Baada ya Kurudishwa Kutoka Marekani.

Kaldinali

JF-Expert Member
May 25, 2012
263
144
Nilipata bahati ya kwenda kusoma Marekani mwaka 2000. Kuna jamaa kama 6 walinipokea na tukaishi wote vizuri sana. Nilipomaliza masomo nikarudi nyumbani nikapata kazi na sasa nnaendelea vizuri sana na maisha. Jamaa wawili kati ya wale 6 walionipokea walirudishwa Tanzania. Kwa bahati mbaya hawa jamaa hawakusoma kule marekani. Tulipokuwa kule tulikuwa na maisha sawa tu kwakuwa kule kila mtu anaweza kupata kazi kirahisi. Sasa wamerudishwa nyumbani hawa mabwana wanahangaika sana. Hawana kazi na hawawezi kupata kazi. Hawakujiwekea akiba hivyo hawawezi kuwa wafanyabiashara. Inatia huruma watu wazima kama hawa kurudi na kuja kuishi kwa wazazi wao wakiwa jobless. Wakati tunashirikiana na kufanya kazi kwa pamoja kujaribu kuondokana na uozo wa chama cha mapinduzi ili kuikomboa nchi yetu, ni muhimu juhudi hizo ziende sambamba na jitihada za kujikomboa kibinafi.

Ninapoongelea ukombozi binafsi nna maanisha ni muhimu kujiandaa vizuri kwaajili ya ushindani binafsi unaoendelea katika jamii. Katika vyama tutapa ukombozi wa kitaifa. Ila wakati huo huo kila mtu binafsi anapaswa kufanya kazi kwa bidii kujiandaa au kujiendeleza yeye binafsi na familia yake.


Kama wewe ni mtu mwenye miaka kati ya 30 mpaka 45 na haujasoma na kuwa na degree na diploma utakuwa unakosea. Binadamu tumepewa nafasi ya kuishi duniani mara moja tu. Swali ni jeje wewe unataka kuishi maisha ya aina gain katika jamii. Jamii yetu imegawanyika kati ya walionacho na wasionacho na kwakiasi kikubwa tufauti yao imeletwa na ELIMU. Asilimia kubwa ya walionacho ni watu waliosoma vizuri na kupata kazi inayoyawezesha kumudu maisha, kuwa na hakiba, kuwa na vitega uchumi na hatimae kuwa na utajiri. Kama na wewe umechagua kuishi maisha mazuri katika miaka yako hii michache hapa duniani (your only one life) ni lazima usome vizuri ili uweze kuvuka kutoka katika tabaka la wasionacho na kwenda kwenye tabaka la walionacho. Kuna njia nyingi ya kuweza kuvuka daraja hilo ila njia ya uhakika kuliko zote ni ELIMU.
 
Wewe ni mtu wa ajabu sana. Kama wewe ulitaka kurudi nyumbani ni wewe. Wao pengine walitaka kubaki na kujiendeleza. Hatuwezi wote tukawa sawa. Kusoma na kumaliza, kupata kazi sio wote wameweza jwenda kwenye hio series.
Wapo waliosoma US hawapati kazi huko na sio chaguo lao kurudi nyumbani.
Narudia tena, kama wewe umejinyookea mshukuru Mungu wako. Na sio kuwabeza na kuwadharau wenzako.
Hujui nini Mungu amewaandikia, soon or later watafanikiwa na watakuacha wewe hapo unajifanya ndo umeshapatia maisha.
Maisha ni pata potea ndugu. Chunga mdomo wako.
 
Ndugu yangu elimu sio kila kitu ni ujanja tu wa mujini. Nenda kariakoo uone wakinga walivyo na hela. Waneishia la saba wale. Nna jamaa yangu aliishia la saba sasa hivi ameoa, ana watoto, ana nyumba nzuri, ana gari na hela kibao kwenye mzunguko. Mi niliyejifanya nna akili ya kufika mpaka chuo sioni matumaini yoyote zaidi ya kuona watu wakipunguza umri kila leo. Tena nikikutana naye ananitania, we uliyepotea njia njoo nikunyweshe bia. Maisha haya ni kujipanga namna ya kutafuta na sio kutegemea njia moja tu. Unatakiwa uchezeshe akili kote kote.
 
