Beauty Eva
Senior Member
- Jul 22, 2016
- 131
- 374
Habari zenu ndugu! Ushauri wenu ni muhimu sana
Kuna mkaka mmoja mstaarabu sana kwa muonekano wake na hata katika mazungumzo yake. Kaka huyu tunatoka nae sehemu moja, ameoa na ana watoto. Shughuli zake anafanyia Arusha.
Mkaka huyu siku za nyuma baada ya kugundua nipo chuoni alikuwa anakuja kunitembelea na kuniletea zawadi ndogo ndogo kama vile ma-apple, chocolate, maziwa ya Azam etc . Nilikuwa nazipokea zawadi hizo kwa moyo mkunjufu maana nilikuwa namchukulia kama kaka yangu.
Siku moja akaniuliza walipo ndugu zangu hususan dada yangu tunaefuatana nae, nikamueleza kuwa dada yangu yupo hapa Arusha na nikampa namba za huyo dada yangu.
Siku zikapita, ukaka ukazidi na zawadi zikawa zinapokelewa. Nilikuja kushtuka siku alipoanza kunitumia msg ambazo zilikuwa zinaonesha kuwa ananivuta kimapenzi na haukupita Musa akaniletea zawadi ya underwears (night 👗 na pant). Baada ya hapo ndipo rasmi akaanza mchakato wa kunipata kimapenzi. Thanks to God kwamba, nilimkatalia na akanielewa japo kwa shingo upande. Tulikata mawasiliano kabisa
Baada ya mimi kumkatalia, kumbe akaanzisha harakati kumpata dada yangu. Binafsi nilikuwa sifahamu kuwa wanawasiliana, hadi juzi hapa ndipo nimebaini kuwa wana uhusiano wa karibu na muda si muda huenda wakamaliza kila kitu. Na nilibaini baada ya dada yangu kunieleza kuwa jamaa anamtaka na dada anasema, tayari moyo wake kwa kiasi kikubwa umetekwa na huyo kaka.
Sasa najiuliza, nimweleze dada kuwa huyo kaka hata mimi alinitaka nikamkataa au niwaache waendelee na hamsini zao?
Kuna mkaka mmoja mstaarabu sana kwa muonekano wake na hata katika mazungumzo yake. Kaka huyu tunatoka nae sehemu moja, ameoa na ana watoto. Shughuli zake anafanyia Arusha.
Mkaka huyu siku za nyuma baada ya kugundua nipo chuoni alikuwa anakuja kunitembelea na kuniletea zawadi ndogo ndogo kama vile ma-apple, chocolate, maziwa ya Azam etc . Nilikuwa nazipokea zawadi hizo kwa moyo mkunjufu maana nilikuwa namchukulia kama kaka yangu.
Siku moja akaniuliza walipo ndugu zangu hususan dada yangu tunaefuatana nae, nikamueleza kuwa dada yangu yupo hapa Arusha na nikampa namba za huyo dada yangu.
Siku zikapita, ukaka ukazidi na zawadi zikawa zinapokelewa. Nilikuja kushtuka siku alipoanza kunitumia msg ambazo zilikuwa zinaonesha kuwa ananivuta kimapenzi na haukupita Musa akaniletea zawadi ya underwears (night 👗 na pant). Baada ya hapo ndipo rasmi akaanza mchakato wa kunipata kimapenzi. Thanks to God kwamba, nilimkatalia na akanielewa japo kwa shingo upande. Tulikata mawasiliano kabisa
Baada ya mimi kumkatalia, kumbe akaanzisha harakati kumpata dada yangu. Binafsi nilikuwa sifahamu kuwa wanawasiliana, hadi juzi hapa ndipo nimebaini kuwa wana uhusiano wa karibu na muda si muda huenda wakamaliza kila kitu. Na nilibaini baada ya dada yangu kunieleza kuwa jamaa anamtaka na dada anasema, tayari moyo wake kwa kiasi kikubwa umetekwa na huyo kaka.
Sasa najiuliza, nimweleze dada kuwa huyo kaka hata mimi alinitaka nikamkataa au niwaache waendelee na hamsini zao?