Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,498
- 51,092
Baada ya Dkt. Magufuli kupita mkoani Kigoma na kumwaga sera zake.
Kisha kesho yake akafuatia Lissu aliyekwenda kung'oa magugu na kupanda ngano yake
Siku iliyofuata, Ikawa ni zamu ya Zitto kupita Kigoma na kung'oang'oa magugu zaidi na kwa kufanya hivyo indirectly akapalilia ngano iliyopandwa na Lissu
Kama sote tujuavyo, uwezo wa Zitto wa kuzungumza kwa Takwimu na mifano, Zitto akaivunjavunja hoja ya Magufuli kuwa anawapenda wana Kigoma ndiyo maana akateua wabunge watatu wa mkoa huo akiwemo waziri Mpango
Zitto akatoa mifano iliyohai jinsi waziri Mpango "mtoto wa nyumbani" "alivyoshindwa kuwa msaada kwa mkoa wake hata kwa vitu vilivyo obvious kabisa visivyohitaji upendeleo wowote.
Zitto akaeleza kuhusu miradi na fedha za msaada zilizokusudiwa makhsusi kwa mkoa wa Kigoma na jinsi waziri huyo alivyoitosa Kigoma kwa kutokutoa ushirikiano.
Kwa nondo hizi za Zitto, ni dhahiri Zitto anafanya kazi ya safisafisha inayoenda kumnyang'anya Magufuli mkoa huo ambao ni kete muhimu sana kwenye uchaguzi huu na pia inaonekana ni dhahiri Magufuli ameonyesha makusudio ya kuutwaa kwenye uchaguzi huu ndiyo maana kaweka nguvu kubwa sana ya kampeni katika mkoa huo.
Kwa hii kazi ambayo Zitto kapiga huko Kigoma, ni dhahiri Juhudi ya Magufuli katika mkoa huo imepotea bure, Zitto anamdelete Magufuli kutoka katika mkoa huo kwa nondo kali bila huruma!
Kwa video cheki hapa chini
Kisha kesho yake akafuatia Lissu aliyekwenda kung'oa magugu na kupanda ngano yake
Siku iliyofuata, Ikawa ni zamu ya Zitto kupita Kigoma na kung'oang'oa magugu zaidi na kwa kufanya hivyo indirectly akapalilia ngano iliyopandwa na Lissu
Kama sote tujuavyo, uwezo wa Zitto wa kuzungumza kwa Takwimu na mifano, Zitto akaivunjavunja hoja ya Magufuli kuwa anawapenda wana Kigoma ndiyo maana akateua wabunge watatu wa mkoa huo akiwemo waziri Mpango
Zitto akatoa mifano iliyohai jinsi waziri Mpango "mtoto wa nyumbani" "alivyoshindwa kuwa msaada kwa mkoa wake hata kwa vitu vilivyo obvious kabisa visivyohitaji upendeleo wowote.
Zitto akaeleza kuhusu miradi na fedha za msaada zilizokusudiwa makhsusi kwa mkoa wa Kigoma na jinsi waziri huyo alivyoitosa Kigoma kwa kutokutoa ushirikiano.
Kwa nondo hizi za Zitto, ni dhahiri Zitto anafanya kazi ya safisafisha inayoenda kumnyang'anya Magufuli mkoa huo ambao ni kete muhimu sana kwenye uchaguzi huu na pia inaonekana ni dhahiri Magufuli ameonyesha makusudio ya kuutwaa kwenye uchaguzi huu ndiyo maana kaweka nguvu kubwa sana ya kampeni katika mkoa huo.
Kwa hii kazi ambayo Zitto kapiga huko Kigoma, ni dhahiri Juhudi ya Magufuli katika mkoa huo imepotea bure, Zitto anamdelete Magufuli kutoka katika mkoa huo kwa nondo kali bila huruma!
Kwa video cheki hapa chini