Baada ya kuona kinachoendelea uchaguzi Kenya, thinking ya UCHAWA CCM nilitegemea ibadilike, kuondoa mawazo ya utwana na utumwa wa kumuona Rais Mungu

Retired

JF-Expert Member
Jul 22, 2016
40,356
73,935
Tuna mengi sana ya kujifunza Kenya na uchaguzi wao.
1. Uwazi
2. Uhuru wa media zao
3. Incumbent president Uhuru hana kauli yoyote kuhusu uchaguzi
4. Katiba yao inaruhusu haya yanayotokea
5. etc etc etc

Summary nzuri ameifanya Askofu Bagonza kama ilivyo hapa chini!


UCHAGUZI MKUU KENYA

KUPIGA KURA Vs KUCHAGUA


Uchaguzi Mkuu wa Kenya unakaribia kukamilika ninapoandika uzi huu; Nimejifunza mengi:

1. Kenya wanapiga kura na kuchagua. Penginepo tunapiga kura, hatuchagui.

2. Kenya wana imani na mfumo wao wa uchaguzi. Penginepo hata wanaoshida wanashangaa wameshindaje.

3. Kenya mgombea akinadiwa na rais anayeondoka anakataliwa. Penginepo mgombea akinadiwa na anayeondoka anadeka.

4. Kenya wakifanya uchaguzi majirani tunakesha. Penginepo tukifanya uchaguzi majirani wanalala mapema maana matokeo wanayajua tayari.

5. Kenya kuna vurugu zinazoletwa na katiba nzuri. Penginepo kuna utulivu unaoletwa na katiba mbaya.

6. Kenya kuna ukabila unaongoza demokrasia. Penginepo kuna itikadi ya vyama zenye nguvu kuliko katiba.

7. Kenya katiba ina nguvu kuliko nchi. Penginepo kuna watu wana nguvu kuliko nchi. Hili ni tata sana.

8. Kenya wanachagua wezi kidemokrasia. Penginepo wezi wananyimwa kura na kuchaguana wenyewe.

9. Kenya wanachagua shetani anageuka kuwa malaika. Penginepo wanachagua malaika anageuka kuwa shetani.

10. Kenya unaweza kumshtaki mtu kabla hajatenda kosa. Penginepo hata aliyetenda kosa tayari unamuomba ruhusa kumshtaki.

KENYA IMESHINDA, WAGOMBEA WAMESHINDWA. PENGINEPO KWA MAJIRANI WANAOGOPA KUJARIBU SUMU KWA KUIONJA.

Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi
 
Viongozi wa Tanzania wanapenda sifa za kijinga kutoka kwa machawa wao ambao hupenda kusikia kile anacho penda yeye na machawa kwa kutambua hilo wanatumia nafasi hiyo vema kabisa

Ni aibu kwa mkuu wa nchi kuanza kulalamikia vyombo vya habari ety kwa sababu wanaonesha picha za watu wachache kwenye ziara yake Sasa huu sio myopic.

Mzee JK yupo hapo Kenya anatoa misifa kibao ila akirudi Tz utashangaa mwaka 2025 ndo akawa Master minder wa kuharibu uchaguzi tena bila aibu.
 
Tuna mengi sana ya kujifunza Kenya na uchaguzi wao.
1. Uwazi
2. Uhuru wa media zao
3. Incumbent president Uhuru hana kauli yoyote kuhusu uchaguzi
4. Katiba yao inaruhusu haya yanayotokea
5. etc etc etc

Summary nzuri ameifanya Askofu Bagonza kama ilivyo hapa chini!


UCHAGUZI MKUU KENYA

KUPIGA KURA Vs KUCHAGUA


Uchaguzi Mkuu wa Kenya unakaribia kukamilika ninapoandika uzi huu; Nimejifunza mengi:

1. Kenya wanapiga kura na kuchagua. Penginepo tunapiga kura, hatuchagui.

2. Kenya wana imani na mfumo wao wa uchaguzi. Penginepo hata wanaoshida wanashangaa wameshindaje.

3. Kenya mgombea akinadiwa na rais anayeondoka anakataliwa. Penginepo mgombea akinadiwa na anayeondoka anadeka.

4. Kenya wakifanya uchaguzi majirani tunakesha. Penginepo tukifanya uchaguzi majirani wanalala mapema maana matokeo wanayajua tayari.