Nilipata bahati ya kwenda kusoma Marekani mwaka 2000. Kuna jamaa kama 6 walinipokea na tukaishi wote vizuri sana. Nilipomaliza masomo nikarudi nyumbani nikapata kazi na sasa nnaendelea vizuri sana na maisha. Jamaa wawili kati ya wale 6 walionipokea walirudishwa Tanzania. Kwa bahati mbaya hawa jamaa hawakusoma kule marekani. Tulipokuwa kule tulikuwa na maisha sawa tu kwakuwa kule kila mtu anaweza kupata kazi kirahisi. Sasa wamerudishwa nyumbani hawa mabwana wanahangaika sana. Hawana kazi na hawawezi kupata kazi. Hawakujiwekea akiba hivyo hawawezi kuwa wafanyabiashara. Inatia huruma watu wazima kama hawa kurudi na kuja kuishi kwa wazazi wao wakiwa jobless. Wakati tunashirikiana na kufanya kazi kwa pamoja kujaribu kuondokana na uozo wa chama cha mapinduzi ili kuikomboa nchi yetu, ni muhimu juhudi hizo ziende sambamba na jitihada za kujikomboa kibinafi.

Ninapoongelea ukombozi binafsi nna maanisha ni muhimu kujiandaa vizuri kwaajili ya ushindani binafsi unaoendelea katika jamii. Katika vyama tutapa ukombozi wa kitaifa. Ila wakati huo huo kila mtu binafsi anapaswa kufanya kazi kwa bidii kujiandaa au kujiendeleza yeye binafsi na familia yake.


Kama wewe ni mtu mwenye miaka kati ya 30 mpaka 45 na haujasoma na kuwa na degree na diploma utakuwa unakosea. Binadamu tumepewa nafasi ya kuishi duniani mara moja tu. Swali ni jeje wewe unataka kuishi maisha ya aina gain katika jamii. Jamii yetu imegawanyika kati ya walionacho na wasionacho na kwakiasi kikubwa tufauti yao imeletwa na ELIMU. Asilimia kubwa ya walionacho ni watu waliosoma vizuri na kupata kazi inayoyawezesha kumudu maisha, kuwa na hakiba, kuwa na vitega uchumi na hatimae kuwa na utajiri. Kama na wewe umechagua kuishi maisha mazuri katika miaka yako hii michache hapa duniani (your only one life) ni lazima usome vizuri ili uweze kuvuka kutoka katika tabaka la wasionacho na kwenda kwenye tabaka la walionacho. Kuna njia nyingi ya kuweza kuvuka daraja hilo ila njia ya uhakika kuliko zote ni ELIMU.

Wewe ulikaaa kweli USA.kama umekaa USA hata ufanye kazi ya aina ipi dollar 400 kwa week hukosi.Ukitegemea mshahara utaumbuka bila investment .full time mzigoni part time biashara.
 
Nilipata bahati ya kwenda kusoma Marekani mwaka 2000. Kuna jamaa kama 6 walinipokea na tukaishi wote vizuri sana. Nilipomaliza masomo nikarudi nyumbani nikapata kazi na sasa nnaendelea vizuri sana na maisha. Jamaa wawili kati ya wale 6 walionipokea walirudishwa Tanzania. Kwa bahati mbaya hawa jamaa hawakusoma kule marekani. Tulipokuwa kule tulikuwa na maisha sawa tu kwakuwa kule kila mtu anaweza kupata kazi kirahisi. Sasa wamerudishwa nyumbani hawa mabwana wanahangaika sana. Hawana kazi na hawawezi kupata kazi. Hawakujiwekea akiba hivyo hawawezi kuwa wafanyabiashara. Inatia huruma watu wazima kama hawa kurudi na kuja kuishi kwa wazazi wao wakiwa jobless. Wakati tunashirikiana na kufanya kazi kwa pamoja kujaribu kuondokana na uozo wa chama cha mapinduzi ili kuikomboa nchi yetu, ni muhimu juhudi hizo ziende sambamba na jitihada za kujikomboa kibinafi.

Ninapoongelea ukombozi binafsi nna maanisha ni muhimu kujiandaa vizuri kwaajili ya ushindani binafsi unaoendelea katika jamii. Katika vyama tutapa ukombozi wa kitaifa. Ila wakati huo huo kila mtu binafsi anapaswa kufanya kazi kwa bidii kujiandaa au kujiendeleza yeye binafsi na familia yake.


