Baada ya kumuoa ndio nimejua alishazaa na mwanaume mwingine

lauzi96

JF-Expert Member
Jul 10, 2014
422
795
Mimi katika maisha yangu nilishaapa sitooa mwanamke mwenye mtoto sababu ninajua mahawala hawaachani tena kama wamezaa ndio huwezi kuzuia kwa kisingizio matunzo ya mtoto kumbe jamaa anakumbushia.

Sasa mwezi wa 3 nimeoa ila huyo msichana mama yangu alikuwa hamtaki hata kumsikia, baada ya kukomaa mama akaniruhusu.

Nimemuoa na ndani ya miezi mitatu kwenye ndoa nimegundua ana watoto wawili ila mimi bado sijachukua uamuzi.

Ninaomba ushauri wenu, nimpe talaka aende kwao maana hii harusi hakuna aliyeitaka kwenye familia yangu mimi nimelazimisha tu na bora angeniambia kabla.
 
Mimi katika maisha yangu nilishaapa sitooa mwanamke mwenye mtoto sababu nnajua mahawala hawaachani tena kama wamezaa ndio huwezi kuzuia kwa kisingizio matunzo ya mtoto kumbe jamaa anakumbushia,sasa mwezi wa 3 nimeoa hila huyo msichana mama yangu alikuwa hamtaki hata kumsikia hila baada ya kukomaa mama akaniruhusu nimemuoa hila miezi 3 kwenye ndoa nimegundua ana watoto 2 ,kwahyo mimi bado sijachukua uamuzi nnaomba ushauri wenu nimpe talaka aende kwao maana hii harusi hakuna aliyeitaka kwenye family yangu mimi nimelazimisha tu na bora angeniambia kabla.
1. Umefunga ndoa kanisa/Msikitini?
2. Ulishawahi muuliza kuhusu kuwa na watoto/ Kama ndiyo alikujibu nini?
 
Jibu kwanza maswali haya kisha ushauriwe.:

1. Je baada ya kugundua hayo, moyoni una amani ya kuendelea kuishi na mkeo?. Maana hata mkishauriwa maisha yanabaki ya watu wawili tu.

2. Je utaweza kubadili mtazamo wako kuwa mwanake aliyezaa NAmwanaume mwingine si rahisi kutulia katika Ndoa.? Maana kama haujabadili mtazamo huo utaishia kuishi na mkeo kwa mashaka makubwa hata akiwa si mchepukaji.
 
Jibu kwanza maswali haya kisha ushauriwe.:

1. Je baada ya kugundua hayo, moyoni una amani ya kuendelea kuishi na mkeo?. Maana hata mkishauri maisha yanabaki ya watu wawili tu.

2. Je utaweza kubadili mtazamo wako kuwa mwanake aliyezaa NAmwanaume mwingine si rahisi kutulia katika Ndoa.? Maana kama haujabadili mtazamo huo utaishia kuishi na mkeo kwa mashaka makubwa hata akiwa si mchepukaji.
na mm nasubiri majibu ya hayo maswali nimshauri
 
Jambo kama hili lilimtokea rafiki yangu tulienda mkoa fulani kwenye sherehe akakutana na binti mmoja ambaye alionekana anajiheshimu maana muda wote kwenye sherehe ile alikuwa mtulivu sana, jamaa akapenda uchumba ukaanza muda wote jamaa yangu alijua yule binti hana mtoto, kuna kipindi alimtembelea alikataa kata kata kufanya nae chochote yaani walikaa siku tatu bila kufanya, ndoa ikafungwa haraka sana baada ya mwaka mmoja ndipo jamaa kugundua yule mwanamke ana mtoto na hapo alikuta sms iliyomtaka yule mwanamke atume pesa au aende kuchukua mtoto kumuuliza akakataa ikabidi jamaa aende mwenyewe kwao na mwanamke ndipo akaujua ukweli.

Kuepusha dhahama ikabidi yule jamaa amchukue yule mtoto aende kuishi nae, siku zimesonga yule jamaa akagundua kuwa mke wake anawasiliana na mtu kupitia jirani wa duka (alikuwa amemfungulia biashara).

Jamaa akapeleleza akagundua kuwa yule mwanaume anamtaka mtoto wake, baada ya muda mwanamke yule akataka kwenda kwao jamaa akamkubalia baada ya kama siku mbili jamaa akafunga Safari kimya kimya mpaka kwao akakuta hajafika akapeleleza anapoishi yule mwanaume aliyezaa na mke wake akaenda huko akamkuta bibie amejiachia anapika ikawa mwisho wa ndoa.

Rule no 1: Usioe mwanamke mwenye mtoto.
 
Ulifanya makosa makubwa sana mawili:

1) Kutomsikiliza mzazi wako ni kwanini hakutaka umuoe huyo binti, badala yake ukakurupuka

2) Kutomchunguza huyo binti au historia yake kabla ya kumuoa.

Kwakuwa alikudanganya, Mwache huyo mwanamke na utulie na kumwomba Mungu akupe mke atakayekufaa.

Pia mwombe mama yako msamaha kwa kumpuuza.
 
Mimi katika maisha yangu nilishaapa sitooa mwanamke mwenye mtoto sababu ninajua mahawala hawaachani tena kama wamezaa ndio huwezi kuzuia kwa kisingizio matunzo ya mtoto kumbe jamaa anakumbushia.

Sasa mwezi wa 3 nimeoa ila huyo msichana mama yangu alikuwa hamtaki hata kumsikia, baada ya kukomaa mama akaniruhusu.

Nimemuoa na ndani ya miezi mitatu kwenye ndoa nimegundua ana watoto wawili ila mimi bado sijachukua uamuzi.

Ninaomba ushauri wenu, nimpe talaka aende kwao maana hii harusi hakuna aliyeitaka kwenye familia yangu mimi nimelazimisha tu na bora angeniambia kabla.
maswali ulioulizwa na wadau yakijibiwa, tutachangia
 
Back
Top Bottom