Baada ya kupigiwa simu jana, nina maswali 3 kwa wapinzani wa UKAWA ndani ya CHADEMA na CUF

Mikael Aweda

JF-Expert Member
Dec 17, 2010
2,973
3,901
Wadau,
Jana nilipigiwa simu na mtu ambaye ninamfahamu kidogo kama mwanachadema kwani tuliwahi kuonana mara moja tukaongea naye kwa muda mrefu maeneo ya ukonga Dsm. Jana alinipigia simu na kunipongeza kwa makala yangu JF na facebook. Baada ya pongezi nyingi kuliko kawaida akanisihi kuwa sisi wazalendo wa kweli ndani ya Chadema tukae kwa umakini na tujadili kwa undani hatima ya chadema yetu ndani ya ukawa.

Baada ya kuongea naye kwa muda mrefu kwenye simu akiwa na umakini wa hali ya juu sana na akionekana kama mtu mwenye kuipenda sana chadema kuliko viongozi wa juu wa chadema, alinisihi nikutane naye kwenye hoteli Ubungo Plaza kwa chakula cha mchana ili tujadili hatima ya Chama chetu. Nilimkatalia.

Hata hivyo, nina maswali matatu kwa wapinzani wa UKAWA ndani ya chadema na CUF.
Mosi, Ni kwa nini wanaopinga ukawa kwa nguvu ni watu wenye matatizo ndani ya vyama vyao kama Yona aliyekanwa uongozi halali wa chadema Temeke kuwa siyo mwenyekiti?? Fuatilia wapinzani wote wa ukawa JF, Utaliona hilo.

Pili, kwa nini taarifa zao au propaganda zao zinatoka zaidi kwenye magazeti yanyomilikiwa na ccm moja kwa moja au makada wa ccm ? Na kwa nini mara nyingi huwa wanaficha vyanzo vya habari zao? (Juliana shonza mwanaccm aliyeasi chadema, ndo ameleta taarifa hapa JF ya mjumbe wa Baraza kuu cuf kujiuzulu)

Tatu, gharama ya kunikaribisha kwenye chakula cha mchana ubungo Plaza kujadili mambo haya inatoka kwa nani na kwa maslahi ya nani?? Au mhusika anagaenda gani zaidi?? Mtu huyu kwa kumwangalia tu kwa macho ya kawaida, siyo mtu wa kunikaribisha chakula cha mchana ubungo Plaza. Na kwa nini ubungo Plaza, mbona mara ya kwanza tulipoonana tulikaa masaa mawili na tukaishia kunywa maji na soda tu tena kwenye mgahawa wa kawaida.
NB; Kilichonishtua zaidi ni pale nilipomshauri kuwa awasilishe hofu yake kwa viongozi wa juu lakini hakutaka hilo, badala yake aonnane na mimi ili tujadili hatima ya chadema yetu sisi wazalendo wa chadema.

Ni maswali ninayojiuliza, wahenga wanasema hakuna swali la kijinga ila kuna jibu la kijinga.

Baada ya kumsikiliza ushauri wa akili yake niliuchanganya na akili yangu, nikajiambia mwenyewe, sidanganyiki.

Nawasilisha.
 
Wadau,
Jana nilipigiwa simu na mtu ambaye ninamfahamu kidogo kama mwanachadema kwani tuliwahi kuonana mara moja tukaongea naye kwa muda mrefu maeneo ya ukonga Dsm. Jana alinipigia simu na kunipongeza kwa makala yangu JF na facebook. Baada ya pongezi nyingi kuliko kawaida akanisihi kuwa sisi wazalendo wa kweli ndani ya Chadema tukae kwa umakini na tujadili kwa undani hatima ya chadema yetu ndani ya ukawa.

Baada ya kuongea naye kwa muda mrefu kwenye simu akiwa na umakini wa hali ya juu sana na akionekana kama mtu mwenye kuipenda sana chadema kuliko viongozi wa juu wa chadema, alinisihi nikutane naye kwenye hoteli Ubungo Plaza kwa chakula cha mchana ili tujadili hatima ya Chama chetu. Nilimkatalia.