Kama wewe ni mtu mwenye miaka kati ya 30 mpaka 45 na haujasoma na kuwa na degree na diploma utakuwa unakosea. Binadamu tumepewa nafasi ya kuishi duniani mara moja tu. Swali ni jeje wewe unataka kuishi maisha ya aina gain katika jamii. Jamii yetu imegawanyika kati ya walionacho na wasionacho na kwakiasi kikubwa tufauti yao imeletwa na ELIMU. Asilimia kubwa ya walionacho ni watu waliosoma vizuri na kupata kazi inayoyawezesha kumudu maisha, kuwa na hakiba, kuwa na vitega uchumi na hatimae kuwa na utajiri. Kama na wewe umechagua kuishi maisha mazuri katika miaka yako hii michache hapa duniani (your only one life) ni lazima usome vizuri ili uweze kuvuka kutoka katika tabaka la wasionacho na kwenda kwenye tabaka la walionacho. Kuna njia nyingi ya kuweza kuvuka daraja hilo ila njia ya uhakika kuliko zote ni ELIMU.
Street smart is the way to go.nimesomeshwa na wazazi Cheti kipo tuu nimeolewa na rich man na Ninabiashara zangu .degree akili ya mtu maskini
 
Wewe ni mtu wa ajabu sana. Kama wewe ulitaka kurudi nyumbani ni wewe. Wao pengine walitaka kubaki na kujiendeleza. Hatuwezi wote tukawa sawa. Kusoma na kumaliza, kupata kazi sio wote wameweza jwenda kwenye hio series.
Wapo waliosoma US hawapati kazi huko na sio chaguo lao kurudi nyumbani.
Narudia tena, kama wewe umejinyookea mshukuru Mungu wako. Na sio kuwabeza na kuwadharau wenzako.
Hujui nini Mungu amewaandikia, soon or later watafanikiwa na watakuacha wewe hapo unajifanya ndo umeshapatia maisha.
Maisha ni pata potea ndugu. Chunga mdomo wako.
Aminiusiamini mwanangu acha kutetea upuuuzi. Kuishi nje ni mtaji kama una malengo. Walipaswa wasome badala ya kuendekeza parties na upuuzi mwingine. Laiti wangekuwa wamesoma angalau wangeweza hata kuulaumu mfumo. Walikosea. Na kwa sasa hali ilivyo hawawezi kusoma Bongo kwa vile wanapaswa wapate mikopo. Hata kama wangeishi nje wangeishia pabaya. Maana wakati wana nguvu wangeweza kupata vibarua. Hawakuangalia kuwa wakizeeka wangeishije. Isitoshe kuishi nje kwa kubangaiza yaani bila makaratasi nao ni aina fulani ya utumwa. Anakufa mtu watu wanachangishana utadhani hawakuwa na akili wala nguvu za kufanya kazi au kutafuta elimu yenye kuweza kuwapatia lau ki akiba. Tubadilikeni jamani duniani tunaishi mara moja.
 
Aminiusiamini mwanangu acha kutetea upuuuzi. Kuishi nje ni mtaji kama una malengo. Walipaswa wasome badala ya kuendekeza parties na upuuzi mwingine. Laiti wangekuwa wamesoma angalau wangeweza hata kuulaumu mfumo. Walikosea. Na kwa sasa hali ilivyo hawawezi kusoma Bongo kwa vile wanapaswa wapate mikopo. Hata kama wangeishi nje wangeishia pabaya. Maana wakati wana nguvu wangeweza kupata vibarua. Hawakuangalia kuwa wakizeeka wangeishije. Isitoshe kuishi nje kwa kubangaiza yaani bila makaratasi nao ni aina fulani ya utumwa. Anakufa mtu watu wanachangishana utadhani hawakuwa na akili wala nguvu za kufanya kazi au kutafuta elimu yenye kuweza kuwapatia lau ki akiba. Tubadilikeni jamani duniani tunaishi mara moja.
It depends wamerudishwa Vipi .kama walikuwa hawana Ada ya shule? USA is the land of opportunity street smart is the way to go.ukitaka kitu chochote hapa unapata hakuna madeal.its about your choices
 
We umesema ulipoenda kule walikupokea na wakakusaidia ,inakuaje leo wamepata matatizo unawacheka?
Unajuaje labda walishindwa kusoma kwa kukosa ada?au walifeli wakagive up?

