KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,589
- 4,599
Baada ya uchaguzi mkuu wa 2015 uliomfanya Rais Magufuli kuwa Rais wa JMT, katika anga la siasa za Tanzania kulizuka jinamizi upande wa vyama vya upinzani la kupinga, kubeza na kulaumu kila kitu. Ukweli ni kwamba jinamizi hilo lilikuwepo tangu kuzaliwa kwa vyama hivyo lakini kwa kuwa linakua, kipindi hiki cha Rais Magufuli limekomaa sana.
Jinamizi hilo limeleta vibweka na vitimbwi kedekede katika jitihada mbalimbali za serikali yetu katika kuwaletea wananchi maendeleo na maendeleo yamekuwa yakichelewa kwa sababu yao. Inasakitisha sana kuona kuna baadhi ya watu wanapinga yale waliyokuwa wanayahubiri, Rushwa na ufisadi vimekuwa ni vitu vya kushangiliwa na kuchekewa na vyama vya upinzani, hakuna wa kuvikemea wala kuvipinga lakini wa kupinga maendeleo wapo wengi. Kwa nini upinzani umegeuka mzigo badala ya tegemeo la wananchi?
Vijana ambao jana tulipokuwa watoto tulisema ni taifa la kesho, wamejikita katika upotoshaji wenye nia na dhumuni ovu, Wanahubiri uongo majukwani, magazetini na mitandaoni ili kuendeleza vitimbwi na vibweka vyao. Siasa za vitimbwi za upinzani zimefanya vijana kujiona katika mizania sawa na wanazuoni na wazee katika kutafakari na kufikiri mambo kwa kina, busara na hekima. Unakuta kuna kijana wa miaka 22-25 ambaye kasomea uongozi wa umma au sayansi lakini kwa kujikweza anajiweka katika mizania sawa na profesa wa sheria katika masuala ya kisheria, hayo ni matokeo ya siasa za upinzani kuharibu kizazi hiki cha vijana.
Miezi miwili baadaye tutashiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa ambao vijana kama hawa watashiriki katika uchaguzi kwa dhumuni la kuchaguliwa ili kuendeleleza uharibu Zaidi. Taifa letu tunalipenda na tunapenda kuona hatima njema ya taifa letu bila kujali nani kachaguliwa kwenye nini na katokea chama kipi lakini kwa muelekeo na vitimbwi vya upinzani huu lazima tuseme hautufai. Gharama ya kukosea kuchagua ni miaka 5 ya vitimbwi, vibweka, maumivu, mateso na kukosa maendeleo
Vijana ni tegemeo la leo na kesho katika taifa lolote na hatima ya taifa lolote ni maamuzi ya vijana hivyo sisi vijana tuutumie uchaguzi wa serikali za mitaa tukitafakari nia na dhumuni la upinzani na mwisho wa kutafakari tuukatae upinzani wa namna kama njia ya kupiga hatua na kusonga mbele Zaidi.
Jinamizi hilo limeleta vibweka na vitimbwi kedekede katika jitihada mbalimbali za serikali yetu katika kuwaletea wananchi maendeleo na maendeleo yamekuwa yakichelewa kwa sababu yao. Inasakitisha sana kuona kuna baadhi ya watu wanapinga yale waliyokuwa wanayahubiri, Rushwa na ufisadi vimekuwa ni vitu vya kushangiliwa na kuchekewa na vyama vya upinzani, hakuna wa kuvikemea wala kuvipinga lakini wa kupinga maendeleo wapo wengi. Kwa nini upinzani umegeuka mzigo badala ya tegemeo la wananchi?
Vijana ambao jana tulipokuwa watoto tulisema ni taifa la kesho, wamejikita katika upotoshaji wenye nia na dhumuni ovu, Wanahubiri uongo majukwani, magazetini na mitandaoni ili kuendeleza vitimbwi na vibweka vyao. Siasa za vitimbwi za upinzani zimefanya vijana kujiona katika mizania sawa na wanazuoni na wazee katika kutafakari na kufikiri mambo kwa kina, busara na hekima. Unakuta kuna kijana wa miaka 22-25 ambaye kasomea uongozi wa umma au sayansi lakini kwa kujikweza anajiweka katika mizania sawa na profesa wa sheria katika masuala ya kisheria, hayo ni matokeo ya siasa za upinzani kuharibu kizazi hiki cha vijana.
Miezi miwili baadaye tutashiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa ambao vijana kama hawa watashiriki katika uchaguzi kwa dhumuni la kuchaguliwa ili kuendeleleza uharibu Zaidi. Taifa letu tunalipenda na tunapenda kuona hatima njema ya taifa letu bila kujali nani kachaguliwa kwenye nini na katokea chama kipi lakini kwa muelekeo na vitimbwi vya upinzani huu lazima tuseme hautufai. Gharama ya kukosea kuchagua ni miaka 5 ya vitimbwi, vibweka, maumivu, mateso na kukosa maendeleo
Vijana ni tegemeo la leo na kesho katika taifa lolote na hatima ya taifa lolote ni maamuzi ya vijana hivyo sisi vijana tuutumie uchaguzi wa serikali za mitaa tukitafakari nia na dhumuni la upinzani na mwisho wa kutafakari tuukatae upinzani wa namna kama njia ya kupiga hatua na kusonga mbele Zaidi.