Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Wakati mchakato wa kampeni ukipamba moto huko Igunga, yalitokea maafa ya nyumba kadhaa kuezuliwa eneo la mbagala na kusababisha wananchi zaidi ya 600 kukosa makazi, wengine kujeruhiwa na kukosa huduma nyinginezo za kibinadamu.
Kufuatia kinyang'anyiro hicho cha ubunge jimbo la Igunga na serikali yote kuhamia huko, hatimaye ccm imeweza kutangazwa mshindi.
Nawaomba wana ccm pamoja na viongozi wa serikali, baada ya kutoka igunga, ile huruma mliyoionyesha kwa watu wa Igunga muielekeze kwa wananchi wa mbagala. Tunafahamu jinsi mlivyokuwa wakarimu kwa kugawa vyakula kama mahindi, sukari na fedha ambayo ni posho kwa ajili ya wanaigunga kujikimu kutokana na uhaba wa chakula unaowakabili.
Wananchi wale wa mbagala nyumba zao zimeharibika vibaya/zimebomoka kwahiyo hawana mahali pa kulala, hawana chakula na hawana huduma nyingine muhimu za kibinadamu. Sasa ni muda muafaka kuwakumbuka na kuwakirimu kwa kuwa ccm ni wakarimu kwa wananchi wake.
Karibuni mbagala.
Kufuatia kinyang'anyiro hicho cha ubunge jimbo la Igunga na serikali yote kuhamia huko, hatimaye ccm imeweza kutangazwa mshindi.
Nawaomba wana ccm pamoja na viongozi wa serikali, baada ya kutoka igunga, ile huruma mliyoionyesha kwa watu wa Igunga muielekeze kwa wananchi wa mbagala. Tunafahamu jinsi mlivyokuwa wakarimu kwa kugawa vyakula kama mahindi, sukari na fedha ambayo ni posho kwa ajili ya wanaigunga kujikimu kutokana na uhaba wa chakula unaowakabili.
Wananchi wale wa mbagala nyumba zao zimeharibika vibaya/zimebomoka kwahiyo hawana mahali pa kulala, hawana chakula na hawana huduma nyingine muhimu za kibinadamu. Sasa ni muda muafaka kuwakumbuka na kuwakirimu kwa kuwa ccm ni wakarimu kwa wananchi wake.
Karibuni mbagala.