Wema auozi,walikusitiri na wewe watendee mema yaliyo kwenye uwezo wako.
Hamna kitu ambacho kimejitosheleza,kuwa na pesa,elimu ni nyongeza tu lakini haimaanishi ndo umekamilika.

Wanaigeria wenye PhD waloomba kazi ya udereva uliwasikia?

Unaweza kunambia azam ana elimu ya level ipi?mana umesema wenye mafanikio ni waliosoma.
 
Natalia mwanangu tell it to the birds. Despite being the land of opportunity, not for all. We have so many brothren suffering down there. The Hollywood world many people perceive does not exist for all. Again, how many earthlings do we have that can't make it back home simply because things turned out to be different? There are a lot out there suffering silently. They can't even afford to think about returning back home. Methinks education is the only solution. Go for it however it depends on your choice and guts.
 
Safari za Marekani si wote wenye malengo ya kusoma, kila mtu ana malengo yake na kama bahati yake imemfikia atafanikiwa na ambao hapakuwa mahali pao pamewakali vibaya, hiyo ndiyo hali halisi.

Kusoma siku hizi ni hakika kunaweza kukusaidia au kukupotezea muda wako. Jambo la msingi fuata mwelekeo wa maisha yanavyokutiririkia ndio mafanikio. Si wasomi wote wenye maisha mazuri na si wasio soma wote wenye maisha machungu. Elimu nzuri ni ile unaosoma kisha unafanyia kazi baada ya uzoefu unaenda kuongeza ujuzi huku kibarua chako kipo, na hata ukiona mambo hayaendi unaweza kubadilisha mwelekeo wa ujuzi ili uwe na soko zuri la ajira. Vinginevyo kuoedelea kusomea hadi PHD wa kupamba maua wakati tanzania ajira ya interior and exterior design haija kua utaona umepotezea muda kwa kitu ambacho hutakifanyia kazi kupata ajira na bora uende kufundisha tuition itakupa cha kuishia.

Nikiwa shuhuda nilipokuwa huko naweza kutolea mifano ila hapa si mahala pake nikwamba;
Marekani jambo la msingi chaguo sahihi la kazi unayotaka, unaweza ukachukua mafunzo ya muda mfupi tu ukawa na pato kupita mwenye PHD, amini usiamini huo ndio ukweli. Kama ujuzi unao hata wa kutoka Tanzania unajihakikishia ajira, mimi sikupoteza muda kupata ajira nilipokuwa chuoni huko kwa vile nilishakuwa na uzoefu wa kazi ingawa nilikuwa nachukua mafunzo kwenye mchepuo mwingine lakini taaluma yangu ya publishing ilinipa mshiko haraka kufanya kazi ya co-editor kwenye gazeti kubwa tu na watu wakawa wanashangaa nimepataje kazi huko ambako hata wenyenye hupata wakati mgumu kupata ajira pale.

Kuna waliosoma GED (general education developoment) kwa wale wasiohitimu highschool elimu ambayo Tanzania tunailinganisha na ngumbalo (elimu ya watu wazima). Nimekuja shuhudia jamaa wamefanya kazi za kuokoteza na kupata uzoefu kisha wanaajiriwa makampuni makubwa na wanatengeneza over $1500 a week wakati wengi wenye kusota na PHD wanaambulia under $1000 a week.

Wengi wanapoteza muda mwingi kusoma mfululizo na wanapohitimu elimu ya juu sana wanakuja kushtukia hakuna wa kuwaajiri kwa sababu ya kukosa uzoefu na kushtukia mwenye GED anaajiriwa kwa sababu ya uzoefu wa kazi. Hali kama hiyo ndiyo tunayoanza kupambana nayo Tanzania.

Maraha na maisha ya kuonyeshana watanzana waliopo ughaibuni ni kitu kinacho wagharimu wengi. Marekani kuna party za watanzania NY, DC, Texas, Minesota na sehemu nyinginezo kwa awamu. Utakuta jamaa akitoka kwenya party hii anakazana kufanya kazi na kukusanya pesa kwa ajili ya kwenda kwenye party nyingine huku ame-lease gari ambalo laonekana ghali sana kumbe la kukodi kwenda kuonyeshana kwenye party. Ipo siku mambo yanaenda visivyo na kuona kibarua kimeota mbawa, bongo hakikuandaliwa kitu hakuna pakufikia, kufikia kwa wazazi aibu maana hata hela sikuwa nawatumia, bora kuzamia ndiyo maisha yanapoanza kuwa machungu.