5. Kenya kuna vurugu zinazoletwa na katiba nzuri. Penginepo kuna utulivu unaoletwa na katiba mbaya.

6. Kenya kuna ukabila unaongoza demokrasia. Penginepo kuna itikadi ya vyama zenye nguvu kuliko katiba.

7. Kenya katiba ina nguvu kuliko nchi. Penginepo kuna watu wana nguvu kuliko nchi. Hili ni tata sana.

8. Kenya wanachagua wezi kidemokrasia. Penginepo wezi wananyimwa kura na kuchaguana wenyewe.

9. Kenya wanachagua shetani anageuka kuwa malaika. Penginepo wanachagua malaika anageuka kuwa shetani.

10. Kenya unaweza kumshtaki mtu kabla hajatenda kosa. Penginepo hata aliyetenda kosa tayari unamuomba ruhusa kumshtaki.

KENYA IMESHINDA, WAGOMBEA WAMESHINDWA. PENGINEPO KWA MAJIRANI WANAOGOPA KUJARIBU SUMU KWA KUIONJA.

Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi
Eti Chadomo wanawapangia ccm utaratibu wa kuendesha uchaguzi 🤣🤣..

Mzee Kenya na Tanzania ni kama China na America,unachotaka hakitakaa kitokee.
 
Tuna mengi sana ya kujifunza Kenya na uchaguzi wao.
1. Uwazi
2. Uhuru wa media zao
3. Incumbent president Uhuru hana kauli yoyote kuhusu uchaguzi
4. Katiba yao inaruhusu haya yanayotokea
5. etc etc etc

Summary nzuri ameifanya Askofu Bagonza kama ilivyo hapa chini!


UCHAGUZI MKUU KENYA

KUPIGA KURA Vs KUCHAGUA


Uchaguzi Mkuu wa Kenya unakaribia kukamilika ninapoandika uzi huu; Nimejifunza mengi:

1. Kenya wanapiga kura na kuchagua. Penginepo tunapiga kura, hatuchagui.

2. Kenya wana imani na mfumo wao wa uchaguzi. Penginepo hata wanaoshida wanashangaa wameshindaje.

3. Kenya mgombea akinadiwa na rais anayeondoka anakataliwa. Penginepo mgombea akinadiwa na anayeondoka anadeka.

4. Kenya wakifanya uchaguzi majirani tunakesha. Penginepo tukifanya uchaguzi majirani wanalala mapema maana matokeo wanayajua tayari.

5. Kenya kuna vurugu zinazoletwa na katiba nzuri. Penginepo kuna utulivu unaoletwa na katiba mbaya.

6. Kenya kuna ukabila unaongoza demokrasia. Penginepo kuna itikadi ya vyama zenye nguvu kuliko katiba.

7. Kenya katiba ina nguvu kuliko nchi. Penginepo kuna watu wana nguvu kuliko nchi. Hili ni tata sana.

8. Kenya wanachagua wezi kidemokrasia. Penginepo wezi wananyimwa kura na kuchaguana wenyewe.

9. Kenya wanachagua shetani anageuka kuwa malaika. Penginepo wanachagua malaika anageuka kuwa shetani.

10. Kenya unaweza kumshtaki mtu kabla hajatenda kosa. Penginepo hata aliyetenda kosa tayari unamuomba ruhusa kumshtaki.

KENYA IMESHINDA, WAGOMBEA WAMESHINDWA. PENGINEPO KWA MAJIRANI WANAOGOPA KUJARIBU SUMU KWA KUIONJA.

Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi
Ngoja tuone
 
Back
Top Bottom