Hata hivyo, nina maswali matatu kwa watu wapinzani wa ukawa ndani ya chadema na CUF.
Mosi, Ni kwa nini wanaopinga ukawa kwa nguvu ni watu wenye matatizo ndani ya vyama vyao kama Yona aliyekanwa uongozi halali wa chadema Temeke kuwa siyo mwenyekiti?? Fuatilia wapinzani wote wa ukawa JF, Utaliona hilo.

Pili, kwa nini taarifa zao au propaganda zao zinatoka zaidi kwenye magazeti yanyomilikiwa na ccm moja kwa moja au makada wa ccm ? Na kwa nini mara nyingi huwa wanaficha vyanzo vya habari zao? (Juliana shonza (mwanaccm aliyeasi chadema, ndo ameleta taarifa hapa JF ya mjumbe wa Baraza kuu cuf kujiuzulu)

Tatu, gharama ya kunikaribisha kwenye chakula cha mchana ubungo Plaza kujadili mambo haya inatoka kwa nani na kwa maslahi ya nani?? Au ana mhusika anagaenda gani zaidi?? Mtu huyu kwa kumwangalia tu kwa macho ya kawaida, siyo mtu wa kunikaribisha chakula cha mchana ubungo Plaza. Na kwa nini ubungo Plaza, mbona mara ya kwanza tulipoonana tulikaa masaa mawili na tukaishia kunywa maji na soda tu tena kwenye mgahawa wa kawaida.
NB; Kilichonishtua zaidi ni pale nilipomshauri kuwa awasilishe hofu yake kwa viongozi wa juu lakini hakutaka hilo, badala yake aonnane na mimi ili tujadili hatima ya chadema yetu sisi wazalendo wa chadema.

Ni maswali ninayojiuliza, wahenga wanasema hakuna swali la kijinga ila kuna jibu la kijinga.

Baada ya kumsikiliza ushauri wa akili yake niliuchanganya na akili yangu, nikajiambia mwenyewe, sidanganyiki.

Nawasilisha.
Ngoja waje tuone hoja zao! kifupi maswali yako yana maana sana!
 
Mkuu Aweda angalia sana usije kutolewa macho na kucha.

Ccm right now hali yao ni tete mpaka katibu mkuu wao na mwenezi wanajifanya nao huwa wanakula kwa mama ntilie na pia na wao huwa wanakunywa gongo by then wananchi wawaone ni wenzao.

Kwa hivi sasa kwao UKAWA ni INTANGIBLE as if wanakamata upepo,hawana mbinu zaidi ya kuingia MISIKITINI.

SI UMESIKIA KINANA AMEOMBA UGENI RASMI SIKU YA MAULID SINGIDA?
 
Wadau,
Jana nilipigiwa simu na mtu ambaye ninamfahamu kidogo kama mwanachadema kwani tuliwahi kuonana mara moja tukaongea naye kwa muda mrefu maeneo ya ukonga Dsm. Jana alinipigia simu na kunipongeza kwa makala yangu JF na facebook. Baada ya pongezi nyingi kuliko kawaida akanisihi kuwa sisi wazalendo wa kweli ndani ya Chadema tukae kwa umakini na tujadili kwa undani hatima ya chadema yetu ndani ya ukawa.

Baada ya kuongea naye kwa muda mrefu kwenye simu akiwa na umakini wa hali ya juu sana na akionekana kama mtu mwenye kuipenda sana chadema kuliko viongozi wa juu wa chadema, alinisihi nikutane naye kwenye hoteli Ubungo Plaza kwa chakula cha mchana ili tujadili hatima ya Chama chetu. Nilimkatalia.

Hata hivyo, nina maswali matatu kwa watu wapinzani wa ukawa ndani ya chadema na CUF.
Mosi, Ni kwa nini wanaopinga ukawa kwa nguvu ni watu wenye matatizo ndani ya vyama vyao kama Yona aliyekanwa uongozi halali wa chadema Temeke kuwa siyo mwenyekiti?? Fuatilia wapinzani wote wa ukawa JF, Utaliona hilo.

