Baada ya kutangazwa kifo cha J.K. Nyerere mwaka 1999, ulifanya nini (first reaction)?

Kifo cha Nyerere kilileta na kukata disco mwezi mzima
na TV zilikuwa hazitangazi chochote kingine zaidi ya msiba
kifo cha Nyerere kinamna fulani ndo 'kilianzisha' bongo fleva

watu waliboreka mno na nyimbo za huzzuni ikawa ruhusa kwa kila msaniikutunga nyimbo yake kwenda kwenye tv na redio

ndo kina Jaydee wakaibukia pia...na wengine....

kabla ya hapo hakukuwa na nguvu sana kwa mziki wa bongo fleva...

binafsi walinifurahisha Club Bilicanas.....wao walijifanya kuna 'Tamasha la kumkumbuka baba wa Taifa'
hapo ikawa fursa ya watu kula debe siku hiyo baada ya kukosa burudani karibu mwezi mzima....

mimi nilipata mateso ya kuikosa CNN kupitia CTN kwa mwezi mzima

The Boss nakumbuka kuna watu walikuwa wanasema nchi ndio itavamiwa baada ya mzee kufa, basi watoto wengi walikuwa wanaogopa muda wote wapo na mama zao....
 
Nilishapata habari ya kifo chake kabla hakijatangazwa rasmi.

Na kabla ya kifo chake hatukutegemea kama atarudi mzima kwani tulishasikia tetesi kuwa ana ukosefu wa kinga mwilini kwa kusumbuliwa na kansa ya damu aka leukemia.

Hakuna cha zaidi ila nilisema Inna li Llahi wa Inna Ilayhi Rajiun.


Ni kweli Samia ametaka ku quit?
 
Mimi wakati huo nilikuwa darasa la sita, tunaishi Musoma na Mzee alikuwa mjeshi hapo Butiama kipindi hicho, tulifurah sana kufunga shule nilikaa msibani mpak watu wote wakatawanyika ni kula na kucheza. Umenikumbusha mbali sana mkuu.
teh teh teh
 
nilisikia tu kwa watu ila sikutaka kujua kinachoendelea hata tv nilikuwa naangalia mda kwa kipindi cha cartoon kikianza.... nilimuwa bado mdogo.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom