Baada ya Kuongoza Jahazi la Kampeni za JK Bw. Mukama na Bw. Kinana Watafaidika Nini?

Gosbertgoodluck

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,855
401
Wakuu,
Hao jamaa wawili inawezekana ilikuwa ni chachu ya 'ushindi wa kiaina' wa jk kwenye kinyang'anyilo cha urais. Mmoja alikuwa ndiye m/kiti na mratibu wa kampeni za jk na mwingine alihusika kwenye kampeni kwa kuielezea na kuifafanua ilani ya uchaguzi ya ccm. Inasemekana ni mmojawapo wa wataalam walioshiriki kuiandaa hiyo ilani. Ninachojiuliza ni je hao jamaa ndiyo wameishia hapo???? Tangu matokeo ya uchakachuaji yatoke sijawasikia tena hata kwenye halfa mbalimbali za kujipongeza kufanikisha uchakachuaji siwaoni na nimehudhuria takriban zote. Kulikoni? Au sasa wanakula 'kuku kwa mrija' kimyakimya, au wametupwa nje kama gunia la deki baada ya kumaliza usafi wa ndani, au wanasubiri vyeo vingine ndani ya serikali na chama??? Nasikia mmojawapo ni m/kiti wa bodi ya magazeti ya serikali.
 
hakuna uchakachuaji,ishu ni kwamba watanzania wlimkataa Slaa,hawakuzoea vitisho vya kumwaga damu,hawkuzoea kumpenda mtu kwa kigezo cha dini
 
kuna namna yake ya kuwapongeza hawa sio lazima wapewe uongozi kwani kinana si ana meli!
 
hakuna uchakachuaji,ishu ni kwamba watanzania wlimkataa Slaa,hawakuzoea vitisho vya kumwaga damu,hawkuzoea kumpenda mtu kwa kigezo cha dini


we post zako zinaendana kabisa na jina lako,yani sijaona hoja hapo its nonsense kalamazoooooooo
 
Mjanja yeyete haitaji kuwa na nafasi ya kisiasa ili kutengeneza pesa, ujanja ni kukamata viongozi na ku make money, Kinana haitaji Uwaziri au umkuu wa mkoa , mambo yako supa kwake ,JK hawezi furukuta , si ni yeye ndio kam Mweka, hope na Ruge atasema hivyo hiyo naye kamuweka JK madarakani, ile fiesta na kina Diamond unadhani bure bure?
 
Back
Top Bottom