Pili, kwa nini taarifa zao au propaganda zao zinatoka zaidi kwenye magazeti yanyomilikiwa na ccm moja kwa moja au makada wa ccm ? Na kwa nini mara nyingi huwa wanaficha vyanzo vya habari zao? (Juliana shonza (mwanaccm aliyeasi chadema, ndo ameleta taarifa hapa JF ya mjumbe wa Baraza kuu cuf kujiuzulu)

Tatu, gharama ya kunikaribisha kwenye chakula cha mchana ubungo Plaza kujadili mambo haya inatoka kwa nani na kwa maslahi ya nani?? Au ana mhusika anagaenda gani zaidi?? Mtu huyu kwa kumwangalia tu kwa macho ya kawaida, siyo mtu wa kunikaribisha chakula cha mchana ubungo Plaza. Na kwa nini ubungo Plaza, mbona mara ya kwanza tulipoonana tulikaa masaa mawili na tukaishia kunywa maji na soda tu tena kwenye mgahawa wa kawaida.
NB; Kilichonishtua zaidi ni pale nilipomshauri kuwa awasilishe hofu yake kwa viongozi wa juu lakini hakutaka hilo, badala yake aonnane na mimi ili tujadili hatima ya chadema yetu sisi wazalendo wa chadema.

Ni maswali ninayojiuliza, wahenga wanasema hakuna swali la kijinga ila kuna jibu la kijinga.

Baada ya kumsikiliza ushauri wa akili yake niliuchanganya na akili yangu, nikajiambia mwenyewe, sidanganyiki.

Nawasilisha.
Ili kumaliza hii weka simu yake hapa vinginevyo atakushughurikia kwa siri
 
Ni lini cuf wameacha kuwa ccm B?
ni lini nccr mageuzi wameacha kuwa tawi la CCM?
haya majina mabaya mabaya ya kuwachafua wenzenu mchana kisha jioni mnawaita marafiki haamaaanshi uroho wa madaraka wa chadema?
 
Mkuu Aweda angalia sana usije kutolewa macho na kucha.

Ccm right now hali yao ni tete mpaka katibu mkuu wao na mwenezi wanajifanya nao huwa wanakula kwa mama ntilie na pia na wao huwa wanakunywa gongo by then wananchi wawaone ni wenzao.

Kwa hivi sasa kwao UKAWA ni INTANGIBLE as if wanakamata upepo,hawana mbinu zaidi ya kuingia MISIKITINI.

SI UMESIKIA KINANA AMEOMBA UGENI RASMI SIKU YA MAULID SINGIDA?

Dr Slaa alipotaja majina ya mafisadi wakiwepo majina ya Marais aliulizwa waandishi kama haogopi kufa. Yeye alijibu, maji ukishavulia nguo, huna budi kuyaoga. Nina uhakika kuwa kila mtu akiogopa kufa au tukiwa dhaifu mbele ya rushwa nina uhakika ccm wataiuza nchi hii kwa bei ya jumla siku moja. Nina uhakika hilo halitatokea katika kizazi changu.
 
Kiongozi umesave, ungefanywa msukule sasahivi. Sasahivi hawana mbinu nyingine zaidi ya kuwanyamazisha kwa namna yoyote watu wote wenye ushawishi ndani ya UKAWA:
 
Ni lini cuf wameacha kuwa ccm B?
ni lini nccr mageuzi wameacha kuwa tawi la CCM?
haya majina mabaya mabaya ya kuwachafua wenzenu mchana kisha jioni mnawaita marafiki haamaaanshi uroho wa madaraka wa chadema?

Baada ya kuungana na ukawa dhidi ya ccm.
 
Mikael P Aweda Hebu tuwekee hati ya makubaliano ya kuungana pia.

Hati ya muungano tunaiandika ndani ya mioyo ya watanzania kwa vitendo siyo kwenye makaratasi. Sheria zinaandikwa na kuvunjwa kila siku au hujui?
Umesahau kananu ya BMK iliyoandaliwa kwa mabilioni ya kodi za watanzania SITTA akaivunja tu wiki ya kwanza kwa kumtanguliza warioba kwa maslahi ya ccm? Ile kanuni iliandikwa ikasainiwa ikavujwa
 
Back
Top Bottom