Mleta mada nakushangaa kama hao ni rafiki zako na walikupokea vizuri, lakini leo umewageuka baada ya kuona umejijenga. Nadhani uzoefu wako wa hapa nyumbani ungefanya jambo la msingi hata kimawazo tu kuwapa ushauri wa kufaa kwani bongo ukitumia bongo mkono hautoki mtupu. Ila ulichokifanya ni sawa na kuwadhalilisha best friends wako na unaonyesha ulivyo rafiki wakati wa raha na wakati wa taabu ukanata mzizi wa urafiki.
 
Ndugu yangu elimu sio kila kitu ni ujanja tu wa mujini. Nenda kariakoo uone wakinga walivyo na hela. Waneishia la saba wale. Nna jamaa yangu aliishia la saba sasa hivi ameoa, ana watoto, ana nyumba nzuri, ana gari na hela kibao kwenye mzunguko. Mi niliyejifanya nna akili ya kufika mpaka chuo sioni matumaini yoyote zaidi ya kuona watu wakipunguza umri kila leo. Tena nikikutana naye ananitania, we uliyepotea njia njoo nikunyweshe bia. Maisha haya ni kujipanga namna ya kutafuta na sio kutegemea njia moja tu. Unatakiwa uchezeshe akili kote kote.
nadhani hujamwelewa mleta mada,hajasema usipo soma huwezi kuondokana na umasikini wa kipato laa! anasema njia ya uhakika ni elimu. elimu imewatoa wengi sana bila kujali unatoka katika familia gani.siyo lazima kila aliye soma awe na maisha bomba inategemea na fani uliyo somea.mathalani Daktari bingwa uwezekano wa kuwa tajiri ni almost 98%,askari wa jeshi aliyesoma ana nafasi kubwa ya kuachana na umasikini wa kipato.kimsingi elimu nzuri ni kila kitu when it comes to fight against poverty.
 
Wewe ni mtu wa ajabu sana. Kama wewe ulitaka kurudi nyumbani ni wewe. Wao pengine walitaka kubaki na kujiendeleza. Hatuwezi wote tukawa sawa. Kusoma na kumaliza, kupata kazi sio wote wameweza jwenda kwenye hio series.
Wapo waliosoma US hawapati kazi huko na sio chaguo lao kurudi nyumbani.
Narudia tena, kama wewe umejinyookea mshukuru Mungu wako. Na sio kuwabeza na kuwadharau wenzako.
Hujui nini Mungu amewaandikia, soon or later watafanikiwa na watakuacha wewe hapo unajifanya ndo umeshapatia maisha.
Maisha ni pata potea ndugu. Chunga mdomo wako.

Ni ujinga na upumbafu kuona utakaa marekani na kufanikiwa....wakome kuwa na mawazo ya kibaharia kama mtu flani hivi humu jf iliyekaa marekani miaka lukuki mwisho wa siku anakuja tz kutaka kuwa mjumbe wa nec....
 
Elimu ndio ufunguo wa maisha
Je maisha bila elimu hayaendi?
Muangalie inzi na mfano wa maisha wewe ukijua hivi mwengine anajua vile hayo ni matatizo tuu usiwakebei kwani fainali haitabiriki
 
Kwa bahati mbaya wanaopiga kelele ni wale ambao hawajatoka nje. Kingine sioni cha ajabu mtu kuamua kuishi nje. Na hii sio kielelezo kuwa watafanikiwa.ni uamuzi.
 
Leo hapa patachimbika. But all in all, its a good advice. Kuwekeza kwenye elimu kuna faida yake, na kujiwekea akiba pia. Fainali uzeeni, sio kila siku utakuwa na nguvu ya kubeba boksi, there is a stopping point.
 
Kama ni maisha ni yako mwenyewe.

Sasa ya nini kujishughulisha na ya wengine?

