusha serikali ya kwamba ilitakiwa kuwa na mkakati madhubuti wa kuusaidia mkoa na sio kuwaachia wakazi wake wapambane wenyewe kwani mambo mengi yanahitaji mkono wa serikali.
 
Bukoba iko overated sana ila kwangu mimi morogoro ni mkoa wa maana kuliko kagera,siku mkiacha masifa na kukubali kuwa zama zimwbadilika mtafika mbali,ile stendi ya mabasi ya mkoa au zizi la ngombe
Unaweza kuwa sahihi, na umeandika kwa hisia na asira, sijuhi kwa nini.Kuhusu stendi hilo limeshajadiliwa humu mara nyingi, tafuta mada usome ujue sababu. Stendi ya msamvu kama si serikali sizani kama ungeandika kwa vijembe namna hii.
 
Unaweza kuwa sahihi, na umeandika kwa hisia na asira, sijuhi kwa nini.Kuhusu stendi hilo limeshajadiliwa humu mara nyingi, tafuta mada usome ujue sababu. Stendi ya msamvu kama si serikali sizani kama ungeandika kwa vijembe namna hii.
Mji unamezwa ule na maji .nyumba zilizokuwa mita hamsini miaka ya 70 toka ufukweni zimeshazama,majanga matupu,boresheni mji wenu mmekazania kujenga vijijini tu which is not bad ila taswira ya mkoa nimkoani.bukoba mjiñi ya mwaka 70 na hii ya leo hakuna mabadiliko huwezi kupotea,magofu tupu.
Kingine wahaya mjue siku hizi makabila yote yanajua umuhimu wa elimu so acheni egoism,kuwa nshomile nshomile
 
Mji unamezwa ule na maji .nyumba zilizokuwa mita hamsini miaka ya 70 toka ufukweni zimeshazama,majanga matupu,boresheni mji wenu mmekazania kujenga vijijini tu which is not bad ila taswira ya mkoa nimkoani.bukoba mjiñi ya mwaka 70 na hii ya leo hakuna mabadiliko huwezi kupotea,magofu tupu.
Kingine wahaya mjue siku hizi makabila yote yanajua umuhimu wa elimu so acheni egoism,kuwa nshomile nshomile
Kuhusu mji kumezwa na maji uko sahihi na hizo zote ni athari za mabadiliko ya tabia ya nchi, kujenga vijijini pia na yenyew ni maendeleo, kuhusu Bukoba mjini siasa za serikali ndiyo zinapakwamisha zaidi, mambo ya elimu sahizi yapo nchi nzima, sema nyinyi ndiyo mnazileta hizo za nshomile nshomile wenyewe kwa sasa hawana hizo egoism hila nyinyi ndiyo mnaziendeleza wenyewe ionekane kwamba ni sifa yao kuu.
 
Kwa nini serikali iingilie wakati ilifanya hivyo? Kuna nyuzi nyingi humu zinasema Kagera hailinganishwi na mkoa wowote kwa maendeleo!
 
Kwa nini serikali iingilie wakati ilifanya hivyo? Kuna nyuzi nyingi humu zinasema Kagera hailinganishwi na mkoa wowote kwa maendeleo!
Sio kweli, mkoa wa kagera bado una changamoto kadhaa kama mikoa mingine, lakini asilimia kubwa umerudishwa nyuma kimaendeleo na hayo matukio. Hivyo Serikali ilipaswa kuja na mkakati wa kuusaidia mkoa.
 
Kilichodidimiza mkoa wa Kagera ni aliyekuwa Mkuu wa mkoa enzi hizo Nsa Kahisi.Alifanya mkoa usimame kimaendeleo baada ya kutaifisha Mali za wafanyabiasharà .Bila haibu Bunge iilipitisha mswada wa kutaifisha magari yaliyokamatwa kwenye uhujumu uchumi Mkoa wa Kagera.Walianzisha kampuni ya uchukuzi ambayo haikufanya kazi kwa kufa kifo Cha mende.Kama hiyo haitoshi chama kikuu Cha Ushirika kilivunjwa na Mali zake zikapelekwa kusikojulikana. Vilevie Kahawa ilibadirishwaa na mafuta ya petrol kutoka nchi za kiarabu .Hivyo wakulima wa kahawa walikuwa wanalipwa kwa kukadiliwa.Hii iliondoa uhaba wa mafuta at the expenses of Kagera peasants
 
