Baada ya kushindwa kulipa mikopo ya wanafunzi, sasa serikali haina hela ya kulipa mishahara

Lukolo

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
5,143
3,196
Tayari baadhi ya taasisi zimeanza kuwaandikia barua wafanyakazi wao kuwajulisha juu ya kuchelewa kwa mishahara ya mwezi wa tano. Katika barua hizo inaelezwa kwamba hazina ipo kimya kabisa kuhusiana na suala la mishahara. Hata pale walipofuatiliwa, waligoma kuzungumzia suala la mishahara ya mwezi huu. Haijulikani, kama itachelewa tu au haitakuwepo kabisa kama ambavyo inatokea kwenye mikopo ya wanafunzi.
 
Serikali sikivu sana hii....wana pesa kusafirisha watalii tu ila si wajenga nchi!!!Ikulu si mahala pa kukimbilia!!!
 
Ndio Maisha bora kwa kila mtanzania,Mbona president anapata hela za kwenda nje tu?mambo ya maendeleo no money Kweli kazzi kweli kweli.
 
Nashangaa hata sie huku bado kimya hata nikijaribu kucheki bado inasomeka NIL
 
Inatia hasira halafu inakera. Tayari kamati za bunge zinaleta record kwamba wanafunzi vyuoni wanajiuza kutokana na kucheleweshewa mikopo, jambo linalohatarisha usalama wa ndugu zetu waliopo huko. Inavyoelekea hadi leo baadhi ya vyuo hawajapata mikopo yao. Ina maana serikali inasubiri makusanyo ya TRA ya mwisho wa mwezi? Hivi kweli ndivyo serikali inavyopaswa kuendeshwa. Naona tusharudi kwenye enzi za Mwinyi. Lakini nashangaa sana, ina maana Kikwete hawezi hata kujiuliza kwa mwenzie Mkapa. Mbona hatukuaona haya wakati wa Mkapa jamani?
 
Nashangaa hata sie huku bado kimya hata nikijaribu kucheki bado inasomeka NIL
Pole, nafikiri utasubiri sana. Si ajabu mkilipwa tarehe 40, baada ya mahesabu ya TRA kufungwa.
 
Nchi hii kuna mizaha mingine inazidi. Inapofika mahali unagusa mshahara wa mtu duuuuuuuuuuuuu napita tu? Wafanyakazi hawaruhusiwi kupanga matumizi au?
 
Mi nashindwa kuwaelewa magamba na serikali yao. Makusanyo ya kodi yameongezeka ukilinganisha na kipindi cha nyuma lakini maisha ndo yamekuwa tite kuliko wakati wowote! Dawa yenu ipo jikoni.... Pambfuu!
 
Na wewe ni mfanyakazi wa Serikali?

Hata kama si mfanyakazi wa serikali, jua mishahara inaleta mafao si kwa walioipokea tu maana wao watanunua bidhaa kutoka kwa wengine. Kwa hiyo kucheza na maisha ya watu kwa kuchelewesha mishahara ni pamoja na wafanyakazi hao kushindwa kujikimu kwa kununua kwa wengine
 
sasa kama Ndulu anadai BOT haijafilisika na midola ipo ya kumwaga iweje watuambie hakuna hela?
kiruuuuu ntaua mtu aisee wasishesee na maisha ya watua rifu
 
Back
Top Bottom