Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,011
- 144,371
Kwa jinsi alivyo-handle issue ya kijana yule wa Koromije kipindi kile, inaonyesha ni mtu asiekubali kushindwa au kusema akae kimya jambo lipite hasa iwapo ana taarifa au ushahidi wa kutosha kuhusu jambo husika.
Kwa msingi huo, kama kuna figisu zilifanyika kumbeba mtoto wa dada,basi nina uhakika wa asilimia 80 Mchungaji kufunguka walau kimafumbo mbele ya waumini wake Jumapili ijayo kueleza kilichotokea lengo ni kujaribu kulinda heshima yake mbele ya waumini wake.
Nasema haya kwasababu mtu huyu namuona hana uvumilivu wa kukaa kimya, na zaidi anaamini yeye si mtu wa kushindwa; hivyo, ni lazima atasema tu unless ameshindwa kihalali, ingawa hata akishindwa kihalali, bado anaweza kutumia maandiko kuhalalisha kushindwa kwake.
Tusubiri mahubiri yake ya Jumapili huenda itakuwa fursa nzuri ya kuju nini kilijiri katika mchujo wa leo.
Kama siyo Mchungaji kuanika kilichotokea, basi hata huyu mwenzetu wa hapa JF ambae nae kaangukia pua, anaweza kuja kutujuza kilichotokea japo kwa lugha ya mafumbo.
Kwa msingi huo, kama kuna figisu zilifanyika kumbeba mtoto wa dada,basi nina uhakika wa asilimia 80 Mchungaji kufunguka walau kimafumbo mbele ya waumini wake Jumapili ijayo kueleza kilichotokea lengo ni kujaribu kulinda heshima yake mbele ya waumini wake.
Nasema haya kwasababu mtu huyu namuona hana uvumilivu wa kukaa kimya, na zaidi anaamini yeye si mtu wa kushindwa; hivyo, ni lazima atasema tu unless ameshindwa kihalali, ingawa hata akishindwa kihalali, bado anaweza kutumia maandiko kuhalalisha kushindwa kwake.
Tusubiri mahubiri yake ya Jumapili huenda itakuwa fursa nzuri ya kuju nini kilijiri katika mchujo wa leo.
Kama siyo Mchungaji kuanika kilichotokea, basi hata huyu mwenzetu wa hapa JF ambae nae kaangukia pua, anaweza kuja kutujuza kilichotokea japo kwa lugha ya mafumbo.