Kilichodidimiza mkoa wa Kagera ni aliyekuwa Mkuu wa mkoa enzi hizo Nsa Kahisi.Alifanya mkoa usimame kimaendeleo baada ya kutaifisha Mali za wafanyabiasharà .Bila haibu Bunge iilipitisha mswada wa kutaifisha magari yaliyokamatwa kwenye uhujumu uchumi Mkoa wa Kagera.Walianzisha kampuni ya uchukuzi ambayo haikufanya kazi kwa kufa kifo Cha mende.Kama hiyo haitoshi chama kikuu Cha Ushirika kilivunjwa na Mali zake zikapelekwa kusikojulikana. Vilevie Kahawa ilibadirishwaa na mafuta ya petrol kutoka nchi za kiarabu .Hivyo wakulima wa kahawa walikuwa wanalipwa kwa kukadiliwa.Hii iliondoa uhaba wa mafuta at the expenses of Kagera peasants
Uko sahihi, uliyo yaandika pia yalichangia na ndiyo serikali hiyo hiyo ilirudisha mkoa nyuma na kuutelekeza.
 
Historia ya Mkoa kabla ya Uhuru

Kabla ya Uhuru na hadi kufikia mwaka 1961, eneo la sasa la Mkoa wa Kagera, lilikuwa ni moja ya maeneo yaliounda jimbo lililoitwa “Lake Province”. Jimbo hili lilijumuisha Wilaya za Bukoba, Musoma, Shinyanga na Tabora. Baada ya uhuru mwaka 1962 mkoa ulibadilishwa jina na kuitwa ‘West Lake Region’ (Ziwa Magharibi) na kujumuisha Wilaya 4 za Ngara, Biharamuro, Karagwe na Bukoba.

Kabla ya mwaka 1979, mkoa huu wa Kagera ulikuwa unaitwa “Ziwa Magharibi”. Jina hilo lilibadilishwa na kuwa “Kagera” mwaka 1979, mara baada ya vita kati ya Tanzania na Uganda, ambapo mkoa, chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa, aliyekuwepo wakati huo, Capt. Peter Kafanabo, ulipendekeza uitwe “Kagera”. Pendekezo la kuubadlisha jina Mkoa wa Ziwa Magharibi na kuitwa Kagera lilitokana na Mto Kagera kugusa sehemu kubwa ya wilaya zote zinazounda mkoa huu ukiwa unatiririsha maji yake kutoka Rwanda kupitia kaskazini na kumwaga maji yake katika Ziwa Victoria.

MATUKIO MAKUU 1962 – 2021
Katika kipindi cha miaka sitini tangu tupate uhuru yapo matukio mengi ya kihistoria ambayo yametokea katika mkoa wa Kagera. Mtiririko wa matukio hayo ni kama yanavyoainishwa hapa chini.

Mwaka 1962
Mafuriko: Mvua kubwa ilinyesha na mafuriko kutokea sehemu kubwa ya Mkoa, ambapo wananchi waliipa jina la “Mvua ya Uhuru” kwa sababu mvua kubwa ya masika ilinyesha baada ya Tanganyika kupata Uhuru.

Mwaka 1966
Ukame: Ukame mkubwa uliodumu hadi mwaka 1970 watokea na kusababisha njaa kali katika wilaya ya Karagwe. Hali hiyo ilisababisha baadhi ya watu kupoteza maisha, kupungua kwa nguvukazi, baadhi ya familia kukosa matunzo kwa ukaribu baada ya wanaume kwenda maeneo ya mbali kutafuta chakula.

Mwaka 1978
Vita kati ya Tanzania na Uganda: Mwezi Oktoba 1978 kulitokea vita kati ya nchi ya Tanzania na nchi ya Uganda. Vita hii ilijulikana kwa jina maarufu la “vita ya Kagera” iliitwa jina hilo kutokana kwamba ilipiganiwa katika ardhi ya Tanzania mkoani Kagera.

Vita hii ilisababishwa na kitendo cha Majeshi ya Uganda, chini ya Nduli Idd Amin Dada, kuvamia ardhi ya Tanzania katika eneo la Missenyi na kudai kuwa eneo lote lililo kaskazini mwa Mto Kagera ni ardhi ya nchi ya Uganda. Vita hivyo vilimalizika mwezi April, 1979 kwa Majeshi ya Tanzania kushinda vita na kumuondoa madarakani Nduli Idd Amin.Vita hivi vya Kagera vilikuwa na athari kubwa kwa mkoa wa Kagera. Athari hizo ni pamoja na vifo, wananchi kunyang’anywa mali zao na uharibifu wa miundombinu ya majengo na barabara.

Mwaka 1983
Operesheni Uhujumu Uchumi: Kutokana na kukosekana kwa bidhaa muhimu katika jamii na kupungua kwa uwianao wa kipato kati ya walio nacho na wasio nacho serikali iliendesha operesheni dhidi ya wahujumu uchumi nchi nzima. Wafanyabiashara wa Mkoa wa Kagera walitupa bidhaa zao kwenye Ziwa Victoria na mto Ngono ili kuhofia kukamatwa na Serikali.

Kugunduliwa kwa Mgonjwa wa UKIMWI: Ugonjwa ambao unadhoofisha kinga za mwili za kujikinga na maradhi ambao baadae ulikuja kujulikana zaidi kama UKIMWI (Ukosefu wa Kinga Mwilini) uligundulika kwa mara ya kwanza nchini Tanzania mkoani Kagera.

Mgojwa wa kwanza aligundulika kuwa na virusi vya UKIMWI alitoka katika Kijijini cha Kanyigo Wilaya ya Missenyi. Mwanzoni wananchi wa Mkoa wa Kagera waliuita ugonjwa huo “Juliana” au “Slim”. Uliitwa Juliana kwa sababu iliaminika kuwa ugonjwa huo uliingizwa nchini na vijana waliokuwa wakitokea Uganda wakiwa wamevaa mashati ya Juliana. Pia uliitwa ‘slim’ kwa sababu waathirika wa ugonjwa huo walikuwa wanakonda hadi kufa. Ugonjwa huu baadae ulienea Tanzania nzima na kuleta athari kubwa katika jamii. Mkoa wa Kagera ulikuwa wa kwanza kuathirika. Ugonjwa huu uliwakumba zaidi vijana, wanajamii ambao wanaotegemewa sana katika uzalishaji mali. Vijana wengi wakaangamia kwa UKIMWI na kufanya familia nyingi kubaki na wazee wakibeba mzigo wa kutunza watoto yatima. Pia muda mwingi wa kuzalisha mali ulipotea katika kuhudhuria mazishi na matanga ya ndugu na jamaa, kuuguza wagonjwa na kutunza yatima. Ugonjwa wa UKIMWI bado upo mpaka sasa katika mkoa wa Kagera na Tanzania kwa ujumla.

Mwaka 1994
Kuingia kwa Wakimbizi wa Rwanda na Burundi: Kutokana na mapigano ya kikabila nchini Burundi na mauaji ya kimbari nchini Rwanda, inakadiriwa kuwa Wanyarandwa na Warundi laki sita (600,000) waliingia mkoani Kagera wakikimbia mapigano hayo. Ujio wa wakimbizi ulisababisha madhara makubwa kwa mkoa wa Kagera
yakiwemo uharibifu wa mazingira na kushamili kwa uhalifu mwingiliano wa utamaduni na kuzaliana.

Mwaka 1995
Mvua kubwa: Mvua kubwa ilinyesha na kusababisha mafuriko na uharibifu wa mazao na miundombinu.Mafurikoyaliathiri sana Wilaya yote ya Bukoba na Missenyi. Madaraja yalisombwa na maji hivyo kuathiri watumiaji na baadhi ya nyumba za watu ziliharibiwa.

Mwaka 1996
Kuzama kwa MV Bukoba: MV Bukoba ikiwa safirini kutoka Bukoba kwenda Mwanza, ilizama katika Ziwa Victoria kilomita nane kabla ya kufika bandari ya Mwanza. Inakadiriwa kuwa watu mia nane (800), wengi wao walikuwa wakazi wa mkoa wa Kagera, walipoteza maisha huku mali yenye thamani ya mamilioni ya shilingi ilipotea. Sababu za kuzama kwa meli hiyo kulisababishwa na ujazaji wa abiria na miziko kupita uwezo wake.

Mwaka 2016
12 Septemba 2016
Tetemeko la ardhi la nguvu ya 5.7 katika vipimo vya Richter lilitokea eneo la Bukoba, kaskazini magharibi mwa Tanzania na kusababisha maafa.

Kitovu cha tetemeko hilo kilikuwa takriban kilomita 44 kutoka mji wa Bukoba, ambao ni mji mkuu wa mkoa wa Kagera, kwa mujibu wa taasisi ya jiolojia ya Marekani.Nyumba nyingi ziliporomoka na kuwaacha mamia ya watu wakiwa bila makao.Tetemeko hilo ndilo mbaya zaidi kukumba Tanzania katika kipindi cha zaidi ya mwongo mmoja.

Kwahiyo badala ya serikali kuendelea kuugawa mkoa wa Kagera, ni vyema ingekuja na mpango wa maendeleo katika mkoa yaani "Special Economic Rehabilitation program" ili kuchochea maendeleo zaidi katika mkoa huu unao kwamishwa na majanga zaidi licha ya wakazi wake kujitahidi kujikwamua kiuchumi.
Watu wenye ubinafsi utawajua tu,sasa mkoa ukigawanywa mnampungukiwa nini,utafikiri mkoa unahamia Rwanda
 
Back
Top Bottom