Yako yamekushinda ama?
 
nadhani hujamwelewa mleta mada,hajasema usipo soma huwezi kuondokana na umasikini wa kipato laa! anasema njia ya uhakika ni elimu. elimu imewatoa wengi sana bila kujali unatoka katika familia gani.siyo lazima kila aliye soma awe na maisha bomba inategemea na fani uliyo somea.mathalani Daktari bingwa uwezekano wa kuwa tajiri ni almost 98%,askari wa jeshi aliyesoma ana nafasi kubwa ya kuachana na umasikini wa kipato.kimsingi elimu nzuri ni kila kitu when it comes to fight against poverty.


Huyu bwana amewajibu critics wote. Someni ujumbe kwa utulivu muelewe. Acheni hasira kwakuwa kuna mambo yanawagusa nyie binafsi. Hii haiwahusu nyie. Ni ushauri kwa vijana wanaoanza maisha. Besides sijacheka wala kukashifu mahali popote. Sijataja jina la mtu-so sielewi huku kumcheka mtu kupo wapi. Wengi wanatazama lakini hawaoni. Wengi wanasikia lakini hawaelewi. Wenye macho mazuri wataona umuhimu, wenye masikio mazuri wataelewa. Salut!
 
Aminiusiamini mwanangu acha kutetea upuuuzi. Kuishi nje ni mtaji kama una malengo. Walipaswa wasome badala ya kuendekeza parties na upuuzi mwingine. Laiti wangekuwa wamesoma angalau wangeweza hata kuulaumu mfumo. Walikosea. Na kwa sasa hali ilivyo hawawezi kusoma Bongo kwa vile wanapaswa wapate mikopo. Hata kama wangeishi nje wangeishia pabaya. Maana wakati wana nguvu wangeweza kupata vibarua. Hawakuangalia kuwa wakizeeka wangeishije. Isitoshe kuishi nje kwa kubangaiza yaani bila makaratasi nao ni aina fulani ya utumwa. Anakufa mtu watu wanachangishana utadhani hawakuwa na akili wala nguvu za kufanya kazi au kutafuta elimu yenye kuweza kuwapatia lau ki akiba. Tubadilikeni jamani duniani tunaishi mara moja.


Waambie baba waambie. Watu wenye agenda za siri mapovu yanawatoka ila ukweli wanaujua mioyoni mwao!
 
Nilipoajiriwa,bosi wangu anamiliki biashara yenye mtaji wa zaidi ya dola Milioni sita au saba hv,ni mtanzania na ana miaka 33,
ana vitega uchumi vingi na vya kutosha,elimu yake ni darasa la saba na si zaidi.........

huyu jamaa amesafiri nchi mbalimbali kibiashara,anaongea kiingereza cha kawaida,ni msomaji mzuri wa jamiiforum ingawa hajajiunga lakini pia anajuai vitu vingi sana vya sasa hv na anaishi kisasa kama vijana wa kisasa.

Nilichojifunza kwa bosi wangu huyu ni kwamba,elimu ni muhimu sana katika maisha,lakini si lazima uwe na elimu kubwa ndo ufanikiwe,mafanikio ni mchanganyiko wa vitu vingi sana,kama kufanya kazi kwa bidii,kusali sana,kuwa na ujasiri wa maamuzi,elimu ya wastani,uelewa wa mambo mengi angalau kidogokidogo,nia ya kufanikiwa na mengine mengi.

sasa mm nasema hv,hao jamaa zako inawabidi wabadilishe mitazamo yao kuhusu maisha huku nyumbani,pia wajifunze wako katika kipindi gani cha kiuchumi na kibiashara,lazima waangalie kuna fursa gani waweze kuzichangamkia,wakichagua kazi wamekwisha...watazeekea nyumbani na mwishowe watakua very frustrated,na hapo kuna hatari ya kuanza kutumia vitu vya ajabu ajabu...wafahamu pia wazazi wao wanaumia sana wakiwaona jinsi walivyo,kusomesha mtu au kumpeleka marekani mtoto si kitu ambacho wazazi wengi wanakimudu ni ghali...tena sana

waambie pia maisha yamebadilika sana siku hz,kuishi au kufanya kazi marekani sio ishu tena,ni kawaida tu,cha muhimu ni noti,noti noti......nasisitiza wasipobadilisha mitizamo yao wataishia pabaya sana huwezi kusema hawawezi kupata kazi wakati kazi zipo zimejaa tele....wawe wabunifu....si lazima aanze na kazi ya kulipwa million mbili....inabidi waanzie chini
maana system imeshawatupa...
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom