Baada ya Kutoswa Uwaziri: Shamsi aungana na wazanzibari wanaotaka Mamlaka Kamili ya nchi yao...

Zanzibar ni koloni la Tanganyika, nani anabisha tunawatawala kisiasa, uchumi na kijamii
 
Dis iz 2 much kila kiongozi akinyang'anywa madaraka utackia kaanza kuxema mambo ya watu kama anataka nae pia arudi na waznzbar wenzake huko huko muungano kitu gan kama watu wanazaliwa wameungana den wanaachanishwa xo let leave them alone
 
We give them every thing but it seem's they don't deserve our help lets leave them and see what they will do without us
 
Huwezi kuwa na mamlaka kamili halafu usiwe nayo wakati huo huo kuhusiana na kitu hicho hicho! Ni sawasawa na kutaka kuwa uko kwenye ndoa na uwe single at the same time... u can't.

Some people want to eat their cake and still have it.

Penye maslahi wanataka mamlaka kamili, penye gharama hawataki.

Mamlaka ni gharama, huwezi kutaka mamlaka halafu ukwepe gharama.Utakuwa kama mtoto mdogo anayetaka heshima ya ukubwa bila kukubali wajibu wa kufanya kazi wa mkubwa.

Hawa watu hawana hata falsafa ya kujadilika. Kuna watu unaweza kuwasikiliza wakiongelea the dangers of Balkanization (Nyerere kwa mfano) ukajua huyu anasimamia wapi philosophically. Huyu Shamsi hata ukimuuliza falsafa yake ni nini zaidi ya the banal opportunism na undumilakuwili hawezi kukuambia anasimamia falsafa gani. Kwa sababu ni habari za opportunism za siasa za bendera kufuata upepo na crowd pleasing common low denominator hokum.
 
sasa huyu ndo anaongea nini anataka mamlaka kamili halfu still nataka muungano uendelee na sarafu moja iendelee kutumika,hata haeleweki msimamo wake ni upi?,thats naendelea kuamini viongiozi wa afrika wanaopigania maslahi halisi ya wananchi wao bila ya kuweka matumbo yao mbele ni wachache sana.
 
Mnafiki sana tena bora kaondolewa angeweza kulishawishi jeshi vibaya, na bado tutasikia mengi subirini

hakuna ambae angemsikiliza cheo chenyewe alipewa baada ya mdomo mdom wake wa kutaka uraisi wa zenji lle ilikuwa analipwa fadhila tu na kunyamazishwa kama alvyofanyiwa k.bilal
 
Hapana hawajalazimisshwa. Wanakuja katika bunge Dodoma wenyewe tena wanachukua na pesa 'haramu' za mkoloni Tanganyika.

Wanachagua makamu wa rais kwasababu ya uzanzibar na walishawahi kutupatia rais mzanzibar. Hakuna aliyewashikia kiboko hata siku moja.

Wana baraza lao la wawakilishi, wanapitisha miswada kama wa kuondoa mafuta na gesi, kuweka mipaka ya nchi yao, kuwa na wimbo wa taifa na bendera yao. Walichoshindwa kufanya ni mswada wa kuvunja muungano, huo hawajawahi kuandika hata siku moja.

Wameleta wajumbe wa tume ya Warioba tena wakidai nusu kwa nusu. Tume ya Warioba inaandaa rasimu ya katiba ya Tanzania. Kama hawataki muungano wasingeleta wajumbe.

Hawajawahi kuapeleka mswada wa kura ya maoni BLW au kwa rais wao. Kama wangetaka wangeshafanya hivyo.

Bunge la katiba linaandaliwa. Wanachotakiwa ni kutokuja hapo watakuwa na nchi yao. Hakuna atakayefungwa jela kwa kutokuja. Wao wanadai waongezewe wajumbe zaidi! Alah, hawataki muungano halafu wanataka wajumbe zaidi wa kitu gani?

Hawajalazimishwa kwasababu katika muungano uliopo wao ndio wafadika. Labda uniambie Mtanganyika anafaidika nini hasa kiasi cha wewe kudhani wanang'ang'aniwa?

Sasa kwanini mara zote waznz ndiyo mara nyingi hudai kutaka kujitenga? na kwanini kusiwe na serikali moja tu?
 
..Njaa inaumaaa..kula usichinje nyau...kweli SIASA ni Fani,ku#*@?+£ wallah!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ila tujiulize haya malalamiko ya wazanzibari na watanganyika yatamalizwa vp?tusijidanganye kwamba hakuna hasara kwenye hili.
 
Yupo sahihi. Wazanzibari hawana woga wa kutaka nchi yao huru kama walivyo baadhi ya viongozi wa Tanganyika. Wao wanaona kuwa kuwepo kwa Tanganyika ni kama kifo chao hivyo wanaiogopa kama ukoma! Washindwe na wanyong'onyeeee!
 
Ukiona hivyo si yeye tu kuna Wazanzibar wengi waliona nafasi kwenye serikali ya muungano wana mtizamo kama yeye aliyesema hayo. Wazanzibar walio na vyeo hawawezi kusema wazi ila likitokea la kutokea kama kwa huyu ndg yetu ndo utaona true color ya wazanzibar. Tukae nao kwa akiri maana hawaeleweki na hawako wawazi siku zote.
 
Hivi jamani HAWA wazanzibar wasijitegemee kabisa wakatupunguzia mzigo. Tunahitaji kura ya maoni haraka kuhusu muungano.
 
Shamsi Nahodha hatutaki porojo zako maana hujui unakisema nini Wala unataka nini. WaZanzibari na WaTanzania MPUUZENI maana hafai hata kuwa messenger Katika Afisi ya mtu binafsi seuze ya Serikali
 
Tatizo la viongozi wetu wakiwa madarakani wanatetea kilakitu hata kama hakina maslahi!, hayo mambo angeyasema hapo kabla kweye baraza la mawaziri la muungano amekaa miaka 8, siyo leo kisa ametoswa ulaji ajifanya Zanzibar yenye mamlaka kwani kwasas hawana? kwani Tanganyika inaitawala Zanzibar? Wajitenge waone watakuwa kama Sudani Kusini kwasasa wanajifanya eti matatizo yetu kati ya waunguja na wapemba hayapo ni waongo tu hawa tuombe uzima tutawasikia tu.

Friday, December 27, 2013





Waziri Mstaafu wa Ulinzi na Jeshi la kujenga taifa, Mhe Shamsi Vuai Nahodha alipokuwa akizungumza na WanaCCM kwenye jengo la Makao Makuu ya CCM Mkoa wa Mjini Magharibi Amani jana.


Mwakilishi wa jimbo la Mwanakwerekwe Shamsi Vuai Nahodha amesena anaungana na kundi la wazanzibar wanaotaka Zanzibar kuwa na mamlaka kamili ndani ya katiba ijayo ya jamhuri ya muungano Tanzania.

Akizungumza na wanachama na viongozi katika ofisi za CCM mkoa wa mjini kichama amesema katika baadhi ya maeneo ya kuendesha nchi suala la mamlaka kamili ni muhimu kuimarisha uchumi wa Zanzibar.

Nahodha aliewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani na waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa amedai yeye ni mtetezi wa suala la mafuta na gesi liondolewe kwenye muungano.


Hata hivyo amesema anashangazwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanaodai sarafu ya Zanzibar, kiti cha umoja wa mataifa na wizara ya ulinzi akidai masuala hayo yanahitaji gharama kubwa za uendeshaji.

Aidha Nahodha amesema wakati Zanzibar ikiendelea kuadhimisha miaka 50 ya Mapinduziu Zanzibar muungano utaendelea kubaki uti wa mgongo wa maendeleo ya ulinzi na usalama wake.

Amesema licha ya mfumbo wa muungano wa serikali mbili kujaa matatizo, lakini njia ya kuyapatia ufumbuzi ziko huru badala ya kun'gan'gania muungano wa mkataba au serikali tatu akidai haiku salama na Zanzibar


Chanzo: Zanzibar Islamic news blog
 
Back
Top Bottom