Baada ya Kutuibiwa Kupitia Richmond &Dowons Sasa Wamegeukia Makanisa Kutaka Utawala 2015

KING COBRA

JF-Expert Member
Nov 10, 2011
2,782
864
Ni Dhahili kuwa Mkataba wa Richmond na Dowons Umehujumu Uchumi wa Nchi na Mpka sasa Hali ni tete na Umezua mpasuko mkubwa Katika Taifa!!

Hapo mwanzo ilikuwa siri kubwa sana kuhusu mumiliki wa Richmond na Yule wa Dowons kiasi cha watu wengi kusema ni Edward Lowassa kwa kuwa alijiuzulu kutokana na Kashifa hiyo!!

Lakini zaidi sana Rais Kikwete aliuambia umma kuwa Hawajui Dowons wala mumiliki wake !!!
Jambo la Kushangaza Kwenye Kikao Cha NEC DODOMA Edward Lowassa baada ya Kupata Ujasili akasema Richmondi ni ya Kikwete na Kwamba hata Dowons ilitokana na yeye Lowassa kumupendekeza Rostamu Kwa Kikwete!!!

Sasa hapa naona Lowassa kajivua Gamba na baada ya Hapo amekimbilia Makanisani kuwambia wachnguaji kuwa yeye Lowassa hahusiki na Richmond wala Dowons na katika mkakati huo anachangisha pesa kuimarisha makanisa hayo huku akitoa angalizo la kugombea 2015!!!

Makanisa mengi sasa yana acha ibada na kupanga miariko mingi ya Lowassa kwa ajiri ya michango , mimi nawataka wanasiasa mwogopeni Mungu kwani hapo munahujumu Makanisa kwani Ibada zina kwama na neno la Mungu linachakachuliwa!!!

Ni kweli tumeingia hasara kubwa kutokana na Richmond lakini sasa acheni Maknisa yawe Huru musihujumu makanisa
mini naungana na mwenye Blong Nova Kambota hii hapa chini:

[h=2][/h]
Tafakuri Yangu Ya Leo: Ya Kakobe na TANESCO mwogopeni Mungu tujaribu kwa Mafisadi




KAMA kuna jambo linalowakera watanzania basi ni hili la Ufisadi miongoni mwa baadhi ya viongozi wetu. Watanzania wanajiuliza, iweje wao waendelee kuwa masikini ilihali wachache wanazidi kuneemeka huku wakikodi ndege kwenda kutumbuliwa vipele huko Berlin Ujerumani? Sasa mimi nina pendekezo binafsi mkiona linafaa tulifanyie kazi wadau.

Hivi mnakumbuka enzi zile za mgogoro kati ya Askofu Zakaria Kakobe na TANESCO? , Kakobe aliendesha harakati zisizo na umwagaji damu akazipachika jina la “TANESCO Mwogopeni Mungu !!” na fulana za njano alichapa tunazikumbuka, Sasa kwa nini na sisi tusitumie mbinu hii kuwashughulikia Mafisadi?

Na hii iwe Tafakuri yangu ya leo jamani……

Nova Kambota Mwanaharakati
“Kitendawili sio deni ukishindwa nipe mji”
0717-709618 au 0766-730256
novakambota@gmail.com
novadream.blog.com
10 Machi 2011
Njombe , Tanzania.
 
Back
Top Bottom